Zanzibar itakufa kama Tanzania ikifa!

Inaweza kuzaliwa Zanzibar mpya. Mfano wanaweza kuunda selikari yao ya Muungano wa visiwa vya Pemba na Unguja. Selikari ya Pemba na Selikari ya unguja zikishughulika na mabo yao ya ndani na Selikari ya Muungano ikishughulikia mambo ya Muungano wao.

Pia maridhiano yanaweza kufanyika kwa raia watakaoamua kubaki kwa hiari yao katika sehemu mojawapo zilizokuwa zinaunda muungano uliovunjika. Tutakapoamua kutumia Busara au Jazba kakika kuvunja muungano ndivyo vitakavyoamu yale yatakayotokea siku ya kuvunjika kwa muungano. Montenegro walipiga kura kujitoa kwenye Muungano na Serbia, Serbia kwa shingo upande wakaamua kuwaruhusu lakini hawakuchukua hatua za kuwafukuza wamontenegro waliokuwa wanaishi serbia. Sana sana Serbia ilitafuta njia nyingine ya kuimarisha mahusiano na Montenegro na si kuendeleza uhasama. Hivyo hata kwa Tanganyika na Zanzibar kuna mambo mengi tunaweza kufaidishana baada kama muungano wetu tutauvunja kwa kufuata taratibu zinazotakiwa badala ya kutumia jazba, kujenga uhasama, n.k

Mkuu nakupa hongera kwa mawzo yako ya BUSARA na napenda kukutowa hofu kuwa hakuna mfarakano wowote kati ya Unguja na Pemba na kinachotokea ni kila mmoja kutumia haki yake ya Kidemokrasia.
Mgawanyiko wa kura ni jambo la kawaida chemgelecho Waswahili" Mtu haachi kutia tonge kwenye mdomo akatia puani" Na "Mcheza kwao hutunzzwa"
Ikiwa anaegombea nafasi ya uongozi anawakilisha matakwa yangu basi ni natural nitampigia kura na hicho ndicho kinachofanyika kule Pemba.
 
Nadhani Semilog umejibu kitaalamu hili. Na wapemba wanaokuwepo Unguja katika jimbo lolote lile hawawezi kushinda uwingi wa wa_Unguja waliopo katika jimbo hilo- Ndiyo maana wanashindwa Unguja. Lakini hii hali siyo nzuri Kwa nini watu wapige kura on this basis. Walioasisi mtizamo huo walikuwa na tamaa zao. Sisi kwa nini tunatumbukia huko. Ndiyo maana nasema kule Zanzibar tuachane na CUF , tuachane na CCM, tuachane na kumbukumbu za tuliowazika za ASP na Hizbu. Tuanze upya . tuanzishe vyama vyetu pale Zanzibar( ni kwa ajili ya Zanzibar tu-tupige siasa ) na tuingie katika kura kutafuta Rais na Wawakilishi.Bara hawamo na hawahusiki kwa lolote lile.

Pakacha , Naanza kuingiwa na wasiwasi na uelewa wako kwa masuala ya Zanzibar. Hivyo nani kakwambia kuwa upinzani kwa CCM uko kwa Wapemba waishio Unguja? Upinzani kwa CCM uko miongoni mwa Waunguja wenyewe na nisingependa kulizungumzia hili unless upinge kauli yangu. Nakumbuka uliwahi kusema kuwa anaepalilia mgawanyiko ni mwenye dhambi, sasa nasema tena hiyo dhambi inaifanya wewe. Tukazane kuvinusuru Visiwa vyetu na baadae tofauti zetu tutatatua kistaarabu.
 
Hakuna faida yeyote ya muungano, kuna mabadiliko gani wazanzibari walio pata baada ya muungano? Na kwanini Tanzania bara hawataki kuiachia zanzibar? Muungano uvungike na tuone kama wabara hatutagombania kwenda zenji. hii yote ni staili ya CCM ya divide and rule. hawa wakiwa kitu kimoja ndio watapata mabadiliko. Yani toka Waomani walivyo ijenga zenji ni mpaka leo hakuna kilicho zidi. Hata hizo nyumba za karume mpaka leo zimewashinda.
 
