Naloli
JF-Expert Member
- Aug 26, 2010
- 416
- 81
Kipindi cha kampeni hadi kipindi cha kupiga kura ambapo zoezi la uchaguzi lilikamilika, kulikuwa na wapiganaji wa CCM wakitetea chama chao hata ktk mambo yasiyostahili utetezi, kiasi watu wakawa wanatilia shaka ufahamu wao. Baada ya zoezi la uchaguzi mkuu kukamilika baadhi yao wametoweka na tumebakiwa na JEYKEY WA UKWELI, MTU WA PWANI na wengineo je Huyu MALARIA SUGU mpiganaji wa CCM aliyetubeza kuwa Baada ya Uchaguzi mkuu wale SUPPORTERS wa DKT SLAA na upinzani hasa CDM hawataonekana hapa JF. Nakumbuka "nilimwambia kuwa sisi ni watetezi wa ukweli na haki, natunamsupport mtu tuaminie ndie mtetezi wa wanyonge na suluhisho la UFISADI na hata CCM wakiiba kura sisi tuteendeleza mapambano humu JF na nchi nzima na kampeni za DKT SLAA ndio zimewasha moto wa mapambano rasmi". Sasa uchaguzi umepita wapiganaji bado tupo humu JF lakini ajabu MALARIA SUGU katoweka yeye, JE kazi aliyotumwa humu JF ameimaliza?