Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,296
- 18,892
Joseph Selasini Phenomenon Politicion,
Mwishoni mwa miaka ya tisini nilikutana na na vijana kadhaa wa vyama vya siasa Tanzania waliokuwa ziarani marekani chini ya udhamini ya PUSH RAINBOW ya Rev Jesse Jackson. Nilikuwa Chicago katika mihanganiko yangu, tukawawa tumefikia hoteli moja na vijana wale. basi nikawakaribisha kinywaji jioni moja huku tukiongea siasa za Tanzania. Kulikuwa na kijana mmoja wa kike kutoka CCM, na wengine wote wa kiume aakiwamo mmoja wa NCCR-Mageuzi (alikuwa Selasini), wa CUF mmoja, UDP mmoja sikumbuki majina yao; nadhani CHADEMA haikuwa na mwakilishi. Yule binti wa kike wa kihaya nilikuwa namfahamu kwa vile wakati anasoma UDSM nilikuwa bado nipo pale, na nilihappen kumfahamu binafsi kutokana na mambo yake binafsi ya mitaani kule ARISA enzi hizo. Baada ya vijana kukata laga chache za Milwahukee, vijana wakaanza kumwaga sera zao; nilicheka sana jinsi Salasini alivyokuwa akiwafunika wenzake wote katika kuelezea sera za chama chake na mstakhabali wa Taifa wakati huo, mpaka jamaa wanaomba wasiendelee kuongea siasa tena. Yule kijanwa wa kike yeye alikuwa anashukuru CCM sana kwa vile ilimfanya afike Marekani!!.