Hakuna faida yeyote ya muungano, kuna mabadiliko gani wazanzibari walio pata baada ya muungano? Na kwanini Tanzania bara hawataki kuiachia zanzibar? Muungano uvungike na tuone kama wabara hatutagombania kwenda zenji. hii yote ni staili ya CCM ya divide and rule. hawa wakiwa kitu kimoja ndio watapata mabadiliko. Yani toka Waomani walivyo ijenga zenji ni mpaka leo hakuna kilicho zidi. Hata hizo nyumba za karume mpaka leo zimewashinda.

muungano ukivunjika ni wapemba ndio watang'ang'ania bara na sio wabara kutaka kwenda unguja.

hamna mtu anayewashika mkiondoka commoro wanachukua nafasi yenu.

mpaka sasa hivi ni wapemba ndio wameenda UN kudai nchi na sio waunguja kwa hiyo hichi ni kielelezo cha kwamba z'bar sio moja kama mnavyodai..

kwa nini waunguja hawajaenda UN kama kweli kuna umoja?

akili yenu ndio inasema kwamba z'bar ikitengana na bara wa-OMANI watamwaga misaada, acheni kuwa na akili za kitumwa. WAWEKEZE SASA HIVI KWANI NANI KAWAZUIA WA-OMANI KUWEKEZA Z'BAR.
 
Last edited:
Kwanza nawasalimu wote wapenzi wa Jamii forum na michango yao mizuri, mimi ni mpenzi sana wa Forum huwa sikosi kuwasikiliza na kusoma post zenu kila siku, ila sasa nimeamua pia kuwa miongoni mwa wachangiaji ili na wengine wasome mawazo yangu, nafikiri ni uamuzi mzuri tu.

Kwa keli swala la Nzanzibar ni gumu sana kama tunavyolichukulia, Mimi binafsi nakubakliana kabisa na mtoa mada kuwa itakuja geuga Burundi kwani , wakibaki pekee yao wapemba hawaamini kama wale wa unguja ni wenzao, wanaamini waunguja ni watu wa bara, na pemba wanaamini wao ni jamii ya mwaarabu na hawakubaliani na mapinduzi yaliyofanywa ya kumtoa sultani, hadi leo wanaamini sultani alitakiwa awepo na ndiye ndugu yao.

Kama unataka kuhakikisha hilo , Fanya utafiti kwa kukutana na wa pemba wanaoishi nje ya Tz jaribu kukaa nao na ongea nao mawazo yao na fanya hivyo kwa watu zaidi ya 10, utakuta wana mawazo yaliyo sawa. Nimekutana na wapemba zaidi ya 20 nje ya nchi, na nimeishi nao vizuri lakini inapofika kusema wao ni watanzania , basi mtabishana hadi asubuhi na hata mkiita kikao cha Watz ni nadra sana kuhudhuria, na sababu kubwa wanasema sisi siyo ndugu zao, ndugu yao ni mwaraabu. Kwa hali hiyo Muungano ukifa wataanza kuwabagua waunguja kuwa wametoka bara. na mwisho wake itakuwa kupigana kana kama Burundi, Mtusi na Mhutu. Tusiombee hayo lakini HABARI NDIYO HIYO!!!
 
Visiwa hivi vitaendelea kuwa sehemu ya Jamhuri!

Huo ndo ukweli!

Kama yakigunduliwa mafuta wachimbe tu kama jinsi wanavyopata pesa ya utalii hawaingiliwi!

Ila waache kusamehe watu kutolipa kodi na kisha kuanza kulalamika wanaonewa wakati kodi 50% haikusanywi!
 
Kwanza nawasalimu wote wapenzi wa Jamii forum na michango yao mizuri, mimi ni mpenzi sana wa Forum huwa sikosi kuwasikiliza na kusoma post zenu kila siku, ila sasa nimeamua pia kuwa miongoni mwa wachangiaji ili na wengine wasome mawazo yangu, nafikiri ni uamuzi mzuri tu.

Kwa keli swala la Nzanzibar ni gumu sana kama tunavyolichukulia, Mimi binafsi nakubakliana kabisa na mtoa mada kuwa itakuja geuga Burundi kwani , wakibaki pekee yao wapemba hawaamini kama wale wa unguja ni wenzao, wanaamini waunguja ni watu wa bara, na pemba wanaamini wao ni jamii ya mwaarabu na hawakubaliani na mapinduzi yaliyofanywa ya kumtoa sultani, hadi leo wanaamini sultani alitakiwa awepo na ndiye ndugu yao.

Kama unataka kuhakikisha hilo , Fanya utafiti kwa kukutana na wa pemba wanaoishi nje ya Tz jaribu kukaa nao na ongea nao mawazo yao na fanya hivyo kwa watu zaidi ya 10, utakuta wana mawazo yaliyo sawa. Nimekutana na wapemba zaidi ya 20 nje ya nchi, na nimeishi nao vizuri lakini inapofika kusema wao ni watanzania , basi mtabishana hadi asubuhi na hata mkiita kikao cha Watz ni nadra sana kuhudhuria, na sababu kubwa wanasema sisi siyo ndugu zao, ndugu yao ni mwaraabu. Kwa hali hiyo Muungano ukifa wataanza kuwabagua waunguja kuwa wametoka bara. na mwisho wake itakuwa kupigana kana kama Burundi, Mtusi na Mhutu. Tusiombee hayo lakini HABARI NDIYO HIYO!!!

