Yanayojiri bunge maalumu la katiba leo tarehe 21.03.2014, dodoma...

Status
Not open for further replies.

A4.

JF-Expert Member
Mar 16, 2014
670
108
Leo ni siku ambayo mh. Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kulihutubia bunge maalumu la katiba. Hotuba yake inakuja baada ya kutanguliwa na hotuba mbili zilizotolewa na; Jaji mstaafu Warioba ambae alitoa hotuba ya maoni ya wananchi juu ya rasimu ya katiba mpya akiwa kama mwenyekiti wa tume hiyo na Amosi Wako ambae ni seneta kule nchini kenya msomi aliyebobea kwenye sheria aliyepata mafunzo hayo chuo kikuu cha dar es salaam (UDSM) kuanzia miaka ya 1969 na pia ni mwanasheria mstaafu wa serikali ya kenya kama alivyo Andrew Chenge wa Tanzania. Alitoa presentation iliyohusu katiba ya kenya namna ilivyopatikana na changamoto walizokumbana nazo. Pia wajumbe 16 wa bunge maalumu la katiba waliweza kumwuliza jumla ya maswali 48, akiwepo mzee Kingunge ambae swali lake lilivuta hisia za wajumbe wengi, na maswali yote yalijibiwa. Je leo ni nini kitajiri? Usikose kufuatilia hapo jioni saa kumi kupitia media mbalimbali nchini tanzania kama tv,radio na mitandao ya kijamii kama hii.

=====
Fuatilia hapa live

https://www.jamiiforums.com/katiba-...-hotuba-ya-rais-uzinduzi-wa-bunge-maalum.html
 
Anataka awe wa kwanza ku-post habari hii.

kweli kabisa naona kila siku post zangu zinaunganishwa kwa kina Skype, Simiyu yetu, n.k wanaopost saa sita ya usiku. Leo nimewawahi ili nifuatilie vizuri huku kama umeme utakatika....
 
Haayaa asiye na mwana aweke jiwe. Je leo Kikwete ataheshimika kitaifa na kimataifa au ndio atalikorogo na kufuta mazuri yote aliyo yafanya toka awe Rais. Je chama chake chenye madai ya kipumbafu ya serikali mbili ambayo kimsingi kiutendaji aiwezekani ila kinadharia na kibabaishaji inawezekana. Je ni siku ambayo tutamzomea hilooo!!! Kikwete atambuwe kwamba wananchi wa sasa si wale wa 1969. Nasubiri kufahamu kama nina Rais au sanamu. Je CCM itamzika kikwete leo??
 
Mambo manne atayazungumzia raisi.
Mosi; muundo wa serikali,
pili; sakata la posho,
tatu; vurugu bungeni
 
Audi A4. unanifanya niwafikirie watu wanaoamka usiku wa manane kupanga foleni za kuchota maji. Wewe utakuwa umeweka jiwe kwenye foleni. Teh teh teh
 
Last edited by a moderator:
kweli kabisa naona kila siku post zangu zinaunganishwa kwa kina Skype, Simiyu yetu, n.k wanaopost saa sita ya usiku. Leo nimewawahi ili nifuatilie vizuri huku kama umeme utakatika....

Utawala wa sheria huzingatia maoni ya kila mwananchi. Hali kadhalika jf inazingatia utawala wa sheria kwa wajumbe wake ndiyo maana inaruhusu kila mjumbe kujiandikia kila apendalo hata kama ni uongo kwa mtindo wa kujumuisha na wasiohusika. Asubuhi njema bana.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom