LUCIFER
Senior Member
- Aug 14, 2012
- 183
- 88
Kuna habari kwamba Waziri Mkuu aliyejiuzuru nafasi hiyo kutokana na kashfa ya mkataba tata wa Richmond, Edward Lowasa anajiandaa kuwekeza katika klabu ya Yanga kupitia kwa mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji, ambaye ni swahiba yake mkubwa kibiashara, kama moja ya njia za kumnusuru katika mipango yake ya kuelekea ikulu mwaka 2015.Jaribio la Lowassa kuingia Yanga lilianza kwa utawala wa mwenyekiti wa klabu hiyo aliyejiuzulu, Lloyd Nchunga,ambapo alidaiwa kwamba Lowasa aliomba kuingiza kiasi cha shilingi 800 milioni hasa wakati Manji ambaye alikuwa ndiye mfadhili mkuu wa klabu hiyo, alipogoma kutoa msaada kwa Yanga, lakini Lloyd Nchunga alikataa, linadaiwa kutomfurahisha Lowassa na watu wanaomuunga mkono akiwamo Manji na Rostam Aziz ambaye naye anaelezwa kuwa ni mpenzi wa Yanga.Itakumbukwa wakati wakisuguana na Manji baada ya mfadhili huyo kujiweka pembeni kama mfadhili wa klabu hiyo na baadaye kuonekana akijaribu kujiingiza kwa kutumia mgongo wa wazee wa klabu waliotaka kukabidhiwa timu, Nchunga alihoji wazee hao wangepata wapi fedha zakuendeshea klabu hiyo na akasema hawezi kukabidhi timu kwa watu ambao hajui itaishia mikononi mwa nani kwani huenda wazee hao wanataka kuikabidhi timu hiyo kwa wafanya biashara wa mihadarati.Ingawa hakuwa amemtaja mtu,lakini kauli hiyo ilionekana kuwaudhi wazee hao na kudai Nchunga amewatusi na kumtusi Manji hivyo watahakikisha anaondoka madarakani kwa njia yoyote na ndicho kilichotokea.Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya klabu ya Yanga, njama za kuondolewa kwa Nchunga zilitokana kushindwa kufuata matakwa ya matajiri wa klabu hiyo wanaodai wana mpango wa kuifanya Yanga kuwa tajiri, lakini liwe lengo la kujipatia vyeo nchini kutokana na historia ya kuhusika kwake na harakati za uhuru wa Tanzania tangu Tanganyika.Inadaiwa Lowassa anataka pia kuwa karibu na watu wenye sauti kwenye chama cha mapinduzi visiwani Zanzibar akiwemo mama Fatma karume ili kumsaidia kupata umaarufu na kujijenga visiwani, tayari kwa kuwania urais. Inafahamika kwamba viongozi wengi wa Baraza la mapinduzi Zanzibar wana mapenzi na timu ya Yanga kutokana na timu hiyo kuwa na urafiki na timu ya za Afrika Sports na Miembeni tangu wakati wa harakati za kuwania uhuru wa nchi hizi mbili na Lowassa ameliona hili.Inadaiwa kazi ya kumsafishia Lowassa njia ya kuingia kwenye enzi ya klabu hiyo, inafanywa na Yusuf Manji ambaye jukumu lake kubwa alilonalo ni kuhakikisha anaibadili Yanga kuwa kampuni, na kwa kutumia udhaifu wa wanachama na wapenzi wa Yanga kutotaka kujua kinachoendelea katika klabu yao, isipokuwa waifunge Simba tu ama kuchukua ubingwa,ndiyo sababu ambayo wenye fedha wameeleza kuwa ndiyo njia rahisi ya kumpachika Lowassa awe mmoja wa wadhamini wa klabu ya Yanga pamoja na kuwepo kwa madai ya muda mrefu kwamba Lowassa ni Simba damu.Lakini u-simba wake kwa mujibu wa vyanzo vya habari utafunikwa na fedha ambazo atazimwaga klabuni Yanga na ikiwa njia ambayo pia ilitumiwa na mtu mwengine aliyewahi kuingia kwenye uongozi waklabu hiyo, Seif Ahmed Magari ambaye licha ya wanaojua kwa asilimia mia moja niSimba, lakini alitumia udhaifu wa kutochimbua mambo kwa wanayanga na kwa kuwa yeye ni mfanyabiashara wa magari mwenye fedha, akajifanya anaongoza kutoa msaada kwa wanayanga, kumbe nia ilikuwa kuingia Yanga ili ahalalishe ujanjaujanja wake katika biashara zake.Miongoni mwa mambo ambayo yatafanywa Yanga ni pamoja na kuvunja jengo lililojengwa na Karume na Maalimu Nyerere nakulifanya la kisasa zaidi ambapo litajengwa kama lile la Quality Business Centre ambapo ndani yake kutakuwa na uwanja wa kisasa, maduka makubwa na kila aina ya starehe ambako kwa mawazo yao wanaamini watakuwa wamewamaliza wanachama ambao hamu yao ni kuiona Yanga inashinda na kuwa na vitega uchumi, lakini kwa wao lengo lao lilikuwa ni kumweka Lowassa kwenye kiti cha urais mwaka 2015.ANOTHER MOVIE….hayawale Mnaojiita WANAZI WA YANGA MUTIMU WA MAPESA MPO?SOURCE: AFRICA LEO, 8[SUP]th[/SUP] of August, 2012.