Zanzibar ni nchi: Dr Bilali arudi kwao

Watanzania said:
Acheni Zanzibar wajitenge ili kanuni ya historia aliyosema Mwalimu Kambarage itimie. Baada ya kujitenga watagundua kumbe siyo wamoja, kuna Wazanzibar na Wapemba. Dhambi ya ubaguzi itaendelea kuwatafuna hadi waone kumbe hata Zanzibar kuna wazanzibara na wanzanzibari. Wazanzibara wakiondolewa Zanzibar, Wazanzibar wataendelea kubaguana hadi mwisho. Wapemba nao itakuwa hivyohivyo, wataona kuna wapemba koko na wapemba weupe. Ubaguzi utaendelea hata wale weupe watajiona si wamoja, kuna wapemba wa Saudia, wapemba wa Oman na wapemba wa kireno. Watanganyika watendelea kuwa wamoja kwa kuwa hawatakuwa wametenda hiyo dhambi ya ubaguzi. Fanyeni haraka wazinzibar na wapemba kujitenga ili kanuni ya historia itimie.

Watanzania,

..mambo yakienda mrama Zanzibar, basi majirani zake wote wataathirika kwa namna moja au nyingine.

..wa-Tanganyika tunapaswa kuomba Zenj iwe na amani na maendeleo.
 
kwani hao Wazanzibari hakuna walioapa kulinda na kuitetea Katiba ya JMT? as a matter of fact wote kuanzia Karume na wenzake wameapa hivyo hivyo!!! ndiyo maana nimewaita ni wahaini.

Rais wa Zanzibar kawaida huapa kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kitu kinachosumbua hapa ni kwamba: Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaweza kuigawa Zanzibar katika Mikoa kwa kushirikiana na Rais wa Zanzibar, lakini mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar yanadai kwamba Rais wa Zanzibar atagawa Zanzibar katika mikoa bila kushauriana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, huko kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa Rais wa Zanzibar kuko wapi?
 
Sasa kama kwa kujitangaza nchi, Zanzibar haitakuwa inawajibika kwa serikali ya Muungano, hiyo JMT si itabaki ya bara tu? Kwa hali hiyo kwa nini tuwe na Makamu (ambaye atakuwa pigo moja tu la moyo kutoka urais) kutoka nchi nyingine? Itabidi vile vile iwekwe wzi kuwa mbunge nayetoka nchi moja asipewe nafasi ya uongozi katika serikali ya nchi nyingine! Itakuwaje raia wa Zanzibar apewe uwaziri katika JMT ambayo haina jurisdiction katika nchi yake?

Amandla......

Well said FM Amandla!!!
Hawa wazanzibari ndo wanayoyoma kuunda dola yao.Sasa sisi tusiwakumbatie tena na waende zao.
Na haswaa huku bara wanawawakilisha wazanzibari ili iweje maana kwa mantiki ya kuanzisha dola yao inayojitegemea, huku bara hawana haki ya uwakilishi na rasilmali za huku kwetu
 
Acheni Zanzibar wajitenge ili kanuni ya historia aliyosema Mwalimu Kambarage itimie. Baada ya kujitenga watagundua kumbe siyo wamoja, kuna Wazanzibar na Wapemba. Dhambi ya ubaguzi itaendelea kuwatafuna hadi waone kumbe hata Zanzibar kuna wazanzibara na wanzanzibari. Wazanzibara wakiondolewa Zanzibar, Wazanzibar wataendelea kubaguana hadi mwisho. Wapemba nao itakuwa hivyohivyo, wataona kuna wapemba koko na wapemba weupe. Ubaguzi utaendelea hata wale weupe watajiona si wamoja, kuna wapemba wa Saudia, wapemba wa Oman na wapemba wa kireno. Watanganyika watendelea kuwa wamoja kwa kuwa hawatakuwa wametenda hiyo dhambi ya ubaguzi. Fanyeni haraka wazinzibar na wapemba kujitenga ili kanuni ya historia itimie.

