Zambia forces Malawi High Commission out of its building in Tanzania

Mahusiano ya Kidiplomasia kati ya Malawi na Zambia yatalega lega,kihistoria Majirani hawa kusini mwa Afrika wana Nasaba,Watu wa Malawi wanaingiliana sana na watu wa Zambia na kuna familia zipo kiasili pande zote za Nchi hizi.Hapa kuna Jambo la kujifunza na haswa suala zima la nguvu za Rais.Rais Mteule wa Zambia Michael Chilufya Sata ni mtu wa visasi na mmtoa maamuzi yote mwenyewe bila kujali sana maamuzi ya washauri wake,Kwa kuwa Watanzania ni wapenda mambo ya haraka na ya mlipuko,Rais huyu (Labda kwa kuwa anatoka upinzani) amekuwa na upenzi mkubwa kutoka kwa Watanzania walio wengi,labda ni kutokana na maamuzi yake makubwa anayoyafanya kwa haraka.

Hapa naandika machache kuonyesha uharaka na utendaji kazi wa Rais Sata,haya ni maoni yangu binafsi nipo wazi kupingwa na kushauriwa kwa sababu tunajifunza kwa njia hii,Kwangu Mimi naona Afrika hatuhitaji Viongozi Wababe kama Sata bali tunahitaji Taasisi kama Bunge,Mahakama na Vyombo vya Ulinzi Imara.Hivi karibuni baada ya kuchaguliwa Rais Sata ameingia ktk mgogoro na Rais Mstaafu,Rupia Banda baada ya Sata kudai kuwa Banda ana asili ya Malawi na kwamba Mama yake Banda bado anaishi Malawi hata baada ya Banda kuwa Rais wa Zambia na sheria mojawapo ya kuwa Rais wa zambia ni lazima uwe mzaliwa wa Zambia na Wazazi wako wote wawili wawe ni Raia wa Zambia.

Rais Sata alifukuzwa (Deportation) Zambia mwaka 2007 baada ya kuonekana kuwa ziara yake hiyo binafsi ilikuwa na nia ya kwenda kusaidia upinzani dhidi ya serikali ya Bingu Wa Mutharika.Mwezi Oktoba 2011 Rais Sata alikataa kuhudhuria Mkutano wa Comesa kwa madai kuwa lazima serikali ya Malawi imuombe msamaha kwa sababu ya kitendo cha kufukuzwa Nchini humo mwaka 2007.Serikali ya Malawi ilikataa kufanya hivyo.

Mara baada ya kuapishwa Rais Sata aliwaomba radhi Angola kwa maelezo kuwa Serikali ya Mzee kaunda ilifanya kosa kubwa kuwasaidia UNITA na Jonas Savimbi,kwa maana hiyo anawaomba Msamaha serikali ya Angola kwa kosa hilo kubwa,alipobanwa na vyombo vya habari vya Nje Sata alidai amefanya uamuzi huo kwa sababu za kiuchumi,ni rahisi kununua mafuta Angola kuliko sehemu yoyote duniani.

Rais Sata mara baada ya kuanza kazi alimfukuza kazi Mkuu wa Ant-corruption Godfrey Kayukwa na nafasi yake kupewa Mwanamama Rosewin Wandi,sababu iliyotolewa ktk kumuondoa Kayukwa ni kwamba Taasisi hiyo ilishindwa kutoa majibu kwanini tenda ya kuchapisha nyaraka za Uchaguzi inapewa kampuni moja bila ushindani/mchakato (National printing group) kwa kipindi cha chaguzi mbili tofauti,hali hiyo ilionyesha kuwepo kwa rushwa ktk skuadi ya Ant-corruption.lakini ukweli wa mambo ni kwamba Ant-Corruption hiyo ilishawahi kumuhoji Sata (Alipokuwa raia wa kawaida) baada ya kumkuta ana jumla ya $ 500,000 ktk moja ya akaunti zake za Bank, Rais Sata pia alishawahi kuzuiwa Uwanja wa Ndege wa Johannesburg/Afrika kusini baada ya kukutwa anasafiri na kiasi kikubwa cha pesa.

Kwa kuonyesha kuwa Sata ni mtu wa visasi,na bado ana kinyongo na Malawi,Mwezi Oktoba ameamuru Redio moja ya Nchini Malawi isirushe Matangazo yake ndani ya Zambia,Redio hiyo inamilikiwa na Atupele Mtoto wa Aliyekuwa Rais wa Malawi,Mzee Bakili Muluzi.

Kwa hiyo maamuzi haya ya kupandisha Pango la Nyumba (Ubalozi) ni moja kati ya njia zake za kuikomesha Malawi,bado tutasikia mengi makubwa katika Utawala huu mpya wa Rais Michael sata.Lakini ni wazi kuwa masuala ya Nje na Diplomasia ya kimataifa kwa ujumla anahitaji ushauri madhubuti,vinginevyo Zambia itapoteza marafiki wengi.Kwani hata Muwekezaji mkubwa wa Zambia ktk Madini na sekta nyingine nyingi China wamekwisha kwaruzana nae,katika moja ya mikutano yake ya kampeni Sata aliwaita Wachina sio wawekezaji bali ni Wakoloni!

Mkuu Mwawado karibu sana tena sana Mkuu na heshima mbele.............Huyu Sata kwa visasi........ananikumbusha Gen Idi Amin......wakakti mwingine matokeo ya Demokrasia ndio kama tunayoyaona Zambia...........ni kweli kabisa anahitaji washauri makini...........na Tanzania tuna nafasi kubwa sana ya ku-influence............. ninachoomba pia asianze kuua wapinzani wake........
 
Ni mbaya sana mtu kuongozwa na visasi. Ukiwa na visasi wakati wote unawaza kuumiza tu!

Tusubiri kama EL akiapishwa hapo january 2016 miaka 5 ya kwanza itakua ni kulipa visasi tu kwa wale waliompinga, miaka 5 mingine kama akipita itakua ni kulipa fadhila za wale waliomsaidia na kumuamini kuwa nae katika kipindi kigumu.
 
visasi huzaa fitna.
ni matumaini yangu maamuzi ya mhe. sata hayajaongozwa na mambo ya visasi bali na nia madhubuti ya kuleta utawala bora
na maslahi kwa nchi yake. kama kweli yameletwa na visasi basi katika upana wa maamuyi hayo naona wakati mgumu kwa
sadc na comesa.
 
Watanzania bana hovyo kabisa,yaani ni majitu yasiyotabirika leo baridi kesho moto.Na kwa tabia hizi na ujinga huu tutaendelea kuongozwa na majizi,mafisadi,majambazi na majitu yasiojari haki,sheria na usawa kwa wengine.
 
Kuna bifu kali inaendelea hivi sasa kati ya Zambia na Malawi. Bifu imesambaa hadi Tanzania. Balozi za Zambia na Malawi zimekuwa zikitumia jengo moja lililoko mtaa wa Ohio jijini Dar Es Salaam. Inasemekana kuwa jengo ni mali ya Zambia na kuwa Malawi walikuwa wamepanga ofisi yao ya ubalozi hapo. Siku chache zilizopita Zambia walipandisha kodi ya pango kwa asilimia 200. Kuona hivyo, Malawi wakachomoa na kuhamia kwenye ofisi nyingine iliyopo karibu na Rose Garden, Mikocheni.

Bifu ilianza baada ya Sata kushinda urais. Lakini kwa wale wafuatiliaji wa siasa baina ya nchi hizi mbili mtakumbuka kuwa mwaka 2007, Sata alienda Malawi kwa matembezi lakini Malawi wakam-deport saa chache baada ya kuwasili nchini humo. Japokuwa Malawi haikutoa sababu za kum-deport, inasemekana walimrudisha Zambia kwa sababu alikwenda Malawi kwa nia ya kumsadia rais wa zamani wa Malawi Bakili Muluzi.

Tayari Sata ameshamwita nyumbani balozi wa Zambia nchini Tanzania lakini bado hajatuma balozi wake mpya. Pia Sata amekataa kuhudhuria mkutano wa COMESA nchini Malawi na ameitaka Malawi iombe radhi kwa yaliyotokea huko nyuma. Tayari Sata ameshaomba radhi kwa serikali ya Angola kwa kitendo cha serikkali ya zamani ya Zambia chini ya chama cha MMD kumuunga mkono Jonas Savimbi wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Sata, ambaye anaitambua Hong Kong kama "country" na Taiwan kama"sovereign State", tayari amesharuhusu vituo vya TV vya Malawi vilivyopigwa marufuku nchini humo kurusha matangazo yao kutokea Zambia.

Sitegemei Membe kuingilia hili.
 
