Bilionea Asigwa
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 16,510
- 28,416
Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), imesema kuwa wanafunzi 3,000 kati ya takriban 40,000 waliomba kujiunga na vyuo mbalimbali nchini, wamekosa udahili kutokana na kuwa na kasoro mbalimbali.
Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Sifuni Mchome, aliliambia gazeti la MWANANCHI kuwa wanafunzi 37,000 walituma maombi yao kwa usahihi kupitia mfumo unaojulikana kama 'Central Admission System'.
"...niliangalia na kuona wanafunzi 40,000 wamefanya maombi, hao 3,000 ndiyo wenye makosa mbalimbali (kwa mfano), wengine wameingia tu na kufikiri ndiyo wameshafanya maombi (kuna) na makosa mengine..." alisema Profesa Mchome na kuongeza: "Barua pepe ambazo zitakuwa zimewarudia ni vyema wakazifanyia kazi kabla ya siku ya mwisho ambayo ni Juni 30, (2012)."
Alisema kuwa Julai 6, 2012, TCU itakutana na vyuo ili kupitia majina ya waombaji ambapo Julai 15 watakaa na kufanya udahili kamili kwa kuwapangia wenye sifa kwenye vyuo walivyoomba, "Nawaambia wanafunzi wasubiri huo udahili wa Julai 15," alisema Profesa Mchome.
Katika hatua nyingine, Wakuu wa vyuo na wadau wengine wa Vyuo Vikuu, walikutana jana jijini Dar es Salaam kujadili mfumo wa pamoja wa tuzo (University Qualification Framework). Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kujadili mfumo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Selestine Gesimba, alisema mfumo huo utasaidia kuweka viwango sawa vya mafunzo yanayotolewa na vyuo vikuu vyote nchini.
Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Sifuni Mchome, aliliambia gazeti la MWANANCHI kuwa wanafunzi 37,000 walituma maombi yao kwa usahihi kupitia mfumo unaojulikana kama 'Central Admission System'.
"...niliangalia na kuona wanafunzi 40,000 wamefanya maombi, hao 3,000 ndiyo wenye makosa mbalimbali (kwa mfano), wengine wameingia tu na kufikiri ndiyo wameshafanya maombi (kuna) na makosa mengine..." alisema Profesa Mchome na kuongeza: "Barua pepe ambazo zitakuwa zimewarudia ni vyema wakazifanyia kazi kabla ya siku ya mwisho ambayo ni Juni 30, (2012)."
Alisema kuwa Julai 6, 2012, TCU itakutana na vyuo ili kupitia majina ya waombaji ambapo Julai 15 watakaa na kufanya udahili kamili kwa kuwapangia wenye sifa kwenye vyuo walivyoomba, "Nawaambia wanafunzi wasubiri huo udahili wa Julai 15," alisema Profesa Mchome.
Katika hatua nyingine, Wakuu wa vyuo na wadau wengine wa Vyuo Vikuu, walikutana jana jijini Dar es Salaam kujadili mfumo wa pamoja wa tuzo (University Qualification Framework). Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kujadili mfumo huo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Selestine Gesimba, alisema mfumo huo utasaidia kuweka viwango sawa vya mafunzo yanayotolewa na vyuo vikuu vyote nchini.
NB
DEADLINE YA KUFANYA MAREKEBISHO NI TAREHE 30 JUNE 2012 KAMA UNA DOGO MWAMBIE ACHUNGULIE ASIJE KOSA CHUO
SOURCE:GAZETI LA MWANANCHI
DEADLINE YA KUFANYA MAREKEBISHO NI TAREHE 30 JUNE 2012 KAMA UNA DOGO MWAMBIE ACHUNGULIE ASIJE KOSA CHUO
SOURCE:GAZETI LA MWANANCHI