Karibu sana na tunakupongeza kwa kutowa maoni yako lakini cha kukuasa ni kuwa kama unataka kujua hali halisi ya visiwa vya Zanzibar kuwa mwangalifu na unaowakuta huko uliko. Wapo wenye mawanzo ya kutafuta maisha huko lakini wapo pia walioshindwa na ukweli wa maisha huku kwetu na hivyo kuamua kuyukimbia ukweli.
UNAKOSEA sana kuifananisha Zanzibar na Burundi kwani hakuna hicho kinachitwa mpasuko kati ya Pemba na Unguja bali upo mpasuko wa maslahi ya watu wachache wanaotumia mambo makubwa mawili yaliyotokea visiwani humo.
Jambo la kwanza ni Mapinduzi ya mwaka 1964. Katika Mapinduzi hayo Wakaazi wa kisiwa cha Unguja waliuwana kwa lengo la kuondowa utawala wa Kiarabu uliokuwa na chimkuko Omani. Wakati wa Mapinduzi tayari Zanzibar ilikwisha changanya damu kati ya wenye asili ya Waarabu na Waafrika. Mapinduzi yaliwaondowa Watawala wa Kiarabu lakini Watu wenye asili ya Uarabu walibaki Visiwani na hawkuwa na pa kwenda. Sasa ni miaka karibu 45 tangu yatokee hayo wapo bado wanaoegemea historia hii ili kupata kukubaliwa na Waunguja.
Jambo la pili ni kuachwa nyuma kimaendeleo kwa kisiwa cha Pemba. Hili lilikuwapo hata kabla ya Mapinduzi na hii ni natural kwani Unguja ndiko kunako na watawala hivyo kupewa upendeleo. Hali hii imezidi kuwa mbaya hivi sasa kwa vile Zanzibar kwasababu ya kubanwa na Muungano haina uwezo wa kuiendeleza Pemba. Hili limewapa advantage viongozi wa upinzani na kusema kuwa Pemba inawekwa nyuma.
Zanzibar hawawezi kupigana wao kwa wao hata siku moja bila kuchonganishwa. Kiburi cha upande mmoja kinaletwa na vikosi vya askari kutoka Bara kwa lengo la kuilinda CCM kwa kuogopa kuwa wapinzani wakishinda Muungano utavunjika.
La uhakika ni kuwa Pemba hawataki hata siku moja kujitenga na Unguja kwani visiwa hivi havikuuungana bali ni visiwa vya pamoja.
La uhakika Zanzibar hawataki kuvunjika kwa Muungano kwani ungekuwea hauwakeri kama wangekuwa na uhuru wa kujiamulia mambo yao na kujiendeleza kiuchumi.
NA LA UHAKIKA zaidi Zanzibar si sawa na Burundi kwani hakuna mmakabila bali kuna tofauti za maslahi na hili lipo popote hat Bara.
 
Nimeshafanya kazi sehemu yenye wapemba na waunguja wengi, mimi(mbara) uk. Yana wanabaguana mpaka basi. Lakini waunguja wako karibu na wabara. Ukitoka eneo la kazi huko nje ndio kabisaaa, yaani ukimuona mmpemba ambaye ubaguzi wake mdogo basi ameishi unguja.
Kama unaona burundi hatari, basi ni kama wajaluo na wakikuyu....
 
Visiwa hivi vitaendelea kuwa sehemu ya Jamhuri!

Huo ndo ukweli!

Kama yakigunduliwa mafuta wachimbe tu kama jinsi wanavyopata pesa ya utalii hawaingiliwi!

Ila waache kusamehe watu kutolipa kodi na kisha kuanza kulalamika wanaonewa wakati kodi 50% haikusanywi!

Nini maana ya kutoingiliwa?
 
Nimeshafanya kazi sehemu yenye wapemba na waunguja wengi, mimi(mbara) uk. Yana wanabaguana mpaka basi. Lakini waunguja wako karibu na wabara. Ukitoka eneo la kazi huko nje ndio kabisaaa, yaani ukimuona mmpemba ambaye ubaguzi wake mdogo basi ameishi unguja.
Kama unaona burundi hatari, basi ni kama wajaluo na wakikuyu....

Chuki zao ni kuwa hawapo Zanzibar ambako Wapemba ni wake wa Wanguja na Muunguja kuzaa na Mpemba. Chuki za huko zinasababishwa na msimamo wa kiitikadi kwamba Wapemba wengi walio nje ya nchi ni wale waliochanganya na walipowasili huko walianza kufika kabla ya Waunguja. Waliowapokea ni wale waliokimbia kwa sababu za Kisiasa.(Inabidi uijue Zanzibar ndio uelewe kuwa kupinga serikali au kutafautiana nayo tu wakati fulani ilikuwa dhambi kubwa ya kupoteza maisha)

Wakati ule umepita kwa huku kwetu na demokrasia inafuata lakini huko pande zote mbili bado hawajaacha kuona kuwa kuhitilafiana kiitikadi si dhambi.

Wazanzibari kwa kawaida ni watu wastahamilivu na wapenda dini vitu ambavyo mkiwa huko havina thamani kwenu. Mauwaji yaliofanyika wakati wa Mapinduzi na kipindi fulani baada ya Mapinduzi yangekuwa ni visasi kwa watu wengine lakini kwa Wazanzibari hayo yote yanaonekana ni historia na waliouliwa watu wao wanaendelea kuipenda nchi yao kama kawaida.
Usichukue kigezo cha hao ulionao kwa maisha ya Wazanzibari kwani wengi wao huku ni kwao tu lakini hawana chochote cha kujifananisha nasi. Hata dini na mila zao wengi wameshaziweka kando.
 
Hakuna mpemba wala Muunguja wanaotofautiana ,si ndani ya Nchi wala si nje ya nchi ,nimeona na kukaa na kutulia ili kuona uchangiaji wa baadhi yenu,hamna tofauti na ngonjera za wafuasi wa CCM kuchomekea uwongo,yaani hata hamuoni aibu kusema mambu ambayo hayapo, WaPemba na Waunguja wanakuwa pamoja na wanasaidiana sana tu,nimekaa Uk nimeona namna wanavyoshirikiana tena huwezi hata kuwabagua labda kwa wale ambao hawajapoteza kilugha ,vile vile Nimeishi Canada nako huko ndio kabisa na upo umoja wa WaZanzibari ,wanasaidiana sana hata watu kutoka Tanzania bara wanapata msaada katika umoja wao huo.

Hizi mnazozisema ni fitna ambazo zinachomekewa na wafuasi wa Sultani CCM ili izidi kukandamiza ,na ajabu CCM wanapokandamiza huwachanganya wote waunguja na Wapemba ,ni waunguja wachache na wapemba wachache ambao wanafaidika zaidi maslahi ni kwa wale waliopo juu huko ambao wao ndio wanajiona ndio CCM ,lakini tembelea unguja mashamba uone mtu alivyosawijika ,kijana wa miaka selasini utafikiri mtu mwenye miaka 56 ,dhiki shida zimewatanda ,mtu cha kukila hakijui ,anaishia mapapai na madafu, hizi chuki mnazozipanda hazitafanikiwa kamwe ,tatizo linaloikabili Zanzibar ni utawala na hakuna jingine maana watawala waliokuwepo nyuso zimewaparama kila mmoja ni mtu wa maslahi binafsi hana habari na mwengine,ni kama watu walioambiwa kuwa kesho hakuna tena uongozi wala serikali kila mtu kivyakevyake ,utawaona wanakusanya na kusanya kwa ajili yao tu ,hawajali kabisa hali ya mtu mwengine ,nasema utawala mbovu ndio uliowafanya nyinyi mnaochomekea kuwa kuna matabaka ya muunguja na Mpemba ,hivyo kama madai yenu yanavyodai ikiwa mnaona hivyo basi fahamuni kuwa matatizo hayo yanasababishwa na utawala usiojali maisha ya wananchi wake ,tofauti hazikosi lakini sio hizo mnazozizungumza ninyi zenu zinajenga uadui baina ya ndugu ,maana mnasema mmoja kazaliwa kidogo mweupe na mwengine mweusii hio ni chuki mnayoijenga ili jamaa zenu wazidi kubaki kwenye madaraka lakini mmechelewa ,Zanzibar one day tes itapata viongozi wenye kujali maslahi ya wananchi wote na hapo ndio mtajua kuwa popo si ndege.
 
Kwanza nawasalimu wote wapenzi wa Jamii forum na michango yao mizuri, mimi ni mpenzi sana wa Forum huwa sikosi kuwasikiliza na kusoma post zenu kila siku, ila sasa nimeamua pia kuwa miongoni mwa wachangiaji ili na wengine wasome mawazo yangu, nafikiri ni uamuzi mzuri tu.