unazungumza kama vile umewekewa M!!! ya mdomo leo zanzibar ikijitowa kesho mtaanza kuchinjana kimakabila ,hamna ari kama kweli mnaari na hayo mnayoyasema mgekuwa mnapigania nchi yenu kama wanavyo fanya hao wazanzibar na kwahali hiyo mnaonesha kuwa nyie ndio wenywe issue zidi ya wazenj ,hivi juu ya ukubwa wa hiyo ardhi na mali zote ambazo mumekuwa nazo wachilia mbali hizo pesa mnazopita mkiomba omaba na hizo za kusaidiwa mnashindwa na nini kuwa kivyenu vyenu .wakati umefika mkangalia hatma ya Tanganyika nayo (kila mtu hulia Mama Yangu na hali mama yetu unapokuwa msiba amkane wakati umefika hamuishi tena maisha ya Nyerere manishi maisha yenu)
 
Labda Zanzibabr itakuwa singapore ya afrika ya mashariki, waache watafute maendeleo. Kuwamo kwao kwenye muungano kumewafanya wrudi nyuma hasa ukizingatia kuwa viongozi wa kutoka Tanganyika ni mafisadi tu. Katika kesi zote za ufisadi, sijasikia kiongozi yeyote wa kutoka Zanzibar akihusishwa ukiachilia yale yaliyompata Rais mwinyi miaka mingi iliyopita wakati wa ulezi wa mama Siti ambaye nasikia siku hizi alishahamia uarabuni (sina uhakika na hilo).
 
Labda Zanzibabr itakuwa singapore ya afrika ya mashariki, waache watafute maendeleo. Kuwamo kwao kwenye muungano kumewafanya wrudi nyuma hasa ukizingatia kuwa viongozi wa kutoka Tanganyika ni mafisadi tu. Katika kesi zote za ufisadi, sijasikia kiongozi yeyote wa kutoka Zanzibar akihusishwa ukiachilia yale yaliyompata Rais mwinyi miaka mingi iliyopita wakati wa ulezi wa mama Siti ambaye nasikia siku hizi alishahamia uarabuni (sina uhakika na hilo).

Swadakta.

Wabara wengi eti wanasema Znz ni mzigo lakini at the same time ati wanawalaumu kwa kutaka kuanzisha mgogoro wa kikatiba (ili wavunje Muungano). Muungano ambao mimi sioni faida yake. Nilidhani ilikuwa wakti muafaka kwa wabara kuwaunga mkono hao 'wavunja Muungano' ili wautue 'mzigo'!

I still believe Znz itapiga hatua sana ikijiondoa kwene makucha ya hawa mafisadi wa bara. Kwa udogo wao watakuwa na urahisi wa kujiendesha na kujimanage vyema zaidi ikiwa watapata uongozi imara wenye nia ya dhati ya kuondoa ufukara wa kujitakia.
 
Swadakta.

Wabara wengi eti wanasema Znz ni mzigo lakini at the same time ati wanawalaumu kwa kutaka kuanzisha mgogoro wa kikatiba (ili wavunje Muungano). Muungano ambao mimi sioni faida yake. Nilidhani ilikuwa wakti muafaka kwa wabara kuwaunga mkono hao 'wavunja Muungano' ili wautue 'mzigo'!

I still believe Znz itapiga hatua sana ikijiondoa kwene makucha ya hawa mafisadi wa bara. Kwa udogo wao watakuwa na urahisi wa kujiendesha na kujimanage vyema zaidi ikiwa watapata uongozi imara wenye nia ya dhati ya kuondoa ufukara wa kujitakia.

Kwa hilo nakuunga mkono Abdulhalim;

Wa-ZNZ hawana hulka ya"udokozi"kama ilivyo kwa wa Bara pindi wakipata madaraka!Mwinyi alikuwa Rais wa Jamhuri lkn hatajwi kwenye uwizi wa kujilimbikizia mamilion ya dola kama hawa wenzake wa Bara !

Mzee Jumbe anaishi maisha ya kawaida kabisa kule kijijini kwake Mji mwema;Mwinyi yupo tu akitegemea mafao yake anayolipwa kihalali na serikali;Mzee Wakili alikufa akiwa hana mali yeyote kubwa ya kujivunia;Mzee Salmim nae maisha yake yanategemea mafao ya serikali kama itakavyokuwa kwa Rais Karume nae akiaga;hata ma-Waziri wake viongozi nao wana sifa za kutopenda makuu!

Viongozi wa TZ toka Bara wameipaka sana matope Tanganyika yetu;alichokifanya Mkapa na wenzake hamna asiyejua.Mramba na Karamagi;Lowasa na Rostam na hata pair ya Msabaha na Chenge ambaye alifikia kuwa na zaidi ya dola milion 1 kwenye akiba yake ya siri nje ya TZ ni baadhi tu ya Wa-bara walionichefua!

Lkn sifa za kutokuwa "wadokozi" ndiyo iwe kibali cha ZNZ kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu yangu Abdulhalim?
 
Lkn sifa za kutokuwa "wadokozi" ndiyo iwe kibali cha ZNZ kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu yangu Abdulhalim?

Malafyale,

Mie daima concern yangu ipo kwa mwananchi wa kawaida. Hawa ndio shida yangu kubwa, kama watasaidiwa kihali kwa kupitia muungano sidhani kama kuna tatizo au kungekuwa na tatizo, lakini kinyume chake ni tatizo kubwa. Kuna msomi mmoja anasema mapinduzi mara nyingi ni 90% economical na only 10% political, huhitaji kuwa na darubini ya kupima mwendo wa galaxies kuona mantiki ya hii philosophical statement . The same argument tumejaribu kuiongelea kule kwenye EAC, if the common mwananchi is excluded kwene kushika uchumi wa nchi yake then we have a problem. Na hii ndio hali inayojitokeza. Viongozi tulionao na mfumo uliopo, they failed us, sio Znz peke yake, hata huko bara, mwananchi wa kawaida amepigika huku wachache wakila keki ya taifa kwa kebehi na ujeuri, sasa sioni tatizo kwanini waZnz wasijaribu kuchukua mdhamana wa mustakabali wao, na sasa nadhani ni wakti muafaka, ngoja ngoja mwishoe mja huishia kufukiwa futi 6 chini ya ardhi bila kuonja utamu wa halua!
 
''I still believe Znz itapiga hatua sana ikijiondoa kwene makucha ya hawa mafisadi wa bara. Kwa udogo wao watakuwa na urahisi wa kujiendesha na kujimanage vyema zaidi ikiwa watapata uongozi imara wenye nia ya dhati ya kuondoa ufukara wa kujitakia.''

Abdulhalim, kama udogo ni maendeleo, ni yapi yaliyopatikana Haiti, Kiribati, Tonga na fiji, Bhutan, Togo,Burundi, Eritrea n.k
Kama udogo ndiyo njia ya kujimanage vipi wapemba wadai kujitoa SMZ, hapo management imesaidia nini.
Kama mafisadi ndio chanzo cha kuvunja muungano mbona hili halisemwi wazi ili tujue muungano haupo. Je ni kwanini Wznz wanalalamika kuwa Mh Rais wa nchi yao amemilikisha uchumi kwa familia yake kama inavyodaiwa sasa?
Abdu, kwanini znz wasiombe kura ya maoni ili tujue kama tumeamua kuvunja jahazi na tunagawana mbao, na iwe hivyo.?
 
''I still believe Znz itapiga hatua sana ikijiondoa kwene makucha ya hawa mafisadi wa bara. Kwa udogo wao watakuwa na urahisi wa kujiendesha na kujimanage vyema zaidi ikiwa watapata uongozi imara wenye nia ya dhati ya kuondoa ufukara wa kujitakia.''

