Nina flyer ya mtandao wa Zain kuna unlimited data Bundle 100,000/= Lakini kuna fine print "fair usage will apply" kuna mtu ametumia hii service anaweza kutuambia kama ni unlimited au limit yake ni ngapi?
Mkuu Goshen hao Zain wanfanya kiasi gani kwa mb?
Na speed yao vipi kwa hiyo 3G.
Leo mimi nilikuwa nafuatilia kwenye ofisi zao, kwa hiyo bando, wao wana 3G, ambayo waliniambia ni sawa na 3GB, bahati mbaya nimesahau spidi yake ni ngapi, kwa upande wa Zantel wanafanya 129tshs/mb kwa mahesabu yangu ya haraka nikaona zain ni nafuu kuliko zantel kulinganisha na vodacom 200tshs/mb. Hiyo 3GB kuimaliza kwa matumizi ya kawaida sio rahisi ila kwa kudownload movies haichukui round, kwa namna fulani hiyo slogan ipo sahihi na upande mwingine siyo sahihi
Mkuu Goshen Bongo internet bado bei mchapo sana tena balaa sasa hiyo laki moja kwa mwezi duh maumivu.Nimekuta China wao unalipia $120 kwa mwaka kwetu hapa hiyo ni mwezi kweli maumivu.