Yawezekana mmesahau, lakini JK aliahidi kutushughulikia wanajamvi baada ya uchaguzi

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Katika hotuba yake ya kukubali kuwa mgombea Uraisi kwa tiketi ya CCM hivi karibuni, JK alionyesha kukerwa na majamvi ambayo yamekuwa mstari wa mbele katika kukosoa mwelekeo wa serikali yake.

Vile vile katika hotuba hiyo, JK alionyesha kughafilishwa na wafadhili ambao ndiyo huwasikiliza "watetea utawala bora" tajwa na aliahidi ya kuwa atawashughulikia wote mara baada ya uchaguzi.

Sina uhakika kama wafadhili JK ataweza kuwashughulikia huku ametuahidi kuendelea kuwapigia magoti ili wambebe kwenye mbeleko zao za misaada na mikopo lukuki ahadi zake za JK za "Maisha Bora kwa Kila Mtanzania."

Kauli hizi za kibabe ziliashira JK alikuwa akitarajia ya kuwa yeye na CCM itaibuka kidedea.

Lakini nasi Mwenyezi Mungu alituahidi yafuatayo:-


Isaiah 54:17 "No weapon formed against you shall prosper, and every tongue which rises against you in judgment you shall condemn. This is the heritage of the servants of the LORD, and their rightness is from ME." Says the LORD"

Vile vile tunahamasika na kutambua mipaka ya mwanadamu pale Mwenyezi Mungu aliponena yafuatayo kwenye:-

PROVERBS 16:9 "You may make your plans, but GOD directs your actions."

SOTE TUSEME AMEN...............
 
Back
Top Bottom