Abdulhalim, kama udogo ni maendeleo, ni yapi yaliyopatikana Haiti, Kiribati, Tonga na fiji, Bhutan, Togo,Burundi, Eritrea n.k
Kama udogo ndiyo njia ya kujimanage vipi wapemba wadai kujitoa SMZ, hapo management imesaidia nini.
Kama mafisadi ndio chanzo cha kuvunja muungano mbona hili halisemwi wazi ili tujue muungano haupo. Je ni kwanini Wznz wanalalamika kuwa Mh Rais wa nchi yao amemilikisha uchumi kwa familia yake kama inavyodaiwa sasa?
Abdu, kwanini znz wasiombe kura ya maoni ili tujue kama tumeamua kuvunja jahazi na tunagawana mbao, na iwe hivyo.?

Bwana mkubwa Nguruvi3,

Sijasema popote kwamba, udogo == maendeleo, ichukue nukuu na uielewe kwanza kabla ya kuigeuza na kuijengea hoja. Kwa kuelezea zaidi mtazamo wangu ni kwamba uongozi bora ndio kitu cha kwanza, shurti kuepo na hawa kwanza. Wakiwepo wataokoa mifarakano na matatizo mengi ya kujitakia yanayoambatana na ubinafsi na ulafi. Sijasema kwamba hivi sasa wanao uongozi bora, lakini kwa courage waliyoionesha na michakato waliyoianza, naamini wapo njia moja kumjua mchawi wao, na hii ni dalili njema ya kuwaondoa wachakachuaji wote wasiojali maslahi ya wazanzibari.

Mie sio msemaji wa SMZ lakini sioni kwanini pesa iteketezwe ili kujua the obvious.
 
Swadakta.

Wabara wengi eti wanasema Znz ni mzigo lakini at the same time ati wanawalaumu kwa kutaka kuanzisha mgogoro wa kikatiba (ili wavunje Muungano). Muungano ambao mimi sioni faida yake. Nilidhani ilikuwa wakti muafaka kwa wabara kuwaunga mkono hao 'wavunja Muungano' ili wautue 'mzigo'!

I still believe Znz itapiga hatua sana ikijiondoa kwene makucha ya hawa mafisadi wa bara. Kwa udogo wao watakuwa na urahisi wa kujiendesha na kujimanage vyema zaidi ikiwa watapata uongozi imara wenye nia ya dhati ya kuondoa ufukara wa kujitakia.


Mkuu hayo maneno niliyo bold ndio jambo la kujiuliza; hao wanaoandaa kujitenga sasa wana nia gani? huwa tunawaamini bila kujua nini malengo yao binafsi
 
Mkuu hayo maneno niliyo bold ndio jambo la kujiuliza; hao wanaoandaa kujitenga sasa wana nia gani? huwa tunawaamini bila kujua nini malengo yao binafsi

Ndugu wenye malengo binafsi hamuwaoni huko kwenu bara?
 
embu tusome KATIBA ya Nchi yetu jamani tuelewe mambo,maneno ya Hayati Baba wa Taifa pia tuyazingatie.wanaosherekea kuvunjika kwa Muungano wetu sidhani kama wameshaisoma historia ya nchi hii.tuachane na majarida/magazeti ya UDAKU tutafika mbali Watanzania
 
Hakuna yeyote anayeumia Zanzibar kuitwa nchi au vinginevyo. Tatizo ni mkanganyiko dani ya katiba zote mbili. Jambo hili linaweza kulete mtafaruku wa kisheria na kiutawala. Mwanasheria mkuu alitolee maelezo ili sote tuelewe vizuri maana ukiona jambo linazungumzwa na wengi tena wenye uelewa wa mambo si vizuri kukaa kimya.
 
