Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
:A S-heart-2:Ninamsaka Cheusi, Cheusi wangu Mangala,
Mtoto kama mdosi, asopenda masihala,
Naona kama kaasi, sioni zake makala,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:First Ladi nahisi, umemficha mahala,
Ninazo pia tetesi, kwa Preta analala,
Rose mtingisha nyusi, yu wapi wangu Mangala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Kila mlo ukakasi, sipati hamu ya kula,
Cheusi njoo upesi, niepe huu msala,
MadamT mkwasi, ni yupi kwangu mbadala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Nakuuliza Demsi, ijibu hii makala,
Ninagona kama fisi, usiku nianapolala,
Chapachapa mikamasi, nalowesha matambala,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Mangala wangu Cheusi, nijuze pako pahala,
Nachekwa kandamnasi, mapenzi yanifanya ****,
Nitajitwanga risasi, nipumzike kwa Mola,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Kaditama yangu pasi, kwako Cheusimangala,
Una utamu wa tasi, laini kama salala,
Sukari kama fenesi, sehemu gani walala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
Mtoto kama mdosi, asopenda masihala,
Naona kama kaasi, sioni zake makala,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:First Ladi nahisi, umemficha mahala,
Ninazo pia tetesi, kwa Preta analala,
Rose mtingisha nyusi, yu wapi wangu Mangala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Kila mlo ukakasi, sipati hamu ya kula,
Cheusi njoo upesi, niepe huu msala,
MadamT mkwasi, ni yupi kwangu mbadala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Nakuuliza Demsi, ijibu hii makala,
Ninagona kama fisi, usiku nianapolala,
Chapachapa mikamasi, nalowesha matambala,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Mangala wangu Cheusi, nijuze pako pahala,
Nachekwa kandamnasi, mapenzi yanifanya ****,
Nitajitwanga risasi, nipumzike kwa Mola,
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.
:A S-heart-2:Kaditama yangu pasi, kwako Cheusimangala,
Una utamu wa tasi, laini kama salala,
Sukari kama fenesi, sehemu gani walala?
Ni siku kenda sijala, kwa kumkosa Cheusi.