Yuko Wapi Mzee Mwanakijiji?

Status
Not open for further replies.
Asalaam Aleikhum.. kupo nipo nipo ila haya mambo ya kijijini ya kutumia mtandao kwa simu kwa kweli sijayazoea. Nitarudi mjini muda si mrefu tumekuja kusalimia wakwe kidogo. Ukiondoa cellphones zilizozagaa.. kijijini hakujabadilika, duka la mzee Mswahili bado lipo pale pale, ile nyumba kwenye kona kwenda shuleni iko vile vile kama inataka kudondoka.. ila huko mjini utadhani niko Detroit!

MKUU;
Bora umejitokeza maana watu walikuwa wakifikiri umenunuliwa na mafisadi. Pole inaonekana ulilowea mjini, sisi tulishazoea sana maisdha ya Bush, kwani hiyo ndiyo Bongo yetu.

Uasipime maisha ya Mjini ni tofauti kwa asilimia 900 na yale ya kijijini Utadhani ni nchi mbili tofauti, kumbe moja.

Najua hujabahatika kunywa chai toka umefika kijijini, kama umekunywa basi ni kwa visenti vyako ulivyotunza kwa ajili ya kuwasaidia wazazi huko kijijini, au kutokana na hali ilivyo umesingizia swaumu.

Hali hii yote inatokana na kile tunachokipingania kila siku, tunachokilalamikia kila kukicha, tunachokazania kukiondoa hapa nchini. UFISADI
 
Ila sisi wengine tuki ondoka hata hatu tafutwi!!
inategemea na quLITY ya mchango wako.....mara nyingi wengi wetu tunatumia ile haki yetu ya uhuru wakujieleza na kuandika, Mwanakijiji hutumia pia haki hiyo na moyo wakujitolea nguvu na akili zake katika kuusaka ukweli wa mambo, sasa na wewe ukiitaka hiyo hadhi anza sasa kutumia muda wako kuitumikia nchi yako kwa nguvu na akili zako ili ukitoweka humu jamvini watu waulizane kulikoni?
 
Asalaam Aleikhum.. kupo nipo nipo ila haya mambo ya kijijini ya kutumia mtandao kwa simu kwa kweli sijayazoea. Nitarudi mjini muda si mrefu tumekuja kusalimia wakwe kidogo. Ukiondoa cellphones zilizozagaa.. kijijini hakujabadilika, duka la mzee Mswahili bado lipo pale pale, ile nyumba kwenye kona kwenda shuleni iko vile vile kama inataka kudondoka.. ila huko mjini utadhani niko Detroit!

Mkuu MwKjj, karibu tena ukumbini.

Bila shaka umeiona hali halisi ya kijijini na tunategemea michango ya maoni humu jamvini itazingatia hali halisi ya maisha ya mtanzania wa kawaida.
  • Bila shaka utaelewa kwa nini tunakubali kupokea zawadi za fulana, khanga na kofia wakati wa uchaguzi,
  • kwanini tunapokea bahasha za posho (sitting allowance) kwenye vikao hata kama ni cha muda mfupi tena palepale kazini kwako,
  • utaelewa kwa nini tunakubali kulipiwa gharama zetu kwenye mikutano mikuu ya uchaguzi wa vyama vyetu na kisha kupokea per-diem kwa ajili hiyohiyo,
  • Pia hutaendelea kushangaa kwamba mtanzania anayelipwa $50 kwa mwezi anaweza kumudu gharama za maisha hadi mwezi unaofuata!
Kuhusu kutumia mtandao kwa cellphone, wanacharge/MegaByte na wakati mwingine credit kwenye simu inaisha kabla hujamaliza kusoma na hasa kipindi hiki ambapo Invisible ameweka graphics kuashiria mfungo wa Ramadhani.
 
Asalaam Aleikhum.. kupo nipo nipo ila haya mambo ya kijijini ya kutumia mtandao kwa simu kwa kweli sijayazoea. Nitarudi mjini muda si mrefu tumekuja kusalimia wakwe kidogo. Ukiondoa cellphones zilizozagaa.. kijijini hakujabadilika, duka la mzee Mswahili bado lipo pale pale, ile nyumba kwenye kona kwenda shuleni iko vile vile kama inataka kudondoka.. ila huko mjini utadhani niko Detroit!

pengine ndivyo walivyo! ukikuta mtu ambaye mawazo yake hayavuki masaa ya chakula cha usiku au mchana, usifikiri anaweza kubadilika haraka.

we have to think beyond the next meal meal!

msalimie baba mkwe!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom