Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,257
- 105,389
Eti unashinda library kusoma mambo unayotaka, huo tunauita ni u much know.....
Ulikuwa unaenda off topics kwa sababu hakuna vitu kama hivyo O level hata A level ya Tanzania, mimi nina syllabus na past papers karibu za mitihani yote tangu 1990 hakuna swali hata moja la Drake's equation kawadanganye wengine si mimi mzee.
Nyie endeleeni tu kubishana na endorsement yenu ni siku ya pili sasa mnazozania neno moja kama mazuzu lakini ukija kwenye namba hupati kitu.
Ukikaa on topic mara nyingi kugundua kitu vigumu, kugundua kitu kipya mara nyingi ni muhimu u transcend topic.
Ndiyo matatizo yetu, tunakariri vitu, curiosity zero. Halafu tunategemea tutafanyaje kitu kipya ?
endeleo, elimu ni mchakato wa kuendeleza
Kama hizo syllabus ni Rosetta Stone ya knowledge kwa nini zinabadilishwa kama nguo ?
Eti unasoma past papers, unasoma au unakariri wewe ? Unasoma ili ushinde mitihani ?
Mifumo ya tabia inayopalilia maendeleo inataka watu wabunifu, waasi. Elimu ni sehemu muhimu ya kupalilia hizi tabia. Lakini elimu hii ni lazima iwe aina ya elimu inayomfanya mwanafunzi agundue ukweli wake yeye mwenyewe, siyo elimu inayomlisha kwa kijiko huyu mwanafunzi kwamba "ukweli ni huu" na "mambo ya muhimu ni haya". Katika mifumo ya tabia inayodumaza maendeleo, elimu ni mchakato wa kuendeleza mapokeo tu (dogma) na kutoa wafuasi na waumini tu, bila ya kutoa kitu kipya.
Mimi sikutaka kuwa mfuasi na muumini tu, nilitaka kujua ukweli kwa juhudi zangu mwenyewe.
Hili ni moja ya matatizo makubwa ya mfumo wetu wa elimu.