Zanzibar kunyimwa 'Change ya RADA'

Wanabodi,
Msipokuwa na majibu sahihi ni bora kabisa kukaa kimya kuliko kukisia ama kuleta Ubishi usiokuwa na maana. Chenji ya Rada ni UFISADI mkubwa ulofanyika na hata kama zimegawiwa bara sielewi zimegawiwa vipi kiasi kwamba haya madai yawe na ukweli wowote. Rada ilinunuliwa kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni swala la Kitaifa na tumelipwa kwa jina la mfuko wa Taifa hivyo hata matumizi yake ni ya serikali ya Muungano.

Tatizo linalowakumba Wazanzibar wengi ni pale wanaposikia serikali ya Muungano basi lazima hiyo iwe inazungumzia bara tu, lakini wasichokifahamu ni kwamba Bunge la Taifa Dodoma linawashirikisha Wazanzibar, Utawala wa serikali yetu wamo Wazanzibar kwa manufaa ya pande zote mbili na hata ukitazama Kamati kuu ya chama tawala imejaa Wazanzibar - Huo mseto walounda Zanzibar majuzi unatumika Bara toka mwaka 1964 ktk serikali yetu ya muungano. Matumizi yote yanalipwa na kodi za wananchi wa pande mbili, Bara ikichangia zaidi kwa kila kitu. Sasa iweje fedha hizi zipelekwe ktk serikali ya (mseto) Mapinduzi wakati ni fedha za Muungano?..

Mkandara, hivi kwa mfano ukatokea wizi kwenye mji wa Mkandara, baada ya msako mali ikandulika iko wapi na kurudishwa nyumbani kwa Mkandara, lakini ndani ya huo mji mali ilikuwa ya Juma Mkandara na sio Juma na nduguye aitwaye Abadala. Sasa, Abdallah ana haki ya kupata kiasi cha mali hiyo iliyorudi hata kama huko nyuma hakushiriki kuinunua?

Swali la RADA liliulizwa bungeni na mwanasheria mkuu alifananua. Hata hivyo Rada ilinunuliwa na Jamhuri ya Tanzania (Mkandara) na hasa mtu aliyelipia ni Wizara ya Uchukuzi-Tanzania Bara (Juma Mkandara). Sasa chenji ya wizi imerudi, Abdallah anataka gawio! Wakati huo huo kumbuka ilinunuliwa na mkopo na hivyo mlipaji wa huo mkopo na Tanzania bara (Juma Mkandara). Kama Abdalla atataka gawio, hakuna shida lakini pia awe tayari kuchangia hela za kununua/mkopo.

Hii mambo mseto haibalishi equation.
 
Kunyimwa misaada?

OIC ndio maana ni muhimu kwa Zanzibar ili na yenyewe isikose misaada kwasababu Maaskofu (wa Tanganyika hawataki)

Lazima kukubali kubeba risks (of each) kwenye umoja..

Topical,

..si Iran, wala OIC, wanaoweza kubeba mzigo wa kufadhili bajeti ya Tanzania by 30%.

..ndiyo maana nikasema Zanzibar wapeperushe bendera yao wenyewe kutuepusha wa-Tanganyika na zahama ya vikwazo vya USA na ndugu zake wa NATO.
 
Wakuu heshima mbele sana,

Kumekuwa na sintofahamu nyingi sana mara baada ya Serikali kwa bahati mbaya au makusudi kugawa fedha ya change ya Rada Tanzania bara pekee na Tanzania visiwani kutokupata hata centi moja, Wabunge wengi wa Zanzibar wameonekana kutokupendezwa na swala hili, Je ni sahihi kwa mgawo wa Rada kugawanywa bara pekee na si visiwani..?

Kwa kutumia common sense si sahihi kabisa. If I may ask zaidi ya location hivi matumizi ya rad a yalilenga upande wa bara pekee?
 
Watanzania wenzangu nawashangaa sana chenji ya rada kivipi semeni ukweli NI CHENJI YA RUSHWA kabla ya kujadili.
 
Wakuu heshima mbele sana,

Kumekuwa na sintofahamu nyingi sana mara baada ya Serikali kwa bahati mbaya au makusudi kugawa fedha ya change ya Rada Tanzania bara pekee na Tanzania visiwani kutokupata hata centi moja, Wabunge wengi wa Zanzibar wameonekana kutokupendezwa na swala hili, Je ni sahihi kwa mgawo wa Rada kugawanywa bara pekee na si visiwani..?
Sr. Magdalena, japo wengi wamekujibu kuwa Rada sio issue ya muungano, wamekosea!. Ukweli ni huu!.
1. Rada ni suala la muungano!. Japo rada ile ilinunuliwa kwa Watanzania kudanganywa kuwa ni rada ya kiraia!, kiukweli radar ile ni radar ya kijeshi iliyotumia "obsolate" technology na ndio maana ilisababisha kelele sana toka kwa nchi wafadhili!. Ulinzi na usalama ni suala la muungano!.

2. Jee rada hiyo ilinunuliwa na nani na inasimamiwa na nani?. Rada ilinunuliwa na Mamlaka ya Usalama wa Anga, TCAA na kusimamiwa na mamlaka hiyo hiyo!. Mamlaka ya Usalama wa Anga ni ya Muungano!. Hivyo rada ni ya muungano!.

3. Jee fedha za rada zilitoka wapi?. Fedha za rada zilichotwa toka mfuko mkuu wa hazina na zilikopwa toka benki ya Stanbic ya Uingereza hivyo fedha hizo ni sehemu ya deni la Taifa!. Mfuko mkuu wa hazina ni suala la muungano!.

4. Mgawo wa fedha hizi ni uthibitisho wa matatizo ya structure ya muungano kwani wakati zinachotwa, zimechotwa mfuko mkuu wa hazina ambao ni wa muungano na zikawa executed kupitia wizara ya mawasiliano na uchukuzi ambayo siyo ya muungano lakini Mamlaka ya Usalama wa Anga, TCAA ambayo ni taasisi ya Muungano iko chini ya wizara ambayo sio ya muungano!.

4. Wakati wa kurudishwa kwa fedha hizo, government negotioation team iliongozwa na wizara ya mambo ya nje ambayo ni ya muungano na the lobby group ni Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ambayo pia ni ya muunngano!.

5. Ilikubaliwa kuwa fedha hizo zitumike kuimarisha elimu ya msingi ambayo sio ya muungano!. This is an oversight!. Wabunge wako right kutetea haki za Zanzibar kupata mgao huo!.

6. Wizara zote ambazo sio za Muungano ikiwemo Wizara ya Uchukuzi, zinasimamia vipi taasisi za Muungano kama Mamlaka ya Usafiri wa Anga, Mamlaka ya Hali ya Hewa na Shirika la Ndege la Tanzania?!.

7. Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia sio wizara ya muungano, lakini ndio inayosimamia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, TCRA ambayo ni taasisi ya Muungano?!.

8. Tukubali tukatae, muungano wetu unatatizo la imbalance kwa Zanzibar kujiona kama equal part ya muungano!, huku sisi bara tukiiona Zanzibar kama sehemu tuu ya muungano ambayo kama mkoa fulani!.

9. Tufike mahali ama Zanzibar ipatiwe haki zake zote stahili ndani ya muungano or let Zanzibar Go! ili sasa ijibebe!. Japo tumechoka kuibeba, lakini Zanzibar sasa sio tuu ni mtoto mtukutu, bali ni toto tundu!. Jee mtoto wako mwenyewe uliyembeba kwenye mbeleko, akianza utukutu na kukupiga mateke huku akieusha rusha miguu umshushe, jee utambwaga chini, au utamshusha taratibu?!.

10. Tanzania kama mama imeibeba sana Zanzibar kwenye mbeleko ya muungano kama mtoto mdogo kwa muda mrefu!. Lakini kwa vile mtoto hiyu hajiwezi kwa lolote wala chochote!, hata apige kelele vipi huku akirusha rusha miguu!. Kamwe hatutambwaga chini mtoto wetu, bali tutamtia adabu tuu!, not to let Zanzibar Go!.
 
Pasco,

..majibu ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda haya hapa chini.

Alisema kwa msingi huo fedha hizo zitatumika kununua vitabu na madawati na pia hazitapelekwa Zanzibar kwa vile ununuzi wa rada ulifanywa na Sekta ya Mawasiliano ya Wizara ya Miundombinu ambayo siyo ya Muungano na siyo Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambayo ni miongoni za Wizara za Muungano.
 
2. Jee rada hiyo ilinunuliwa na nani na inasimamiwa na nani?. Rada ilinunuliwa na Mamlaka ya Usalama wa Anga, TCAA na kusimamiwa na mamlaka hiyo hiyo!. Mamlaka ya Usalama wa Anga ni ya Muungano!. Hivyo rada ni ya muungano!.

