Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
Wanawake wengi watapata maambukizi haya katika maisha yao. Maambukizi haya huwasha, ni chungu lakini ni rahisi kutibu. Walio na ugonjwa wa Sukari huambukizwa haraka kwa sababu ya sukari nyingi katika damu yao. Pia kwa wanao ugua Ukimwi. Daktari atakupa madawa ya kutibu.
Nini dalili za maambukizi ya kuvu?
Unatibu vipi maambukizi haya.
Kama umewahi kuambukizwa basi unaweza kununua kirimu ya anti-fungalna ujipake, ikiwa hujawahi kuambukizwa basi muone daktari akushauri.
Utazuia vipi maambukizi ya ukungu
Nini dalili za maambukizi ya kuvu?
- Kuwashwa ndani na nje ya uke.
- Golegole nzito yenye gamu kutoka kwenye uke
- Uchungu au hali ya kuchomeka unapokojoa au kushiriki ngono
- Ngozi iliyogeuka nyekundu sehemu ya uke
- Golegole inayotoka katika uke yenye harufu mbaya
- Ishara kujitokeza juma moja kabla ya kwenda hedhi.
Unatibu vipi maambukizi haya.
Kama umewahi kuambukizwa basi unaweza kununua kirimu ya anti-fungalna ujipake, ikiwa hujawahi kuambukizwa basi muone daktari akushauri.
Utazuia vipi maambukizi ya ukungu
- Wacha kutumia dawa za kuua bakteria - antibiotics ikiwa si lazima
- Kunywa maziwa mala - yorghurt kupiga vita bakteria
- Usivae chupi zinazokubana sana. Vaa chupi za nyuzi za pamba na zisizikubane
- Osha mikono na iwe imekauka kila wakati
- Jaribu usitumie marashi, poda na sabuni za marashi kuosha sehemu nyeti
- Osha sehemu nyeti kila mara na uhakikishe umekausha vizuri
- Jaribu kuimarisha kiwango cha sukari katika damu yako
- Tumia kondomu na wacha kushiriki ngono ukitumia midomo.