Zain africa challenge 2010 na vyuo vyetu TZ.

Mimi naomba nianze kwa kuwatetea vijana wetu...kushindwa kwao kujibu maswali vizuri mbele ya kadamnasi ya watazamaji wa TV karibia Afrika nzima,hakumaanishi kwamba vijana wale hawana uwezo. Mara nyingine tension ya kuwa quizzed mbele ya TV waweza kuingia kiwewe,na hio sio kwao tu,wapo watu wazoefu waliowahi kujikanyaga kwenye kujibu maswali (mfano Obama wakati wa moja ya debate zake na bibi Clinton wakati wa primaries za US aliwahi kuchemsha). Labda huko nimekwenda mbali,tuangalie humuhumu kwenye jamii forum ni wangapi wanahofu ya kujikanyaga kwa hoja zao kiasi kwamba wanaamua kushiriki katika mijadala kwa kutumia majina ya bandia~mimi nikiwa mmoja wao).

That said nirejee kwenye hoja ya msingi kuhusu kushuka kwa viwango vya elimu. Nakubaliana na wote kwamba ni kweli viwango vyetu vimeshuka na responsibility ya kushuka viwango hivyo ni makundi (3).
1) serikali (kwa kutoweka na kusimamia viwango vya elimu-hali hii imepelekea mashule kutokuwa na waalimu bora; vitabu vya kufundishia; maabara za sayansi na miundombinu inayofaa.

2) Jamii (kwa kushindwa kutoa kipaumbele katika masuala ya elimu. Jamii ingekuwa proactive katika kuchangia elimu, kufanya tathmini ya viwango na kutoa ushauri sahihi na kujitolea kufundisha vijana wetu pale ambapo kuna pengo la waalimu. Jamii ya Kenya, Ghana-ime institutionalize zoezi la kuchangia elimu over and above serikali inavyofanya (harambee), wakati wenzetu wana fundraise kwa ajili ya kupata fees za kusomesha watoto sisi tuna fundraise kugharimia harusi za watoto. Ukiachilia NGO chache kama Haki elimu, wanajamii hatuna utamaduni wa kutoa constructive criticism/ideas juu ya kuboresha elimu na pia kama. Jamii hatujaweza kujitolea kuwasaidia wanafunzi wetu...while tumekazania kuwataka makondakta wawasaidie wanafunzi kusafiri kwenye mabasi,sijawahi kusikia wanachama wa chama cha mainjinia kikijitolea kufundisha hesabu kwa wanafunzi wetu katika kipindi cha likizo, sijaona tukijitolea as community service ku spend 20hours per year kwenda kufundisha shule ya kijijini kwetu au mtaa wetu. Laiti kila msomi Mtanzania angejitolea masaa 20 tu kwa mwaka kuwafundisha vijana wetu...walau tungepiga hatua. Ukiangalia masaa tunayotumia kwenye vikao vya harusi,kitchen party,sherehe zenyewe, misiba, socializing kwenye vilabu kwa wastani kwa mwaka yanazidi masaa ishirini tunayoongelea. Hatuhitaji kusubiria volunteers kutoka Korea na Peace Corps waje, tuanze wenyewe...

Kundi la mwisho ni la wazazi. Hivi kweli mzazi unahitaji serikali ije nyumbani kwako kusimamia homework za watoto wako? Wangapi tuna spend muda nyumbani kukagua maendeleo ya shule ya watoto wetu na kutoa mwongozo? Katika hili twaweza kuwasamehe wale wazazi ambao hawakupata fursa ya kusoma, lakini wapo wasomi wengi tu ambao hawana muda wa kusimamia watoto wao?

Kwa hali hiyo tatizo la viwango vya elimu linatokana na sababu pana zaidi ambazo sote tuna wajibu wa ku play our part.

Kama unadhani wale vijana wa Arusha uwezo wao mdogo, subiria miaka 12 ijayo, mtakapowaona vijana walio product za hizi shule za kata zenye waalimu walioandaliwa kwa mfumo wa fast-tracking...huko kutakuwa worse zaidi.

My worries sio vijana hao kushindwa kushiriki katika competition ya ZAIN, bali nahofia kama watamudu ushindani katika fursa za kazi,pale watakapokuwa wanashindana na wenzao wa Afrika Mashariki

sijakuelwa?yaani wanashindwa kujibu kwa kuwa na tensio wanaonekana kwenye TV??mbona wanaweza kuongea kwa simu?SIJAKUELEWA
 
Bw/Bi. Pareto hoja zako ni maridhawa, ila nakataa hoja yako ya kuwatetea vijana kwa kisingizio cha kupata homa ya quiz. Homa hiyo kwanini waipate wao tu?