3. Jee fedha za rada zilitoka wapi?. Fedha za rada zilichotwa toka mfuko mkuu wa hazina na zilikopwa toka benki ya Stanbic ya Uingereza hivyo fedha hizo ni sehemu ya deni la Taifa!. Mfuko mkuu wa hazina ni suala la muungano!.


7. Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia sio wizara ya muungano, lakini ndio inayosimamia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, TCRA ambayo ni taasisi ya Muungano?!.

!.

Pasco,
No 2, TCAA ni sawa na TRA when it comes to Muungano. Wizara ya uchukuzi Zanzibar wamenyofoa mambo mengi sana.

No 3, deni lilochukuliwa na Jamhuri ya muungano wa Tanzania, anayelipa ni Tanganyika! Hivyo kama ni kugawana chenji ya wizi pia tugawane mrejesho wa deni.

No 7, Wizara ya Science na Technology imekuwa added kwenye mambo ya muungano - check hansard za bunge utapata majibu ya Mh Samia Suluhu. Kumbuka posta iko chini ya hii wizara. Mapema mwezi uliopita moja ya idara ya hii wizara wamezindua office zao kwenye jengo jipya la office ya Makamu wa Rais- Muungano huko Tunguu, Unguja.
 
Sr.Magdalena,

..Ulinzi ni suala la muungano, lakini kwa kawaida ZNZ huwa haichangii chochote ktk masuala ya muungano.
..kabla ya kulalamika, wabunge wa ZNZ wangeeleza wakati rada inanunuliwa ZNZ walitoa kiasi gani toka hazina yao. inajulikana kwamba makusanyo yote ya TRA Zanzibar hubakia hukohuko...mbona hatujasikia ZNZ wakililia kushirikishwa ktk kulipa madeni ya nje, kila siku ni kelele za kudai misaada na mgao??
..LET ZANZIBAR GO!!!
Mkuu Joka Kuu, unayo anwani ya wabunge wa ZNZ kule Dodoma, ningependa kukipeleka kipande hiki wakisomea. Waooo! LET ZNZ GO ASAP!
 
Change ya Rada si suala la muungano.

Mkuu Ngongo hebu twende taratibu. Katika kutetea bei kubwa ya rada ilisemwa kuwa hiyo rada inatumika pia katika masuala ya kiulinzi; Ulinzi siyo suala la Muungano? Kama Rada inalinda mipaka ya nchi na kung'amua ndege zinazoingia kwenye anga la Tanzania inakuwaje Rada isiwe jambo la Muungano; kukana kuwa si suala la muungano kunamaanisha kuwa anga ya Zanzibar si ya Muungano!!! Kizungumkuti tu hiki!
 
Last edited by a moderator:
Wakuu heshima mbele sana,

Kumekuwa na sintofahamu nyingi sana mara baada ya Serikali kwa bahati mbaya au makusudi kugawa fedha ya change ya Rada Tanzania bara pekee na Tanzania visiwani kutokupata hata centi moja, Wabunge wengi wa Zanzibar wameonekana kutokupendezwa na swala hili, Je ni sahihi kwa mgawo wa Rada kugawanywa bara pekee na si visiwani..?

.
Kwani wao Zenji wameuza bendera yetu kupeperushwa na meli za Iran kwa bei gani? Wametupa mgawo sisi wabara?
.
 
Mkandara, hivi kwa mfano ukatokea wizi kwenye mji wa Mkandara, baada ya msako mali ikandulika iko wapi na kurudishwa nyumbani kwa Mkandara, lakini ndani ya huo mji mali ilikuwa ya Juma Mkandara na sio Juma na nduguye aitwaye Abadala. Sasa, Abdallah ana haki ya kupata kiasi cha mali hiyo iliyorudi hata kama huko nyuma hakushiriki kuinunua?

Swali la RADA liliulizwa bungeni na mwanasheria mkuu alifananua. Hata hivyo Rada ilinunuliwa na Jamhuri ya Tanzania (Mkandara) na hasa mtu aliyelipia ni Wizara ya Uchukuzi-Tanzania Bara (Juma Mkandara). Sasa chenji ya wizi imerudi, Abdallah anataka gawio! Wakati huo huo kumbuka ilinunuliwa na mkopo na hivyo mlipaji wa huo mkopo na Tanzania bara (Juma Mkandara). Kama Abdalla atataka gawio, hakuna shida lakini pia awe tayari kuchangia hela za kununua/mkopo.