embu tusome KATIBA ya Nchi yetu jamani tuelewe mambo,maneno ya Hayati Baba wa Taifa pia tuyazingatie.wanaosherekea kuvunjika kwa Muungano wetu sidhani kama wameshaisoma historia ya nchi hii.tuachane na majarida/magazeti ya UDAKU tutafika mbali Watanzania
Nipo.na wewe mkuu,lakini hayo ni mawazo ya Mtanzania Bara, mtu mwenye nia njema na muungano.
Mkuu mambo haya SI UDAKU,leo hii Mwanasheria Mkuu,custodian wa Katiba ameshimdwa kuelezea maana halisi ya mabadiliko ya katiba ya Zanzibar(NIPASHE),na jinsi inavyo athiri muungano.
Mzee Mwanakijiji humuhumu jamvini amependekeza kuliona suala la vipengele vinavyokiuka muungano kuwa Uhaini, that is how serious the issue is.
Ufa mkubwa umeingia muungano,hatua hazichukuliwi kuuziba!
Sasa kama alivypsema hayati Baba wa Taifa,imeshakuwa WAO Wazanzibari na SISI Watanganyika.Kwa ubaguzi huu Wazenj warudi Nchini kwao
 
Anayesema wa Zanzibari si wadokozi nani? Shida ni kuwa hakuna cha kudokoa. Lakini hata kwenye hicho kidogo wameiba sana ila hawavumi tu. Viongozi wao wamehodhi ardhi, wafanyabiashara hawalipi kodi n.k. Wanaoiba wote wanaenda kujenga bara. Wapemba waliojenga bara wangewekeza kwao, wangekuwa mbali sana.

Mnaosema kuwa wakiachiwa watakuwa Singapore nyingine mbona hamuangalii walivyofanya pale walipoachiwa? Walipiga kelele wakitaka wawe na mamlaka yao yenyewe ya bandari. Wakaachiwa. Mbona bandari yenyewe haijageuka Rotterdam nyingine? Wana mamlaka kamili juu ya uwanja wao wa ndege. Koko wapi kilichoendelea. Wana mamlaka kamili kuhusu zao lao la karafuu. Leo liko wapi? Wana mamlaka kamili kuhusu utalii. Nako wako wapi? Cha msingi ni kuwa hulka yao si ya maendeleo. Sitoshangaa badala ya kuwa Singapore watageuka Haiti nyingine. Lakini pamoja na yote hayo, watangaze wazi bila kumung'unya maneno kuwa hawautaki Muungano, waende zao. Future yao iwe mikononi mwao.

Kinachonisikitisha katika mjadala huu ni hizi hisia kuwa kuvunjika Muungano ina maana kufukuzana. Watu tumeoleana, tutafukuzana vipi? Tuvunje Muungano lakini tuendelee kuishi kwa amani. Wazanzibari watakaotaka kuishi Bongo waruhusiwe bila kubughudhiwa ili mradi wafuate taratibu kama wahamiaji wengine. Vile vile kwa wabongo wanaotaka kuishi Zanzibar. Tusiendeleze chuki , itatufikisha pabaya.

Amandla.......
 
Anayesema wa Zanzibari si wadokozi nani? Shida ni kuwa hakuna cha kudokoa. Lakini hata kwenye hicho kidogo wameiba sana ila hawavumi tu. Viongozi wao wamehodhi ardhi, wafanyabiashara hawalipi kodi n.k. Wanaoiba wote wanaenda kujenga bara. Wapemba waliojenga bara wangewekeza kwao, wangekuwa mbali sana.

Mnaosema kuwa wakiachiwa watakuwa Singapore nyingine mbona hamuangalii walivyofanya pale walipoachiwa? Walipiga kelele wakitaka wawe na mamlaka yao yenyewe ya bandari. Wakaachiwa. Mbona bandari yenyewe haijageuka Rotterdam nyingine? Wana mamlaka kamili juu ya uwanja wao wa ndege. Koko wapi kilichoendelea. Wana mamlaka kamili kuhusu zao lao la karafuu. Leo liko wapi? Wana mamlaka kamili kuhusu utalii. Nako wako wapi? Cha msingi ni kuwa hulka yao si ya maendeleo. Sitoshangaa badala ya kuwa Singapore watageuka Haiti nyingine. Lakini pamoja na yote hayo, watangaze wazi bila kumung'unya maneno kuwa hawautaki Muungano, waende zao. Future yao iwe mikononi mwao.

