Yuko wapi Ramadhan Ally Kihiyo?

Nimemkumbuka sana wanajamvi Mh Kihiyo aliyekimbia ubunge Temeke kwa kuulizwa mwalimu wake wa darasa...Mwenye mawasiliano naye atujuze yuko wap Mheshimiwa??
 
Nimemkumbuka sana wanajamvi Mh Kihiyo aliyekimbia ubunge Temeke kwa kuulizwa mwalimu wake wa darasa...Mwenye mawasiliano naye atujuze yuko wap Mheshimiwa??
Kihiyo yupo anaishi Tabata Mawenzi-Dar; anaishi maisha ya ubabaishaji, anatapeli watu kwa kujiita Mbunge mstaafu. Ana skendo kibao za kiutapeli alafu ni miongoni mwa watu walioanzisha chama cha siasa kinachojulikana kama CHAUMA; anatembea na Briefcase ndani yake anajaza kadi za CCM na CHAUMA.
 
Kihiyo yupo anaishi Tabata Mawenzi-Dar; anaishi maisha ya ubabaishaji, anatapeli watu kwa kujiita Mbunge mstaafu. Ana skendo kibao za kiutapeli alafu ni miongoni mwa watu walioanzisha chama cha siasa kinachojulikana kama CHAUMA; anatembea na Briefcase ndani yake anajaza kadi za CCM na CHAUMA.
Ukibahatika kupata picha yake tuwekee hapa, kwani ni mtu muhimu aliyeongeza msamiati wa kiswahili-kihiyo" :asiyejua kitu; muongo, mbabaishaji etc
 
Hiyo Ilikuwa ni miongoni mwa kesi zilizompatia umaarufu mkubwa sana bwana Lamwai, Bwana Kihiyo alidanganya kuwa alisoma Dar Tec, huo Ubunge wa Temeke ulimtia umaskini sana Bwana Kihiyo, kwani kabla ya kugombea aliuza daladala zake mbili na nyumba na akawekeza kwenye ubunge ambao aliangushwa mahakamani

uchaguzi ule wa Temeke ulikuwa na msisimko sana, kwani mpinzani wa Mrema alikuwa Sicso Mtiro mtoto wa mjini ambaye baadae alikuja kuwa chief protocal wa Kikwete kabla ya kuamishiwa Ubalozini,

Mrema kwa upande wake bado alikuwa kwenye ile peak yake huku akiwa na mtaji wa Sheikh Mtopea
Marehemu Mtopea alitokea tawi la NCCR la KWAZULU NATAR lililokuwa mtoni kichanga.
 
Lakini watu wengi wanadhani kihiyo inamaanisha mtu mwenye elimu ndogo, kumbe inamaanisha mtu aliyeghushi cheti kuonesha kiwango cha Elimu asichonacho!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom