TandaleOne
JF-Expert Member
- Sep 4, 2010
- 1,644
- 709
Mheshimiwa Rais atoa hotuba kali kwa vijana ambayo inalenga kuwajenga na kuwataka wafanye tathmini ya kutosha kwa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi wa ngazi ya Taifa ya Jumuiya hiyo ya Vijana.
Alianza kwa kuwakumbusha Ibara ya 5 ya katiba ya chama cha mapinduzi ambayo inaeleza MALENGO NA MADHUMUNI ya CCM.,ambapo imeelezwa kwenye ibara hiyo kuwa madhumuni ya CCM ni "kushinda katika uchaguzi wa serikali kuu na Mitaa"
Lakini pia akaeleza kuwa CCM kinategemea Jumuiya yake hii kufanya kazi ya siasa miongoni mwa vijana wa TANZANIA na kuwashawishi wakubali kuwa wanachama na wapenzi wa CCM. Akasisitiza kuwa matumaini makubwa ya msingi kuliko yote ya Chama Cha Mapinduzi ni kuona jumuiya yake hii inakuwa MKOMBOZI wa vijana.
Akawataka wahakikishe kuwa wanapata Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti na viongozi wengine ambao wataongoza vyema,watakaoongoza juhudi za kuendeleza, kutetea na kulinda maslahi ya CCM. Viongozi wanaoijua na kuipenda jumuiya ya Vijana.
Na pia akawataka baada ya uchaguzi wajipange kutimiza wajibu wao kwa jumuiya yao na Chama kwa Ujumla..,
HOTUBA INAENDELEA....
Alianza kwa kuwakumbusha Ibara ya 5 ya katiba ya chama cha mapinduzi ambayo inaeleza MALENGO NA MADHUMUNI ya CCM.,ambapo imeelezwa kwenye ibara hiyo kuwa madhumuni ya CCM ni "kushinda katika uchaguzi wa serikali kuu na Mitaa"
Lakini pia akaeleza kuwa CCM kinategemea Jumuiya yake hii kufanya kazi ya siasa miongoni mwa vijana wa TANZANIA na kuwashawishi wakubali kuwa wanachama na wapenzi wa CCM. Akasisitiza kuwa matumaini makubwa ya msingi kuliko yote ya Chama Cha Mapinduzi ni kuona jumuiya yake hii inakuwa MKOMBOZI wa vijana.
Akawataka wahakikishe kuwa wanapata Mwenyekiti, Makamu mwenyekiti na viongozi wengine ambao wataongoza vyema,watakaoongoza juhudi za kuendeleza, kutetea na kulinda maslahi ya CCM. Viongozi wanaoijua na kuipenda jumuiya ya Vijana.
Na pia akawataka baada ya uchaguzi wajipange kutimiza wajibu wao kwa jumuiya yao na Chama kwa Ujumla..,
HOTUBA INAENDELEA....
Ndugu zangu mimi kama mwanaCCM nipo ndani ya huu mkutano mkuu wa uchaguzi ndani ya jumuiya hii ya chama lakini yanayotendeka humu ndani kwa kweli sikubaliani nayo na ndio mana hata CHADEMA wanapotusema nje ni vema tukawa waungwana na kukubali kuwa ni vema tukajaribu kubadilika lakini ni vigumu mana tunaendelea kuwahadaa watanzania kuwa tupo kuwatetea wao.
Mimi nipo ndani ya CCM hapa katika kikao hiki lakini siungi mkono vitendo vya rushwa vinavyoendelea kuitafuna CCM mpaka sasa ndio matokeo yanatangazwa ya washindi wa uchaguzi lakini ukweli ni kwamba wanatangazwa waliofanikiwa kutoa fedha na kuweza kuchaguliwa sasa hiki ni chama gani kama mpaka utoe fedha ndio uchaguliwe.
HUU NDIO UCHWARA UNAOENDELEA KUWAPA UMAARUFU WAPINZANI WETU PALE TUNAPOKUWA WAGUMU KUJIREKEBISHA.
HAPA NDIO MATOKEO YANAANZA KUTANGAZWA PUNDE NITAYAJUMUISHA HUMU ILA TUNASIKITISHWA MAANA BILA KUWA NA PESA HUWEZI ONGOZA UVCCM NA KWELI VIJANA TUMEONESHA MFANO MBOVU MANA TUMESHINDWA KUSHIKAMANA NA KUTETEA SWALA LA RUSHWA.
MATOKEO YA MWENYEKITI NI WIZI MTUPU MTU KWA SABABU ANAO UWEZO WA KUTOA PESA KATOA NA KAPITA DUUUUUUUUUUU NAUMIA HAPA KAMA NIMLUKIE LUKUVI MANA NDIO ANATANGAZA MATOKEO MANA NAPATA HASIRA SANA.
MWENYEKITI SADIFA MAKAMU MBONI MHITA HAYA NDIO MATOKEO YALIYOPANGWA NA WANAOJIITA VIGOGO WA CHAMA MIMI KWELI NASEMA KAMA TUNAHITAJI KWENDA MBELE NA CCM YETU VEMA TUBADILIKE .