Jstrong
Member
- Mar 24, 2011
- 60
- 13
Kile kikundi cha UAMSHO kinachodai zanzibar huru kikidai hakitaki muungano sasa hivi kinatawanywa na FFU kwa mabomu ya machozi na risasi baada ya risasi kadhaa kupigwa hewani.
Wapo hapa Kisonge wakitaka kuelekea kituo cha polisi cha MKUNAZINI. Fujo hizi ni baada ya viongozi wao leo kukamatwa baada ya swala ya magharibi na leo walikua na mkutano eneo la Lumumba.
Mi sitaki kusema muungano uwepo au usiwepo,ila busara ingefanyika kuitisha kura ya maoni kwa wote kwamba uwepo ama la ili kuepusha shari,wenzetu wanafikiri wafanye nn kupiga hatua za kimaendeleo ss twapoteza muda na swala hili.