Huyu Sata anaonekana ni 'mpumbavu' saana
toka awe Rais yeye ni 'revenge tu na malawi
hana kingine kipya cha kufanya..
 
membe hawezi kuingilia kwa sababu sata ana bifu kubwa tu na ccm alishatamka wazi'sijui wapinzani wanasubiri nini kuwasiliana na sata'subiri utaona yatakayojitokeza siku si nyingi
 
Huyu Sata anaonekana ni 'mpumbavu' saana
toka awe Rais yeye ni 'revenge tu na malawi
hana kingine kipya cha kufanya..

The Boss. Unajua kwamba wewe ndo unaweza kuonekana ni mpumbavu awa tahira wa kutupwa ikiwa kama hutathibisha kuwa rais Sata ni mpumbavu kwa namna gani.? Kama hujui siasa za Zambia kwa sasa bora ukakaa kimya kuliko kusema hivyo..!?
 
Huyu Sata anaonekana ni 'mpumbavu' saana
toka awe Rais yeye ni 'revenge tu na malawi
hana kingine kipya cha kufanya..

Lakini pia yeye kaomba radhi kwa nchi nyingine kutokana na yaliyofanywa na Zambia huko nyuma.
 
membe hawezi kuingilia kwa sababu sata ana bifu kubwa tu na ccm alishatamka wazi'sijui wapinzani wanasubiri nini kuwasiliana na sata'subiri utaona yatakayojitokeza siku si nyingi

Mkuu inawezekana maana hata sera zake ni tofauti na zetu. Nakumbuka mwaka 2008 alisema akiwa rais ange-revoke leseni za wawekezaji wa nje if they resisted his orders to give at least a 25% stake in their companies to Zambians though at his inauguration as President, he assured foreign investors that they are welcome in Zambia provided that they improve conditions for their Zambian employees.
 
Sata asipokuwa makini atajikuta anacheza na siasa za ndani huko Malawi. Urafiki wake na Bakili Muluzi unajulikina, na sote tunajuwa kumekuwepoa na zogo kubwa kati ya Bingu wa Mutharika na Bakili Muluzi. Na mambo yanavyoendelea inaonekana kama Bakili anamtumia Sata ili kum-fix adui yake (Bingu) lakini anaweza kujikuta anatuhumiwa kwa kuingilia 'domestic politics' za nchi nyingine. Pupa nyingi sana!
 
Mnasikiliza upande moja tu, hivi hao Malawi miaka yote hiyo bado wanategemea kwa jirani kwa nini hawanunui jengo lao? Ushenzi mtupu sidhani kama na sisi Tanzania tunajibanza nje kwa jirani. Zambia washawapeleka mahakamani kina Chiluba et al sisi tunasubiri nini kuwashitaki Mkapa et al ambao wamelihujumu taifa? Tena huyu hata Kiwira aliiba .... ....
 
hata wewe una uhuru wa kusema fisadi papa na visasi vyake..........

Shabiki wa Manure khe he khe kheeeeeeeeeeeeeee anayejifichaficha ... ..... unakumbuka ule wimbo ''anza wewe na mi namaliza bora tusielewane vibaya'' ... I'm waiting seriously.
 
Mahusiano ya Kidiplomasia kati ya Malawi na Zambia yatalega lega,kihistoria Majirani hawa kusini mwa Afrika wana Nasaba,Watu wa Malawi wanaingiliana sana na watu wa Zambia na kuna familia zipo kiasili pande zote za Nchi hizi.Hapa kuna Jambo la kujifunza na haswa suala zima la nguvu za Rais.Rais Mteule wa Zambia Michael Chilufya Sata ni mtu wa visasi na mmtoa maamuzi yote mwenyewe bila kujali sana maamuzi ya washauri wake,Kwa kuwa Watanzania ni wapenda mambo ya haraka na ya mlipuko,Rais huyu (Labda kwa kuwa anatoka upinzani) amekuwa na upenzi mkubwa kutoka kwa Watanzania walio wengi,labda ni kutokana na maamuzi yake makubwa anayoyafanya kwa haraka.

Hapa naandika machache kuonyesha uharaka na utendaji kazi wa Rais Sata,haya ni maoni yangu binafsi nipo wazi kupingwa na kushauriwa kwa sababu tunajifunza kwa njia hii,Kwangu Mimi naona Afrika hatuhitaji Viongozi Wababe kama Sata bali tunahitaji Taasisi kama Bunge,Mahakama na Vyombo vya Ulinzi Imara.Hivi karibuni baada ya kuchaguliwa Rais Sata ameingia ktk mgogoro na Rais Mstaafu,Rupia Banda baada ya Sata kudai kuwa Banda ana asili ya Malawi na kwamba Mama yake Banda bado anaishi Malawi hata baada ya Banda kuwa Rais wa Zambia na sheria mojawapo ya kuwa Rais wa zambia ni lazima uwe mzaliwa wa Zambia na Wazazi wako wote wawili wawe ni Raia wa Zambia.

