Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
kwa kweli tunakoelekea kunatisha, likiisha hili linaibuliwa hili:
Serikali ya mapinduzi Zanzibar imesema hakuna uwiano wa kutosha katika nafasi za kazi za utendaji kwenye afisi za kibalozi nje ya nchi kati ya vijana wa Zanzibar na Tanzania bara.
Waziri wa nchi afisi ya makamu wa pili wa rais Mohammed Aboud amesema tatizo hilo ni moja ya kero za muungano zinazoshughulikiwa ili wanzanibari waweze kuajiriwa katika afaisi hizo.
Akijibu suala katika kikao cha baraza la wawakilishi amesema serikali imeona upo umuhimu kwa nafasi za ajira katika ofisi za kibalozi kuajiriwa kwa usawa kati ya vijana wa Zanzibar na Tanzania bara. Hata hivyo waziri Aboud amesema kuchelewa kuyapatia ufumbuzi matatizo ya muungano likiwemo suala hilo kunaweza kuwafanya wazanzibari kutokuwa na imani kwa vile hawafaidiki na matunda ya muungano.
source: HAKUNA UWIANO WA UAJIRI NAFASI ZA KIBALOZI | Mzalendo.net