Hii mambo mseto haibalishi equation.
Mkuu wangu tafadhali.... Kwanza labda nianze na kusema hakuna mtu anayeitwa Juma Mkandara! kwa maana kwamba hakuna mkopo wala malipo yanayofanywa na serikali ya Bara - hakuna kwa sababu hatuna serikali ya bara isipokuwa ya Muungano. Na hiyo serikali ya Muungano Zanzibar imo kwa hiyo kama kuna marejesho yoyote ya fedha zile za Rada inatakiwa kutumiwa kwa ujenzi wa Tanzania na sii bara, hivyo moja kwa moja Zanzibar inahusika.

Tatizo tulokuwa nalo nchini ni kwamba watu woote wanaojua asili ya Muungano wetu ulikuwaje wameisha kufa! na kama wapo hai basi ni wazee waliopoteza hata kumbukumbu. Na kibaya zaidi sisi waafrika na hasa Watanzania tuna asili ya kusahau, tuna utamaduni wa kutotunza nyaraka muhimu za Kitaifa kama urithi wa kizazi kijacho. Lakini madai mengi ya Zanzibar ni halali isipokuwa tatizo la muungano wetu halielezi kwa ufasaha nini sheria, tozo/fungu la Zanzibar ktk mchango wake ktk Jamhuri. Yapi ya zanzibar na yapi ya Bara (maana haipo). Kutokuwepo serikali ya Tanganyika kumezua utata zaidi kikatiba, sheria na kiuchumi ktk mchakato wa mapato na matumizi yake.

Angalia basi, maswala yote ya Kitaifa (Jamhuri) yanazihusu nchi zote mbili japokuwa Tanganyika haipo..Na ukitazama kwa makini bunge letu la Jamhuri lipo kutunga sheria na kupitisha bajeti ya Jamhuri. Makadiirio yote ya mapato yanajumlisha mikopo na ukusanyaji wa kodi za wananchi wa pande zote mbili lakini ajabu hapo hapo kuna ibara ya katiba ya Jamuhuri ya Muungano inasema kuwa - mamlaka yote ya kutunga sheria Tanzania, mambo yote yasiyokuwa ya Muungano yatakuwa mikononi mwa Baraza La Wawakilishi. Hili ni baraza la Zanzibar halipo bara wala ktk serikali ya Jamhuri hivyo tunagonganisha sheria mbili hapa.

Kuna sheria za Zanzibar ktk maswala yasiyokuwa ya muungano lakini hayo hayo yasiyokuwa ya Muungano hayana serikali Bara kuyatungia sheria za bara tu maana hatuna bunge la kutunga sheria za Bara tu. Hivyo tunashindwa kuelewa ni sheria zipi zitumike Zanzibar maana kuna wawakilishi wake ktk bunge la Jamhuri ambao wanapitisha Sheria ambazo zilitakiwa kuwa za States ya bara tu ila zote zinakuwa za Kitaifa wakati hazitambuliwi Zanzibar.

Huku Majuu ingejulikana wazi kwamba jambo lolote linalozungumziwa bungeni linahusu tu serikali ya Jamhuri ya Muungano. Hawawezi kutunga sheria yoyote isiyohusiana na Jamhuri nzima wala kupitisha bajeti isiyohusiana na serikali ya Jamhuri. Maswala yote yasiyokuwa ya muungano hayaruhusiwi kujadiliwa ktk bunge la Jamhuri, kila state ingekuwa na sheria yake, bajeti yake halafu ndio unakuta bunge la Jamhuri ambalo linazungumzia maswala ya Muungano tu.

Vivyi hivyo ukienda ktk maswala mengine yote yanayosemwa sii ya Muungano utakuta yanajadiliwa ktk bunge letu wakati Haiwahusu Zanzibar maana wao wanawajibika na sheria za state lakini hutuwezi kuwaacha Bara bila sheria hivyo inajadiliwa na kupitishwa na bunge la Taifa - kuwafunga Zanzibar ktk sheria mpya ilihali hili lilikuwa swala la states kuamua sheria gani itumike. Kama fedha ya rada imetoka ktk wizara ya miundombinu lakini bajeti ya taifa ndio iliyotumika kuorodhesha fedha hizo. Bajeti ambayo inakusanya kodi za watu wa pande zote mbili hivyo sii swala la kupangiwa wizara au shirika la Umma bali fedha hiizo zimetoka na kozdi za wananchi wote ndio msingi wa malalamiko ya Wazanzibar. Ndio maana tumekuwa na migogoro ktk Zanzibar kwa sababu sheria zetu zinaingilia maswala yasiyokuwa ya muugano.