Kinachonisikitisha katika mjadala huu ni hizi hisia kuwa kuvunjika Muungano ina maana kufukuzana. Watu tumeoleana, tutafukuzana vipi? Tuvunje Muungano lakini tuendelee kuishi kwa amani. Wazanzibari watakaotaka kuishi Bongo waruhusiwe bila kubughudhiwa ili mradi wafuate taratibu kama wahamiaji wengine. Vile vile kwa wabongo wanaotaka kuishi Zanzibar. Tusiendeleze chuki , itatufikisha pabaya.

Amandla.......
Mkuu FM Amandla!!
Nakubaliana na wewe kabisa kwa observation yako ya hali tuliyo nayo na ile ambayo tungependa iwe.
Hapo mwanzo nilisema hii mada ni kiuchokozi kimawazo na nafikiri tunasonga mbele na kujua yale yatakayo jiri huko mbeleni.
The natural gut feeling kwa wabara ni kutaka hawa wenzetu watokomee mbali kama muungano ukivunjika.
Wishful thinking and wishing for the best never helped anybody
Kwa bahati mbaya , kutokana na historia ya binadamu, UENDO na CHUKI ni mtu na pacha wake.Ndugu na ndugu wakigombana hapo pana shetani,uamuzi wake huwa wa utata sana.
Ndio maana Mzee Mwanakijiji alitonya katika mada yake kuwa kuchezea muungano ni UHAINI.
Kuna mifano kadhaa ambayo inaelezea hali kama ya kwetu sisi hapa.
Urusi na Georgia,China Mainland na Taiwan, India na Pakistan, Korea Kaskazini na Kusini, na sasa tunaona hata Sudan Kusini na Kaskazini.
Hali hii inakuja kwetu, na mimi sioni hatua zozote kuchuliwa kuokoa mtelezo wa matukio yanavyozidi kudidimiza muungano.
 
Kwa mabadiliko haya rais wa JMT hana nguvu huko Zanzibar, OK, bado anamiliki Jeshi la Polisi na JWTZ. Pengine hivi ndo vinamfanya Kikwete akae kimya tu. Lakini mambo haya huwa yanaanzia kwenye maandishi. Kwa nini wameona ni muhimu kutamka kuwa Zanzibar ni nchi na mipaka yake ni hii? Wanataka Mwingine aseme Tanganyika ni nchi na eneo lake ni hili. Lengo lao; kulazimisha tuingie kwenye ufederali, yaani serikali tatu. Lakini Tukishaunda Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Muungano ni kwisha! Itakuwa serikali isiyo na NGUVU ikiwa na wizara chache tu zenye mambo ya muungano;i.e. ulinzi na usalama, mambo ya nje, mambo ya ndani, n.k.

Wazanzibari wamekuwa wakilalamika mambo ya Tanganyika kushughulikiwa na serikali ya muungano moja kwa moja kwa sababu hiyo inawafanya Watanganyika wai-dominate serikali ya muungano kwani mambo yao mengine yamo ndani ya muungano. Hivyo wazanzibari wangependa kuona kukiwa na separation kati ya serikali ya muungano na ya Tanganyika basi kile kiburi cha Watanganyika ndani ya serikali ya muungano kitaisha, itabidi nguvu iwe sawa..... Sasa nguvu ikiwa sawa kwenye serikali ya muungano, itabidi na gharama ya kuiendesha ichangiwe sawa; Kukishakuwepo serikali ya Tanganyika haitakubali kutoa asilimia 99 ya gharama za kuendesha serikali ambayo mtu anayechangia asilimia moja anakuwa na nguvu sawa. Hapa ndo kifo cha muungano kitakapotokea.

Lakini vile vile itakuwa vigumu kuyaridhisha haya mabadiliko ya sasa ya katiba ya Zanzibar bila kuiweka serikali ya Tanganyika. Viongozi wetu wanaweza kuamua kukaa kimya lakini ukweli UTAENDELEA KUWATOLEA MACHO na iko siku utawatafuna!!
 
Back
Top Bottom