Rais Sata alifukuzwa (Deportation) Zambia mwaka 2007 baada ya kuonekana kuwa ziara yake hiyo binafsi ilikuwa na nia ya kwenda kusaidia upinzani dhidi ya serikali ya Bingu Wa Mutharika.Mwezi Oktoba 2011 Rais Sata alikataa kuhudhuria Mkutano wa Comesa kwa madai kuwa lazima serikali ya Malawi imuombe msamaha kwa sababu ya kitendo cha kufukuzwa Nchini humo mwaka 2007.Serikali ya Malawi ilikataa kufanya hivyo.

Mara baada ya kuapishwa Rais Sata aliwaomba radhi Angola kwa maelezo kuwa Serikali ya Mzee kaunda ilifanya kosa kubwa kuwasaidia UNITA na Jonas Savimbi,kwa maana hiyo anawaomba Msamaha serikali ya Angola kwa kosa hilo kubwa,alipobanwa na vyombo vya habari vya Nje Sata alidai amefanya uamuzi huo kwa sababu za kiuchumi,ni rahisi kununua mafuta Angola kuliko sehemu yoyote duniani.

Rais Sata mara baada ya kuanza kazi alimfukuza kazi Mkuu wa Ant-corruption Godfrey Kayukwa na nafasi yake kupewa Mwanamama Rosewin Wandi,sababu iliyotolewa ktk kumuondoa Kayukwa ni kwamba Taasisi hiyo ilishindwa kutoa majibu kwanini tenda ya kuchapisha nyaraka za Uchaguzi inapewa kampuni moja bila ushindani/mchakato (National printing group) kwa kipindi cha chaguzi mbili tofauti,hali hiyo ilionyesha kuwepo kwa rushwa ktk skuadi ya Ant-corruption.lakini ukweli wa mambo ni kwamba Ant-Corruption hiyo ilishawahi kumuhoji Sata (Alipokuwa raia wa kawaida) baada ya kumkuta ana jumla ya $ 500,000 ktk moja ya akaunti zake za Bank, Rais Sata pia alishawahi kuzuiwa Uwanja wa Ndege wa Johannesburg/Afrika kusini baada ya kukutwa anasafiri na kiasi kikubwa cha pesa.

Kwa kuonyesha kuwa Sata ni mtu wa visasi,na bado ana kinyongo na Malawi,Mwezi Oktoba ameamuru Redio moja ya Nchini Malawi isirushe Matangazo yake ndani ya Zambia,Redio hiyo inamilikiwa na Atupele Mtoto wa Aliyekuwa Rais wa Malawi,Mzee Bakili Muluzi.

Kwa hiyo maamuzi haya ya kupandisha Pango la Nyumba (Ubalozi) ni moja kati ya njia zake za kuikomesha Malawi,bado tutasikia mengi makubwa katika Utawala huu mpya wa Rais Michael sata.Lakini ni wazi kuwa masuala ya Nje na Diplomasia ya kimataifa kwa ujumla anahitaji ushauri madhubuti,vinginevyo Zambia itapoteza marafiki wengi.Kwani hata Muwekezaji mkubwa wa Zambia ktk Madini na sekta nyingine nyingi China wamekwisha kwaruzana nae,katika moja ya mikutano yake ya kampeni Sata aliwaita Wachina sio wawekezaji bali ni Wakoloni!


ndugu yangu umejitahidi sana kuanalyse though kuna mapungufu makubwa sana kwenye analysis zako....(kwa mtazamo wangu)
Kitendo walichokifanya Malawi kwa Sata ni kibaya sana, na kimsingi ilitakiwa Banda aliyekuwa Rais wa wakati huo(sasa hivi ni mpinzani) atoe tamko la kulaani kitendo hicho kwa kuwa kilimdhalilisha Mzambia sio tu Kiongozi mkubwa wa chama cha Upinzani, kitendo cha kunyamazia ufedhuli huo kilidhihirisha ushirika haramu wa Banda na Mutharika kwa ajili ya kuwanyanyasa raia wanaowapinga!!!Kitendo cha kujifanya wanamkaribisha leo akiwa Rais ni unafiki mkubwa unaotakiwa kukemewa na wapenda demokrasia wote...(kumthamini mtu akiwa na kitu na kumtupa akiwa hana kitu ni kiwango kikubwa cha kudhalilisha utu wa binadamu)...Chukulia mfano kama UK wamfukuze raia wa Ujerumani kama alivyofanya Mutharika kwa Sata, huo mgogoro utakuwa mkubwa dunia nzima!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! anachokifanya Sata sasa hivi ndo sawasawa..hakuna kumung'unya,hakuna visa vya kichinichini ila waziwazi akamuambia alichokifanya Mutharika kwa Mzambia hata angekuwa sio yeye binafsi hakitakiwi kabisa, kujilazimisha urafiki na Mtu anayedhalilisha raia wako ni unafiki na ufedhuli...ushirikiano wa nchi zetu uwe kwa manufaa ya raia wetu sio kuwabagua na kuwadhalilisha...