Nways, hoja yako kuhusu jamii kukosa mwamko wa elimu ni ya ukweli kabisa. Lakini hatua tuliyoifikia kama nchi ni kuvunjika kwa social and economical structures, hususan suala la kipato. Ktk hali kaa usitegemee chochote kitatengemaa mkuu.
 
Dahh nimekaa natazama kipindi cha Zain Africa challenge kati ya University of Ghana na University of Arusha,kwa kweli ni aibu vijana wetu hawana uelewa wa mambo kabisa yaani wanabaki kubun buni tu majibu...I felt very bad and disturbed

Hiyo ni picha ya elimu yetu Tanzania. Tunapiga soga sana na kupenda njia za mkato kwa kila kitu hata kuandika notisi za darasani na matokeo yake ndiyo hayo!
 
Mi niliswitch channel mara tu kilipoanza..nilijua kwamba kitatokea nini
 
Dahh nimekaa natazama kipindi cha Zain Africa challenge kati ya University of Ghana na University of Arusha,kwa kweli ni aibu vijana wetu hawana uelewa wa mambo kabisa yaani wanabaki kubun buni tu majibu...I felt very bad and disturbed
wajichagulie zawadi wenyewe hapa hao wanafunzi wa Arusha University
01.gif
02.gif
04.gif
03.gif
17.gif
18.gif
19.gif
21.gif
09.gif
10.gif
11.gif
13.gif
12.gif
14.gif
15.gif
16.gif
06.gif
05.gif
20.gif
22.gif
23.gif
24.gif
27.gif
26.gif
25.gif
28.gif
29.gif
07.gif
30.gif
31.gif
32.gif
33.gif
34.gif
35.gif
37.gif
08.gif
39.gif
40.gif
50.gif
47.gif
 
wote nimewasikia na what you've commented with the university students of tz.
bwana ukwweli ni kwamba elimu zetu za kibongo ni ile ya mtaala ulioachwa na waingereza... wa kumfanya mwanafunzi aje awe mtumikishwaji... na sio mtumiaji wa hiyo elimu aliyo pewa chuoni ( yaani kufanya vitu kwa kujitegemea na sio lazima aajiriwe. so kutokana na hiyo elimu ya kutegemea na kukariri vyuoni mwetu na ndo mana wanachemsha na huo ndo mwanzo lets chect it out.. ni vyuo vichache sana ambavyo kuna watu wenye ufahamu mkubwa na wanatumika sana..sasa ni wakati wizara ya elimu kuangalia na kutathmini nini mstakabali wa wanfunzi hao. si mnaona wa form four...
 
Wanaweza kuipata kama in their school life hawajawahi kusimama mbele ya darasa hata kupresent something. Vyuo vyingi huwa wanapresent final year project only....hasa hasa mainjinia na wanafunzi wa sayansi. Sina habari sana na wafunzi wa arts.....wengine wanaweza kutujuza.

Bw/Bi. Pareto hoja zako ni maridhawa, ila nakataa hoja yako ya kuwatetea vijana kwa kisingizio cha kupata homa ya quiz. Homa hiyo kwanini waipate wao tu?

Nways, hoja yako kuhusu jamii kukosa mwamko wa elimu ni ya ukweli kabisa. Lakini hatua tuliyoifikia kama nchi ni kuvunjika kwa social and economical structures, hususan suala la kipato. Ktk hali kaa usitegemee chochote kitatengemaa mkuu.
 
Dahh nimekaa natazama kipindi cha Zain Africa challenge kati ya University of Ghana na University of Arusha,kwa kweli ni aibu vijana wetu hawana uelewa wa mambo kabisa yaani wanabaki kubun buni tu majibu...I felt very bad and disturbed
Mbona nimesikia kwenye muhutasari wa magazeti asubuhi kuwa University of Arusha imeingia nusu fainali au ilikuwa geresha? Na kama wameingia watakuwa wameingiaje kwa jinsi mnavyowakandia? Tatizo kubwa la vijana wa siku hizi ni tamthilia za kwenye TV k.v Second chance, Prison break and many others from southern America. Sisi tulikuwa na debate kwa sababu wakati wa jioni kabla ya prep ndo kilikuwa kiburidisho lakini sasa hivi ni TV. Tusiwalamu wao bali tujilaumu sisi wazazi na viongozi tunaowajengea hayo mazingira ya kukesha kwenye TV without even taking a look on his/ her exercise book.
 
Hivi serikali huwa inapitia mijadala Kama hii jaman hapa ndio tungeweza kupata pa kuanzia juu ya uchakavu wa mitaala yetu

Nje ya Mada sijui kigogo huyu n Yule wa kule twitter

Sent using Jamii Forums mobile app
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom