VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Leo mtoto hatumwi dukani.Leo, asiye na mwana aeleke jiwe.Leo,ukigeuka nyuma unakuwa jiwe la chumvi.Leo,macho mbele kama tochi. Leo,masikio na macho ni marafiki muhimu. Leo, kila kitu kina watu;wale wastaarabu na fyatu.Usisubiri kusimuliwa.Jionee au sikiliza mwenyewe leo.
Kwa nyaraka zilizopo,shughuli hiyo itakuwa jioni.Leo,Bunge la Katiba linafikia vifungu vya 37,38 na 39 vya Rasimu ya Kanuni za Bunge hilo ili kuvipitisha.Vifungu tajwa,pamoja na mambo mengine, vinazungumzia namna ya upigaji kura wa kupitisha Rasimu ya Katiba utakavyokuwa ndani ya Bunge hilo.Wapo wa KURA YA SIRI na KURA YA WAZI/DHAHIRI. Leo watajulikana vyema.
Lazima leo Bunge liamue kupitisha au kuviondosha vipengele hivyo vya Kanuni. Ni leo.Si kesho. Lakini, kupitisha SIRI au DHAHIRI kutafanywa kwa SIRI au DHAHIRI? Mwenyekiti wa muda ataongozwa na Kanuni au Taratibu zipi leo kuamua kuendesha kura za SIRI au DHAHIRI wakati itakapojitokeza haja ya kufanya hivyo? Leo kitaeleweka tu.Zege halilali!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
--------------
Kwa nyaraka zilizopo,shughuli hiyo itakuwa jioni.Leo,Bunge la Katiba linafikia vifungu vya 37,38 na 39 vya Rasimu ya Kanuni za Bunge hilo ili kuvipitisha.Vifungu tajwa,pamoja na mambo mengine, vinazungumzia namna ya upigaji kura wa kupitisha Rasimu ya Katiba utakavyokuwa ndani ya Bunge hilo.Wapo wa KURA YA SIRI na KURA YA WAZI/DHAHIRI. Leo watajulikana vyema.
Lazima leo Bunge liamue kupitisha au kuviondosha vipengele hivyo vya Kanuni. Ni leo.Si kesho. Lakini, kupitisha SIRI au DHAHIRI kutafanywa kwa SIRI au DHAHIRI? Mwenyekiti wa muda ataongozwa na Kanuni au Taratibu zipi leo kuamua kuendesha kura za SIRI au DHAHIRI wakati itakapojitokeza haja ya kufanya hivyo? Leo kitaeleweka tu.Zege halilali!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (sasa Dodoma)
--------------
Wadau, nikiwa hapa Bungeni Dodoma, Mwenyekiti wa Muda wa Bunge Maalum anawatahadharisha wajumbe juu ya hatari ya kunyoosheana vidole kwa itikadi za kisiasa. Ufafanuzi huo umetolewa baada ya Mheshimiwa Ole Sendeka kumshutumu waziri wa Katiba na Sheria wa Zanzibar, Abubakar Hamisi Bakari kuwa ana maslahi ya chama chake cha CUF. Sendeka alisema hivyo kutokana na Abubakar ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Kanuni kukataa majedwali ya marekebisho ya Sendeka na Ummy Mwalimu kwa madai kuwa hayakuwasilishwa kwenye kamati.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni Prof Mahalu ameeleza kuwa kulijitokeza makosa kwenye sekretarieti na kwamba aliwaomba wabunge waendelee kujadili vifungu hivyo pamoja na hiyilafu zilizokitokeza.
Binafsi nilikuwa sijawahi kumuona Mh. Pandu Kificho akiongoza mkutano wowote. Kutoka moyoni,hakuna spika mwenye hekima,busara,uvumilivu na upendo niliyewahi kumuona katika umri wangu kama Kificho. Kinachotokea bungeni {utovu wa nidhamu kwa baadhi ya wabunge} ni malezi ya hovyo {sio ovyo} waliyopata wabunge wetu toka kwa walezi wao. Mnaokataa kataeni habari ndiyo hiyo. Tutegemeeni siku 150 wakiwa bungeni kwa sababu tu ya utovu na ukosefu wa hekima. Nimekuwa nasema elimu na hekima ni vitu tofauti kabisa.
Jana bunge liliahirishwa kwakuwa wabunge walidai wamechelewa kupewa nakala ya sheria namba 32 hadi 43. Leo bunge limeahirishwa kwa sababu secretariet imetoa majedwali mawili ambapo jedwali moja halionyeshi majina ya akina Mwalimu na Sendeka.
Kwa vyovyote vile wazembe wanajulikana na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa dhidi yao.
Kama mwendo huu utaendelea kila siku bunge litakuwa linaahirishwa huku posho zetu waamka taabani zikiendelea kuliwa.
Ushauri wa bure kwa kamati ya kanuni, waandae sheria ya mpito kwamba hapo bungeni yeyote atakaeonekana kuanzisha vurugu asilipwe posho. Na kwa njaa walizonazo hao watu utaona kama watafanya tena fujo.
Kuna tabia nyingine imezuka ya watu kupiga tu kelele za kuzomea hata kama jambo linaweza kuzungumzika na majadiliano yakaendelea. Hili mimi naona linasababishwa na baadhi ya wabunge wanaotaka bunge kiahirishwe ili wakafanye starehe zao. Dawa ya hawa watu ni kuwawekea monitor atakaeandika majina ya wapiga kelele ili yanapotokea mazingira ya hivyo, majina yanasomwa then kama kawaida wanakatwa posho.
Haya yasipofanyika, hakuna rasimu wala katiba mpya hapo mjengoni. Tutarudi mwaka 77 kuendelea na zilipendwa. Kikwete alisema 'mkileta utoto hatutapata katiba mpya. Na kwa vile nchi haiwezi kuendeshwa bila katiba tutarudi kwenye katiba ya zamani'
Bungeni: Waandishi wa Habari Makanjanja
Ndivyo mchangiaji aliemaliza punde alivyosema katika Bunge hili la katiba waandishi wa habari ambao ni Makanjanja wasipewe nafasi na wanyimwe vibali vya kutoa taarifa za Bunge kule Dodoma wakati bunge linaendelea.,
Mjumbe mmoja ambaye ni mwakilishi wa Taasi zisizo za kiserikali (NGO) Mustapha ,kawa mbogo kwa madai ya Kua Mwenyekiti wa Bunge la Mabadiliko ya Katiba anapendelea na kuendeshwa na vyama vya siasa na watu maarufu kwa kuwapa nafasi za kutoa hoja huku akiwasahau wajumbe 201 walioteuliwa na Raisi na kujiona hawana wanachokifanya kwnenye Bunge hilo.
Je ni kweli Mwenyekiti anapendelea.
Mnyika kachangia kuhusu mavazi rasmi kachangia vazi la kitenge liongezwe mwenyekiti wa kamati ya kanunii kamkubalia. duuu bi kiroboto kaibuka anachangia anamkrash mnyika kwamba mavazi ya vitenge yasiruhusiwe kachangia pumba infact bi kiroboto yuko shallow.
kuna jamaa kakrash skafu kamtolea mfano. savimbi wa bongo. Mmoja kaibuka na vazi la kimasai nalo vipi liruhusiwe? Bi. sarungi kaja na mambo ya urembo wa asili nazani anamaanisha aruhusiwe kuvaa culture zake. Yaani kuna vituko kidogo.
Nassari kaongelea kwamba unadhifu ni kuvaa kimagharubi vazi la kitenge lisiruhusiwe labda huko kwenye kamati.