Mbili....Umeongelea kuhusu mfumo kuwa imara kwa maana ya mahakama,bunge na jeshi ndo kunaweza kuleta mabadiliko ya kimaendeleo kwa nchi NI SAWA kabisa ila lazima pawepo pa kuanzia...lazima awepo leader wa kulead mabadiliko hayo na mtu huyo ndiye Rais mwenyewe...nasikitika kukuambia kuwa weakness ya bunge leo na mahakama pamoja na watendaji wa serikali unatokana na kukosa mtu mwenye dhamira ya dhati ya kulead mabadiliko for the better,naomba nikupe mfano mdogo, CEO wa TIB Mr Noni amewaambia kamati ya bunge kuwa kuna watu walitumwa na vigogo wakachukue fedha pale bank (i.e. some billlions) nje ya utaratibu wa ukopeshaji wa kibank, na waliochukua pesa hizo ni pamoja na SImon group waliotumwa wakachukue UDA pia...Noni anaongea haya mambo bila kigugumizi kuwa walitumwa na vigogo!!!halafu anasema eti anawadai hawa watu wanakataa kumlipa,mi najiuliza anawadai vp wakati hakuhusika na mchakato wa kuwakopesha?????!!!remember hawa akina NONI ndo kati ya watalaamu wetu waliobobea ktk mabo ya banking...wameamua kuchakachuka akili kwa kuwa vigogo wamechakachuka akili. Ndugu yangu Mwawado unadhani mimi nikiwa Rais nitaendelea kufanya kazi na NONI???siyo rahisi hata kidogo..atakwenda kama vigogo wake walivyokwenda kwa sanduku la kura!!!!watu wanakuamrisha ufanye ufedhuli na wewe unajua fika kuwa huu ni ufedhuli basi wewe ni fedhuli zaidi ya waliokuagiza. Back to the topic, Zambia kumefanyika ufisadi wa hali ya juu sana, alisema mpaka kwenye ofisi ya Rais kuna mafisadi na wamejitajirisha kwa ufisadi leo unamtaka SATA awaombe ushauri ....thubutu wa kitu gani? huyu mtu wa kuzuia rushwa alikuwa wapi kukemea rushwa kwenye uchaguzi?eti aliwahi kumhoji SATA si alitumwa na Banda huyohuyo!leo Lema anavyokamatwakamatwa huko ARUSHA unataka tuwaamini polisi kuwa wanafanya HAKI???Ole sendeka alikuwa anatoka kwenye kesi kwa maandamano mpaka aliposhinda kesi yake, UVCCM wanaandamana bila vibali halafu Lema anakamatwa kwa kuwa ameongozana na wapiga kura wake toka mahakamani....eti mimi nikiwa Rais nitampigia makofi Mwema na vijana wake kuwa anafanya vyema!...never on earth!!!! wewe unasema ni mtu wa visasi,siyo visasi ni utendaji kazi thabiti usio na unafiki....mtu hafai piga chini, weka mwingine na baadaye watakujua kuwa hutaki mchezo na ndipo mfumo mzima utabadilika kama ulivyopendekeza kwenye uzi wako hapo juu...

Umesema China ni mwekezaji mkubwa pale Zambia, sawa ila wafuate utaratibu ili wazambie wafaidi uwekezaji wao...leo wachina wanashindana na machinga wetu kuchukua vizimba vya kuuza viatu kariakoo...eti wawekezaji? wapi bwana ni unyonyaji tu....unamshindanisha mbongo mwenye mtaji wa laki tano na mchina mwenye kiwanda kwao China!!for your informtion, ili wananchi wako wafaidi na uwekezaji wa wahindi na wachina lazima serkali iwe strictly sana na ifuate rules zote za uwekezaji na za vibali vya kufanya kazi hapa..(sasa hivi hata hapa kwetu hazifuatwi na wala hakuna aliye serious kuzifuatilia, namjua mhindi mmoja ni mtaalamu wa MS excel lakini ameajiriwa kama engineer na analipwa vizuri mara kadhaa ya mshahara wa engineer mtanzania!!!hajui kitu kingine zaidi ya kukusanya data na kuzicompile! ni kweli tunawahitaji watu wa hivyo???)

