Elections 2010 Yote yamekuwa lakini hili lazima!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Wananchi wa Tanzania naomba niseme hivi,Yote yamekuwa Tunamshukuru mungu nachotaka kuwashukuru watanzania wenzangu nikuhusu usikivu,Busara,Hekima,Unyenyekevu, yote nikuonyesha watanzania walivyokuwa wakomavu wasiasa!Tanzania bara wananchi wamekuwa wastaarabu na wameonyesha ukomavu wa wakidemokrasia alikadharika Tanzania Zanzabar wamekomaa kisiasa na Demokrasia imekuwa kwa zanzibar nimewapongeza na kila mpenda amani Tanzania nilazima awapongeze kwa hatua waliyoifikia!
Tanzania bara nimefurahishwa kwakuwa wasikivu japo sikuzote wanao leta vurugu katika nchi ni Vyama vilivyoko madarakani!Tumeshuhudia jinsi NEC ilivyofanya madudu kwakuchelewesha matokeo!.Hapakuwepo na sababu yakuchelewesha!
Watanzania kama kwakitu nilicho jivunia niustarabu wetu na wote najua tumezingatia amani ya nchi yetu na pili tumeweka maslahi ya nchi mbele!Amani nikitu cha kwanza hata wangeshinda upinzani bila amani nikazi bure!
Amani ikishapotea nimda mrefu kurudisha amani lakini ni mda mfupi kupoteza amani!
Tumeshuhudia Rwanda,Drc,Burundi,Uganda kwa yeyote ambaye anajua kutoweka kwa amani nilazima hatakuwa tayari kupoteza amani!Namshukuru Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa kutuunganisha nakutufanyatuwe kitu kimoja!
Ila nachukua Flusa hii kuwambia wote waliokuwa wakieneza udini miskitini wasirudie kwani vita ya udini haina suruhisho!Nawale waliokuwa wanaeneza Makanisani nawao pia!
Nawale waliokuwa wakieneza ukabila wasifanye hivyo kwani amani ikitoweka chuki itakuwa hata kwa vizazi vyao na siyo kwa sasa!
Mwisho nawapongeza wote walioshinda kwakupitia Upinzani nadhani viongozi waliopo madarakani watakuwa wamepata somo nini maana ya "PEOPLE POWER"

Amani iwejuu ya Tanzania.ungu ibariki Tanzania:pray2:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom