IsayaMwita
JF-Expert Member
- Mar 9, 2008
- 1,127
- 140
- Thread starter
- #21
Nakubalina na wewe kabisa. Hii amani tunayodanganyiwa ndiyo inayotuponza na tunachezewa kama watoto wadogo. Tusipochagua kuingia mitaani na baadhi yetu kuwa tayari kutolewa kafara hatuendi popote na ni vyema tukakaa kimya tu na kwaacha mafisadi watese.
Noamba wanaharakati waunganishe watu waingie barabarani, huu ndio ukombozi uliobakia kwa mtanzania. Tusiangalie sana nani atakuwa Raila wetu, maadam sasa hayupo tuanze tu kidogo kidogo kisha material condition itatupatia mtu, awe anatoka CCM ama kwingineko hatutajali sana.
Amkeni watanzania, haki kamwe haipatikani kwenye sahani, haki inapiganiwa.
Mavanza;
Mkuu, hakika umenena, umenena muungwana, kweli ni lazima wengine wetu tujitoe kafara kwa faida ya kizazi kijacho, haiwezekani Mafisadi wazidi kuneemeka huku hatima ya watoto wetu haijulikani, haiwezekani mitoto ya mifisadi ndiyo iifaidi nchi hii, haiwezekani ndugu yangu, ila tutampata wapi Raila wa nchi hii?