Mwacheni Sata asafishe nchi yake labda na wakwetu watajifunza kwake,natamani sana siku tupate Rais wa jamii ya Sata,asiye mnafiki na anayeweza kuyatenda anayoyaamini kuwa yatawaletea watu wake maendelo....hivi utasikitika ukisikia Mr Hosea ameondolewa nafasi yake pale PCCB?ufisadi upo kila sehemu tena wa waziwazi eti yeye anasema hawezi kwa kuwa wakubwa wanawalinda...yet hajiuzulu!tenda haki,simamia haki ,tekeleza unachokiamini ni sawa..ukipingwa ktk haki resign na historia itakukumbuka..i wish ningekuona au nikupigie simu maana nahisi unamiss facts nyingi sana kuhusu hili.
 
Mkuu Mwawado,

Heshima mbele, vile umesema upo tayari kupingwa kwa maelezo yako basi nikujibu kiungwana maana umekuwa mungwana sana. Tatizo la Afrika ni viongozi kupenda kutunza hali iliyopo. Watu walitegemea Sata aingie na kuacha mambo kama yalivyokuwa wakati wa Band.

Wazambia walimchagua Sata kwasababu ajenda zake zilikuwa wazi toka awali. Na yale anayoyafanya sasa ndio aliyokuwa anaahidi wakati wa kampeni. Sasa mlitaka atende tofauti na alivyoahidi. Standards za Zambia karibu kwa kila kitu ni tofauti sana na za Tanzania. Mwanasisas anaweza kudanganya hata maprofesa wa vyuo vikuu hapa TZ na wakampigia makofi, lakini mwanasiasa Zambia hawezi kuwadanganya undergraduate watamzomea live na kutoa nje.

Zambia bei ya sembe ikipanda wanaingia mtaani, watanzania wasomi ukipandisha bei ya petrol na umeme, wanaandika makala kuwa jamani hii ndio hali halisi duniani kote, tusiandamane tutavunja misingi ya amani aliyotuachia Nyerere. CHADEMA walisema inawezekana kushusha bei ya cement, Profesa wa Uchumi akasema hizo ni ndoto za mchana, lakini leo serikali inaposema itashusha bei ya cement, Prof huyo huyo anaisifia serikali kuwa inasikiliza matatizo ya wananchi wake, amesahau kuwa mwaka jana tu alipinga kuwa jambo hilo haliwezekani

Mbona watu hawajaandika kuwa hata baadhi ya maamuzi yaliyochukuliwa na serikali ya awamu ya nne yalikuwa dhahiri ya kulipa visasi. Yaani tumeweza kuona visasi vya Zambia ila hatujaviona visasi vya TZ.
 
Mwawado,
Nimekusoma ndugu yangu. Lakini sisi wengine tumevutiwa na mwanzo wa Sata kwa sababu amefanya ambayo yanahitaji kufanywa Tanzania.
Ametuonyesha kuwa kumbe inawezekana. Sasa kama yeye kafanya kwa visasi au kukurupuka, hiyo sisi tunaotaka kuona mabadiliko Tanzania hatujui na haituhusu. Lakini kwa kuwa hatujakata tamaa kwamba Tanzania bora isiyo na ufisadi inawezekana, tumevutiwa na mwanzo wa Sata Zambia. Hivi sasa CCM wana mipango ya kurithishana madaraka na kulindana jambo ambalo linaendelea kuididimiza nchi yetu kiuchumi na kimaadili. Tunahitaji rais ambaye atakuwa mkali, atakayechukua hatua ngumu, atakayewafukuza kazi baadhi ya maafisa bila kuwaangalia usoni na kuweka uoga mioyoni kwa wale wanasubiri na kutamani kuwa mafisadi wapya.
 
Kiongozi mzuri,anatoa maamuzi maguma.Pia ha cheki cheki ovyo.
 
Acha Sata asafishe Zambia. Katika miaka mitano Zambia itaimarika sana kiuchumi kutokana na kuwa na uongozi makini.
 
Back
Top Bottom