Yanayotokea CUF leo yatatokea CHADEMA kesho na CCM keshokutwa!

Dijovisonjn

JF-Expert Member
Nov 14, 2011
466
125
Leo chama cha wananchi CUF kinampokea mwenyekiti wake Prof. Lipumba, wanachama wengi wa CUF wanatarajia mwenyekiti wao kuja kukinusuru chama chao na mgogoro/mpasuko unaowasumbua!
Wakati haya na yale yakiendelea ndani ya CUF wafuasi wengi wa CCM na CHADEMA haswa wa CHADEMA wamekuwa wakishangilia kumomonyoka kwa CUF.
Tatizo ninaloliona kwa watanzania wengi ni kwamba hawatambui kiini au chanzo haswa cha kumomonyoka kwa CUF na laiti kama wangejua chanzo wale wote wanaoicheka CUF wasingethubutu kufanya hivyo hata kidogo badala yake wangewashauri viongozi wao ili kuepuka hilo balaa la kumomonyoka kama ambavyo CUF inamomonyoka leo hii.
Ndugu zangu chanzo cha mgogoro CUF ni kile kinachoitwa "strictly party discipline" kitu ambacho karibia kila chama nchini wanacho, Kilichowondoa Hamad Rashid CUF ni "strictly party discipline" kinachowavuruga CUFU ni "strictly party discipline" kitakachoenda kuiua CHADEMA kesho ni "strictly party discipline" na kitakachoiua CCM keshokutwa ni "strictly party discipline"

Ushauri wangu kwenu wanachama wa vyama vya siasa hebu jaribuni kuwashauri viongozi wenu wapunguze "strictly party discipline" la sivyo vyama vyote vitakwenda na maji eti!
 
"strictly party discipline" This term is too General.Samahani mdau hebu funguka zaidi,unalenga kipi hasa kwa kusema hivyo?
 
"strictly party discipline" This term is too General.Samahani mdau hebu funguka zaidi,unalenga kipi hasa kwa kusema hivyo?

Mkuu 2naposema "strictly party discipline" tunamaanisha kuwa kiongozi yeyote wa chama haswa mbunge hawezi kufanya jambo au kuongea kitu ambacho chama chake hakitaki kusikia, mfano sio kweli kwamba wabunge wote wa CHADEMA hawapendi ongezeko la posho ila kutokana na "strictly party discipline" inawabidi wasilipende hilo ongezeko! au sio wabunge wote wa CCm wanapenda kuitikia NDIYOOOOOOOOOOOO!!! kwa kila jambo wanapokuwa bungeni ila kwa 7bu ya "strictly party discipline" wanafanya hivyo.
Sasa tuje kwa ndugu
hamad Rashid, mbuge huyu kidemokrasia hana kosa lolote ila ki "strictly party discipline" ana kosa kubwa sana, katika "strictly party discipline" kiongozi unapoona tatizo uruhusiwi kuliongea itakubidi usubiri vikao vya vyama ndo uliongee hata kama vikao vitafanyika after 6 month!!!
sidhan kama wabunge wote kwa maisha yote watakubali hii hali, kipindi hiki mbunge aliyeichoka hii hali alikuwa wa CUF next atakuwa wa CHADEMA then wa CCM
 
Chadema iko kwenye level nyingine kabisa!! We use brains to support Chadema, hatufanyi kwa kutaka kupewa msamaha wa kodi au kupewa vyeo au kuonea wengine! ni kwa mapenzi mema na nchi yetu!! Najua kuna watu wenye tabia za viongozi wa CCM ndani ya CDM lakini upepo unawafanya wajiulize mara 10. So, watchout your mouth!!
 
cjakushawishi kwa 7bu hutaki kushawishika! hv ulishawah kujiuliza ni kwa nini wabunge na masaneti wa USA wanafanya kazi kwa uhuru zaidi na kuwawakilisha wananchi wao ipasavyo? jibu ni dogo sana, ni kwa sababu hawafungwi na mdudu anayeitwa "strictly party discipline" sasa ni kwa nini na sisi na vyama vyetu tusiwaondolee wabunge wetu "strictly party discipline" ili watuwakilishe sisi kwa 100% na si kwa 30% wanavyofanya kwa sasa?
 
  • Thanks
Reactions: EMT
sikipondi chama chochote kile cha siasa lia ninachofanya ni kutaka kila mtu ajue naiwazia nini Tanzania. Unaweza kudhani kuwa CHADEMA wapo sawa lakin wataalam wa masuala ya siasa hatuangalii uimara wa jana na leo bali tunaangalia mfumo mzima wa chama! Hebu kama utaweza nipe tofauti ya mfumo wa vyamavya siasa vya CCM, CHADEMA na CUF
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Leo chama cha wananchi CUF kinampokea mwenyekiti wake Prof. Lipumba, wanachama wengi wa CUF wanatarajia mwenyekiti wao kuja kukinusuru chama chao na mgogoro/mpasuko unaowasumbua!
Wakati haya na yale yakiendelea ndani ya CUF wafuasi wengi wa CCM na CHADEMA haswa wa CHADEMA wamekuwa wakishangilia kumomonyoka kwa CUF.
Tatizo ninaloliona kwa watanzania wengi ni kwamba hawatambui kiini au chanzo haswa cha kumomonyoka kwa CUF na laiti kama wangejua chanzo wale wote wanaoicheka CUF wasingethubutu kufanya hivyo hata kidogo badala yake wangewashauri viongozi wao ili kuepuka hilo balaa la kumomonyoka kama ambavyo CUF inamomonyoka leo hii.
Ndugu zangu chanzo cha mgogoro CUF ni kile kinachoitwa "strictly party discipline" kitu ambacho karibia kila chama nchini wanacho, Kilichowondoa Hamad Rashid CUF ni "strictly party discipline" kinachowavuruga CUFU ni "strictly party discipline" kitakachoenda kuiua CHADEMA kesho ni "strictly party discipline" na kitakachoiua CCM keshokutwa ni "strictly party discipline"


Ushauri wangu kwenu wanachama wa vyama vya siasa hebu jaribuni kuwashauri viongozi wenu wapunguze "strictly party discipline" la sivyo vyama vyote vitakwenda na maji eti!


Kweli vyama kupanda na kushuka ni jambao la kawaida, ila Hapo kwenye red umekosea CCM mbona ishakufa!
 
Chadema iko kwenye level nyingine kabisa!! We use brains to support Chadema, hatufanyi kwa kutaka kupewa msamaha wa kodi au kupewa vyeo au kuonea wengine! ni kwa mapenzi mema na nchi yetu!! Najua kuna watu wenye tabia za viongozi wa CCM ndani ya CDM lakini upepo unawafanya wajiulize mara 10. So, watchout your mouth!!
Dijovisonjn hoja yake inasimama! Ni hoja nzito tena yenye mshiko na mantiki kubwa sana. Wale madiwani wa Arusha kilichowatoa CHADEMA ni nini? Nasikia walikuwa wanauliza mantiki ya wao kuzuiwa kuhudhuria vikao vya "full council" wakati wenzao ambao pia hawakumtambua Kikwete kama Rais wanahudhuria vikao vya bunge na vyeo vya kibunge wamegawana. Hoja yao badala ya kujibiwa wakaishia kutimuliwa!!

wabunge wa CHADEMA hawamtambui Kikwete kama Rais lakini wanahudhuria vikao vya Bunge na vyeo vya kibunge wamegawana, lakini wenzao ambao walikuwa hawamtambui Meya wa Arusha wanawazuia wasihudhurie vikao vya Halmashauri ya Arusha na kuwazuia wasipewe vyeo vya kidiwani. Hapo utaona kwa kuwa kwenye ngazi za juu za CHADMEA wabunge ndiyo wenye maamuzi, jambo lao haliwaletei matatizo bali kwa madiwani ambao walikuwa hawana nguvu hiyo kwenye chama walitimuiliwa.
 
Ila hii ipo all over the world....chama ni taasisi...kina katiba na kanuni....you are not forced to join any,if u decide to join that means u have just agreed to abide to the constitution and all bylaws....
mbona vyama vya wenzetu western haviyumbi?
tatizo ni kubwa kuliko hizo strickly party discipline....
hapa kuna chama kikubwa kama CCM chenye resources then kuna vyama vidogo ambavyo resources zake ni michango ya watu wachache....what do u think
kwa nchi changa kidemocracy kama yetu strictly party discipline sio issue kubwa sana,NA Mara nyingi imetumika kuhodhi madaraka kwa wachache wenye nguvu na kuwakandamiza wengine.
 
Ila hii ipo all over the world....chama ni taasisi...kina katiba na kanuni....you are not forced to join any,if u decide to join that means u have just agreed to abide to the constitution and all bylaws....
mbona vyama vya wenzetu western haviyumbi?
tatizo ni kubwa kuliko hizo strickly party discipline....
hapa kuna chama kikubwa kama CCM chenye resources then kuna vyama vidogo ambavyo resources zake ni michango ya watu wachache....what do u think
kwa nchi changa kidemocracy kama yetu strictly party discipline sio issue kubwa sana,NA Mara nyingi imetumika kuhodhi madaraka kwa wachache wenye nguvu na kuwakandamiza wengine.

Nadhani kidogo wewe utakuwa umenielewa, ni kweli "party discipline" ipo nchi nyingi sana duniani (sio zote mfano USA hawana) nilichokuwa nakiongerea ni kitu kilichoifikisha CUF hapa ilipo kuwa ni "strictly party discipline" (naomba nieleweke kwanza kuwa "strictly party discipline" ni tofauti na "party discipline") vyama vyetu vyote vina "strictly party discipline" kitu ambacho kidemokrasia sio kizur ndo maana nikawaomba wale wafuasi na wanachama wa hivi vyama wawashauri viongozi wao wapunguze u-"strictly party discipline" ili yaliyotokea CUF yasitokee na kwao!
 
CDM na CUF wahalandani hata kwa chembe!
Kifo cha CUF ilikuwa wazi na wenye uelewa walijua kuwa CUF inakufa na itazikwa 2015 rasmi
 
Ukitaka kujua kama vyama vya siasa hapa Tanzania vinafanana au la hata usipate shida hebu angalia party structure zao wote kisha angalia mfumo wao ukoje, naamini utagundua kuwa wooooooooooooooooooooote wamecopy na kupaste toka CCM ila wao wakaondoa mashina tu.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
CDM na CUF wahalandani hata kwa chembe!
Kifo cha CUF ilikuwa wazi na wenye uelewa walijua kuwa CUF inakufa na itazikwa 2015 rasmi

Utasubiri sana hadi umri wako wa kuishi utakapoisha na cuf utaiichana ikinawiri
 
Aliyeiua CUF ni Maalim Seif kwa kukubali kuolewa na CCM full stop, mengine yote ni mbwembwe tu.
 
Back
Top Bottom