Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Wanabodi,
Recently nimefurahishwa sana na wenzetu wa Zanzibar! Kwa nini? Wemeacha kuongea sana siasa kama walivyokuwa mwanzoni wenzetu wamejifunza kwamba too much politics hazitupeleki popote, sasa wanaongelea maendeleo... Jamaa wakiendelee hivi... wabara tunaachwa.
Angalia mojawapo haya mengi SMZ inayofanya. Narudia kuwaomba vijana kama Zitto, Mnyika, January etc ensure we tranform politics za Tanzania bado tunaongea mambo ya kizamani, lets talk about real development....
HabariLeo | Wakurugenzi wa Mipango watakiwa kuwajibika
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema wakurugenzi wa Mipango na Sera watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu, watalazimika kujiondoa wenyewe kwa
sababu watakuwa wameshindwa kazi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo, Omar Yussuf Mzee wakati akifungua mafunzo kwa watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwemo wakurugenzi wa Mipango na Sera mjini Unguja ambayo
yamefadhiliwa na Jumuiya ya Madola.
Mzee alisema Serikali malengo yake makubwa ni kuona wakurugenzi hao wanakuwa wabunifu katika maeneo mbalimbali na baadaye mafanikio makubwa yanafikiwa.
Alisema wakurugenzi hao kutokana na majukumu yao makubwa wao ni kiungo kizuri kati ya wizara na taasisi zote zilizomo katika wizara hiyo.
"Wakurugenzi wa Mipango na Sera ndiyo tegemeo kubwa la mafanikio katika wizara zetu za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar...tunawataka wawe wabunifu katika utendaji wa shughuli zao za kazi za kila siku," alisema Waziri huyo.
Aidha, alisema wakurugenzi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao, itakuwa wameshindwa kazi na hivyo watalazimika kukaa pembeni kutoa nafasi kwa watendaji wengine.
Alisema Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein ameamua kuunda Idara za Mambo ya Utafiti na Sera katika kila Wizara kwa lengo la kubuni uwezo na mambo ya utafiti katika wizara hizo.
Recently nimefurahishwa sana na wenzetu wa Zanzibar! Kwa nini? Wemeacha kuongea sana siasa kama walivyokuwa mwanzoni wenzetu wamejifunza kwamba too much politics hazitupeleki popote, sasa wanaongelea maendeleo... Jamaa wakiendelee hivi... wabara tunaachwa.
Angalia mojawapo haya mengi SMZ inayofanya. Narudia kuwaomba vijana kama Zitto, Mnyika, January etc ensure we tranform politics za Tanzania bado tunaongea mambo ya kizamani, lets talk about real development....
HabariLeo | Wakurugenzi wa Mipango watakiwa kuwajibika
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema wakurugenzi wa Mipango na Sera watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu, watalazimika kujiondoa wenyewe kwa
sababu watakuwa wameshindwa kazi.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo, Omar Yussuf Mzee wakati akifungua mafunzo kwa watendaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwemo wakurugenzi wa Mipango na Sera mjini Unguja ambayo
yamefadhiliwa na Jumuiya ya Madola.
Mzee alisema Serikali malengo yake makubwa ni kuona wakurugenzi hao wanakuwa wabunifu katika maeneo mbalimbali na baadaye mafanikio makubwa yanafikiwa.
Alisema wakurugenzi hao kutokana na majukumu yao makubwa wao ni kiungo kizuri kati ya wizara na taasisi zote zilizomo katika wizara hiyo.
"Wakurugenzi wa Mipango na Sera ndiyo tegemeo kubwa la mafanikio katika wizara zetu za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar...tunawataka wawe wabunifu katika utendaji wa shughuli zao za kazi za kila siku," alisema Waziri huyo.
Aidha, alisema wakurugenzi watakaoshindwa kutekeleza majukumu yao, itakuwa wameshindwa kazi na hivyo watalazimika kukaa pembeni kutoa nafasi kwa watendaji wengine.
Alisema Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein ameamua kuunda Idara za Mambo ya Utafiti na Sera katika kila Wizara kwa lengo la kubuni uwezo na mambo ya utafiti katika wizara hizo.