Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Leo chama cha wananchi CUF kinampokea mwenyekiti wake Prof. Lipumba, wanachama wengi wa CUF wanatarajia mwenyekiti wao kuja kukinusuru chama chao na mgogoro/mpasuko unaowasumbua!
Wakati haya na yale yakiendelea ndani ya CUF wafuasi wengi wa CCM na CHADEMA haswa wa CHADEMA wamekuwa wakishangilia kumomonyoka kwa CUF.
Tatizo ninaloliona kwa watanzania wengi ni kwamba hawatambui kiini au chanzo haswa cha kumomonyoka kwa CUF na laiti kama wangejua chanzo wale wote wanaoicheka CUF wasingethubutu kufanya hivyo hata kidogo badala yake wangewashauri viongozi wao ili kuepuka hilo balaa la kumomonyoka kama ambavyo CUF inamomonyoka leo hii.
Ndugu zangu chanzo cha mgogoro CUF ni kile kinachoitwa "strictly party discipline" kitu ambacho karibia kila chama nchini wanacho, Kilichowondoa Hamad Rashid CUF ni "strictly party discipline" kinachowavuruga CUFU ni "strictly party discipline" kitakachoenda kuiua CHADEMA kesho ni "strictly party discipline" na kitakachoiua CCM keshokutwa ni "strictly party discipline"
Ushauri wangu kwenu wanachama wa vyama vya siasa hebu jaribuni kuwashauri viongozi wenu wapunguze "strictly party discipline" la sivyo vyama vyote vitakwenda na maji eti!
Wakati haya na yale yakiendelea ndani ya CUF wafuasi wengi wa CCM na CHADEMA haswa wa CHADEMA wamekuwa wakishangilia kumomonyoka kwa CUF.
Tatizo ninaloliona kwa watanzania wengi ni kwamba hawatambui kiini au chanzo haswa cha kumomonyoka kwa CUF na laiti kama wangejua chanzo wale wote wanaoicheka CUF wasingethubutu kufanya hivyo hata kidogo badala yake wangewashauri viongozi wao ili kuepuka hilo balaa la kumomonyoka kama ambavyo CUF inamomonyoka leo hii.
Ndugu zangu chanzo cha mgogoro CUF ni kile kinachoitwa "strictly party discipline" kitu ambacho karibia kila chama nchini wanacho, Kilichowondoa Hamad Rashid CUF ni "strictly party discipline" kinachowavuruga CUFU ni "strictly party discipline" kitakachoenda kuiua CHADEMA kesho ni "strictly party discipline" na kitakachoiua CCM keshokutwa ni "strictly party discipline"
Ushauri wangu kwenu wanachama wa vyama vya siasa hebu jaribuni kuwashauri viongozi wenu wapunguze "strictly party discipline" la sivyo vyama vyote vitakwenda na maji eti!