Ili kuondoka na utata huu, tunalazimika kuunda serikali ya Bara, kuwepo na serikali tatu yaani ya bara, visiwani na ile ya jamhuri hivyo sheria zinapotungwa tunajua fika ukienda Zanzibar kuna bendera ya Zanzibar yenyebsheria zake nje ya sheria ya Bara, halafu tuna sheria za Kitaifa ambazo zinatuhusu wote.

Haya maswala ya Zanzibar kurusha bendera yetu kwa shirika la Iran kusema kweli binafsi yangu naona ni ujinga mtupu hata kulijadili. Sisi ni nchi iliyo Huru na tunaweza kabisa chagua marafiki zetu na nani maadui zetu. Na hakika kuzaliwa kwa nchi huru ya Tanzania kumetokana na kutangaza vita dhidi ya mambo manne nayo ni kupinga - UKOLONI, UKOLONI MAMBOLEO, UBEBERU na UBAGUZI wa aina yoyote ile. Sasa tunakuja leo kuungana na wale wale tulotutawala sisi kwa zaidi ya miaka sijui 200 au 500 kwa dhamira yao ile ile ya Ukoloni, mamboleo, ubeberu na ubaguzi wakitukabidhi sisi bakora ya Unyapala.. Sijui inatuweka sisi mahala gani - We've turned be advocate of the same..shame on us!
 
Imeandikwa tarehe 01 Mei 2013 By Beda Msimbe, Dodoma

PAMOJA na ukweli kuwa bajeti ya serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania hulipia masuala ya M uungano na Elimu ya Msingi Zanzibar sio suala la Muungano, hoja kwa nini fedha za rada hazijaenda kwenye shule za msingi Zanzibar imelazimisha Spika wa Bunge Anne Makinda kutaka watu wanaoshughulika na Muungano kuelezea kadhia hiyo.


Tamko la Spika bungeni lilitokana na mwongozo ulioombwa na Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid (CUF) aliyekariri vifungu vya katiba vyenye mwelekeo wa kuonesha kwamba fedha hizo zimetokana na shughuli za muungano na hivyo zinapaswa kwa namna nyingine kusaidia shule za Zanzibar.

Alisema kuwa masuala ya rada ni ya muungano na hivyo
chenji hiyo inagusa Zanzibar. Awali katika swali la msingi Mbunge wa Nungwi, Yusuf Haji Khamisi alitaka kujua sekta ya elimu ya Msingi Zanzibar imetengewa kiasi gani cha fedha kutoka katika fedha za rada.

Naibu Waziri Fedha, Janet Mbene alisema kwamba mchanganuo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wanaohusika na masuala ya elimu bado kuifikia na ikifika itajulikana mahitaji na fedha kutolewa.

Hata hivyo, majibu hayo yalifanya wabunge kadhaa kusimama na Mbunge wa Kasulu Mjini, Joseph Machali
(NCCR- Mageuzi) aliuliza kigugumizi cha serikali kuhusu mgawo wa Zanzibar wakati zabuni zimeshatolewa za kuchapa vitabu.

Kauli hiyo ilimnyanyua Naibu Waziri, Tamisemi, Kassim Majaliwa ambaye alianza kutoa mchanganuo wa fedha
hizo ambazo zinaonesha dhahiri kwamba ni kwa ajili ya shule za msingi za Tanzania Bara.

Fedha za rada ni marejesho ya fedha za Tanzania kutoka kampuni ya BAE Systems ya Uingereza ambayo
ilidanganya wakati wa kuiuzia Tanzania rada (chombo cha kuongozea vyombo vya usafiri angani).

Fedha hizo ambazo zimeingia katika bajeti ya serikali kiasi cha Sh bilioni 72.3 kwa mujibu wa makubaliano
yaliyofikiwa baina ya serikali na BAE Systems ya Uingereza kupitia Idara ya maendeleo ya nchi za Nje ya Uingereza (DFID), fedha zote zilizorejeshwa kutokana na mauzo ya rada zitapelekwa sekta ya elimu kugharamia mahitaji muhimu.


Source; Habari Leo
 

Kweli kama hizo PESA tungeona zinasaidia Wananchi wa Tanganyika Jinsi Wabunge wa Bara wanavyopigania ningekuwa UPANDE wao; Lakini la hasha hao wabunge wa CCM wanataka kuzikimbiza USWISI wazilete 2015 wabaki madarakani

Aheri CUF wazipiganie wawape Wananchi na Wanafunzi wa Zanzibar pia... Angalau utaona zimekwenda sehemu moja kwa Mafanikio...
 
Hizo pesa tulishasema kuwa hazitafika. Mhusika mkuu wa sakata hili ni Bernad Membe ambaye alisimama kidete kupinga pesa hizo kurejeshwa kwa namna nyingine. Hili lipo katika rekodi ya Membe kama alivyoshindwa kutuambia nani kaiba.
Membe ana makando kando mengi wakati ukifika yatawekwa hadharani. Kwa ufupi huyu Membe hafai.

Kuhusu Zanzibar, wao wanasema hawataki muungano sasa wanataka pesa za Tanganyika za nini.
Pesa ni za Tanganyika kwasababu katika bilioni 27 zilizoibwa sijui Zanzibar ilichangia senti ngapi.

Wao wakae kimya wameanzisha baraza lao la mitihani waendelee na mambo yao.
Tunasema muda wa kudowea na kujificha ubavuni mwa Tanganyika kwa jina la Tanzania sasa basi.
Hakuna senti kuvuka bahari!
 
Jee Zanzibar walipatiwa sehemu ya malipo yaliyotokana na marejesho ya pesa za Rada zilizo rejeshwa kwa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania?
 
Za asubuhi,
Wadau nimeamka ghafla na ni kama vile nilikuwa naoteshwa, lakini hapana sioti, ninakumbukumbu nzuri tu,
Ingawa si kumbukumbu dhahiri.

Mwenzenu yanayoendelea katika inchi hii huwa yanasababisha hadi wakati mwingine niweweseke kwa tafakari kali.

Iko hivi,
Wiki iliyopita kwa chati nilikuwa nalifuatilia Bunge la bajeti linaloendelea Dodoma na nikamsikia kwa masikio yangu naibu waziri mmoja akimjibu Mbunge mmoja alieuliza kutaka kujua juu ya Ilivyotumika ile Pesa iliyorejeshwa kutokana na ununuzi tata wa Rada uliopelekea serikali ya Tanzania kuhaha na hatimae kufanikiwa kuishawishi pamoja na huruma ya serikali ya Uingereza kwa Tanzania kuhakikisha sehemu ya pesa hiyo inarejeshwa na hatimae serikali ya Tanzania kutueleza kuwa pesa yote hiyo itaelekezwa katika matumizi ya kuboresha huduma za kijamii ikiwemo maswala ya elimu.

Sasa jibu lililotolewa na Mjibu swali (naibu waziri kama sikosei) ndilo lililonistajaabisha;
Sikulielewa pale, Sijalielewa hadi sasa, Na nahisi itakuwa ngumu kwangu kulielewa.
Alisema baada ya kujibu swali la nyongeza, "Kuhusu pesa za Rada; zimetumika huku bara na si kwaajili ya kutumika Zanzibar" -Na aliishia hapo.

Nina imani masikio yangu yamesikia kitu kama hicho.

Kama kuna alielisikia hili ama ana ufahamu mpana juu ya habari hii naomba tupanuane mawazo.

Ila ukakasi ninaouona kama masikio yangu hayakuniongopea;
Ni wazi Pesa hiyo ilitokana na walipa kodi Watanzania (Watanganyika na Wazanzibari)
Sasa vipi irejee kisha itumike Tanganyika tu?

Sielewi
 
mi nawashangaa wazanzibari kama walikua na uwezo wa kuwauwa mapadri kwa kuzani wanatetea muungano wanashindwa nini kuwaangamiza wanafiki wote walio huko wanaochelewesha uhuru wa kweli wa zanzibar?
 
wazenji wanataka vya bure, kama mnataka vya bure, njooni tuwape chenji, pia tutawanunulia na vyakula na chochote mtakachotaka tutawafanyia shopping...lakini malipo yake muwe tayari kwa lolote.....si mnataka vya bure!

vipi tende na halua mtawapa?
 
Msibabaishe watu nyinyi ni wezi tu hakijulikani cha Muungano wala cha Tanganyika. Ikija faraja hii yetu, maafa yetu sote.
 
Back
Top Bottom