Kama kuna mambo watanzania wengi walikuwa wanatarajia kutokana na utabiri feki wa sheikh Yahya basi kuona uchaguzi mkuu unasimama kama ilivyotokea mwaka 2005.Uzushi wa mtabiri huyu ni kuwa mmoja wa wagombea wa urais angekufa kabla ya tarehe ya uchaguzi.Lakini uchaguzi umepita na hakuna lililotokea.Sijui yuko wapi sasa kujibu nini kimetokea.Sisi tusioamini uzushi ule tulijua hakuna kitu kama hicho.Watanzania wawe makini na mtu huyu.