Kwa keli swala la Nzanzibar ni gumu sana kama tunavyolichukulia, Mimi binafsi nakubakliana kabisa na mtoa mada kuwa itakuja geuga Burundi kwani , wakibaki pekee yao wapemba hawaamini kama wale wa unguja ni wenzao, wanaamini waunguja ni watu wa bara, na pemba wanaamini wao ni jamii ya mwaarabu na hawakubaliani na mapinduzi yaliyofanywa ya kumtoa sultani, hadi leo wanaamini sultani alitakiwa awepo na ndiye ndugu yao.

Kama unataka kuhakikisha hilo , Fanya utafiti kwa kukutana na wa pemba wanaoishi nje ya Tz jaribu kukaa nao na ongea nao mawazo yao na fanya hivyo kwa watu zaidi ya 10, utakuta wana mawazo yaliyo sawa. Nimekutana na wapemba zaidi ya 20 nje ya nchi, na nimeishi nao vizuri lakini inapofika kusema wao ni watanzania , basi mtabishana hadi asubuhi na hata mkiita kikao cha Watz ni nadra sana kuhudhuria, na sababu kubwa wanasema sisi siyo ndugu zao, ndugu yao ni mwaraabu. Kwa hali hiyo Muungano ukifa wataanza kuwabagua waunguja kuwa wametoka bara. na mwisho wake itakuwa kupigana kana kama Burundi, Mtusi na Mhutu. Tusiombee hayo lakini HABARI NDIYO HIYO!!!

Hivyo ni vitisho na propaganda ambazo zinatumiwa na Selikari zilizopo madarakani kuendelea kuishikilia Zanzibar kwenye muungano. Toka mwanzo badala ya kuwafanya wazanzibari waishi pamoja, tumeendelea kuwatenganisha ili tuwatawale kirahisi. Yawezekana bara ndi maana hata maendeleo hatupati kwa sababu tumeendelea kuwagonganisha wau wasio na hatia ili wasielewane.
 
Hali ya kisiasa ya zanzibar ilivyo sasa hivi ni kama burundi au rwanda.
Zanzibar hakuna upinzani wa kisiasa bali kuna ukabila. Waunguja wanapigia kura ccm na wapemba cuf.

Kwa mantiki hiyo ninaamini kwamba endapo muungano utavunjika na ikarudi kuwa tanganyika na zanzibar, miezi mitatu ya mwanzo itakuwa ni furaha kwa wazanzibar kwa ajili wamekua na nchi yao wenyewe, halafu machafuko yataanza pale uchaguzi wa kumteua rais wa zanzibar utakapoanza. Wapemba watapigia kura cuf na waunguja ccm(asp) na hapo ndio zanzibar itakapopasuka na unguja kuwa nchi na pemba kuwa nchi na rais wake sshamad. Wapemba hatakubali rais awe muunguja kwa ajili imekua hivyo siku nyingi sana na waunguja wanaamini kwamba wapemba ni wabaguzi watawabagua sana.

mambo yote haya yatatokea katika kipindi cha mwaka mmoja.

fact: Uk kuna wazanzibari wengi lakini wamegawanyika katika makundi mawili wapemba na waunguja. Waunguja wapo karibu na watu wa bara na wapemba wako wenyewe. Pamoja na kuja ulaya bado wameshidwa kuwa ndugu. Kama wakikuyu na wajaluo uk



Athari za kuvunjika kwa muungano
1.wa bara waliokuwa zanzibar wataambiwa warudi kwao na wengine hata kupoteza maisha yao. (hawako wengi)

2. Wapemba ambao wanamaduka bara itabidi wayafunge na warudi kwao, sijui pemba ilivyokuwa ndogo watamuuzia nani vitu.

3.wazazibari wenye magorofa kariakoo itabidi wayaache na warudi kwao. Hata mzee mwinyi itabidi aondoke aliache lile gorofa lake msasani na white sands hotel.

4. Kwa sisi tuliooa zanzibar itabidi wake/waume zetu warudi zanzibar na watoto wabakie bara (kitu kibaya sana hichi).

5. Wakati mamboa yote haya ya kiendelea wananchi wakitaabika viongozi watakua wanagawana madaraka. Je wazanzibari mmefikiria au ni kufuata mkumbo wa viongozi

mkoa wa kinondoni una watu zaidi ya zanzibar nzima.
Solution: Kuwa na serikali moja rais mmoja na pemba na unguja kuwa mikoa yenye ma mayor ambao watapigiwa kura na wananchi.

MOD peleka kwenye udaku hii kitu please, hamna kitu humu. (pumba tupu)
 
Back
Top Bottom