Za sahizi wanajamii. Ni siku nyingi sijajiunga nanyi lakini leo ninahitaji msaada wenu wa mawazo. Nina uhusiano wa mapenzi na msichana mmoja toka 2007. Ni muda mrefu sana lakini kinachonishangaza moyo wangu unajiuliza mara mbili mbili kumuoa najiuliza sana kwanini. Ila tatizo kubwa ana wivu sanaaa umepitiliza kabisa kiasi kwamba vitu vidogo anasema nimemcheat anataka tuachane bila ushaidi. Kuna kipindi flani nilinyimwa unyumba kwa zaidi ya miezi 8 nikamwambia sitakuja kumuomba unyumba daima.
Kiukweli bado nampenda lakini nakereka sana vitu vidogo anasema tuachane imezidi sana. Kutokana na umbali wa ninapoishi nimejikuta na uhusiano na msichana mwingine ambao si wa mapenzi na huyu dada anatambua kuwa nina msichana. Mwezi wa 7 nilikua nimepanga kumvisha pete huyu mpenzi wangu lakini kabla ya muda kufika akaja ghafla mkoa akakuta msg za yule rafiki yangu ikawa balaa akampigia simu yule dada akamwambia sisi ni marafiki tuu.
Hakutaka kuamini akachukua vitu vyake vyote akaondoka zake. Baada ya siku chache akaanza kupigia simu wasichana wote aliokuta msg zao na kuwaambia vitu vya ajabu ajabu kwamba mimi nina wasichana wengi na mambo mengine machafu sana ambayo siwezi ongea.
Naona story inakua ndefu anyway sasahivi tunawasiliana vizuri ila kila siku napigiwa simu usiku wa manane nikiwa nimelala asubuhi nakutana na messege tuachane kweli nimechoka huu wivu wa hatari. Hebu jamani naombeni msaada huyu dada ananifaa au ndo ntaishia kuchomwa kisu maana ni mcha.....
Kiukweli bado nampenda lakini nakereka sana vitu vidogo anasema tuachane imezidi sana. Kutokana na umbali wa ninapoishi nimejikuta na uhusiano na msichana mwingine ambao si wa mapenzi na huyu dada anatambua kuwa nina msichana. Mwezi wa 7 nilikua nimepanga kumvisha pete huyu mpenzi wangu lakini kabla ya muda kufika akaja ghafla mkoa akakuta msg za yule rafiki yangu ikawa balaa akampigia simu yule dada akamwambia sisi ni marafiki tuu.
Hakutaka kuamini akachukua vitu vyake vyote akaondoka zake. Baada ya siku chache akaanza kupigia simu wasichana wote aliokuta msg zao na kuwaambia vitu vya ajabu ajabu kwamba mimi nina wasichana wengi na mambo mengine machafu sana ambayo siwezi ongea.
Naona story inakua ndefu anyway sasahivi tunawasiliana vizuri ila kila siku napigiwa simu usiku wa manane nikiwa nimelala asubuhi nakutana na messege tuachane kweli nimechoka huu wivu wa hatari. Hebu jamani naombeni msaada huyu dada ananifaa au ndo ntaishia kuchomwa kisu maana ni mcha.....