Yaliyotokana na Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema

Regia Mtema

R I P
Nov 21, 2009
2,970
864
Wakuu nimeona nivema nikawapa majina ya kamati kuu mpya ya CHADEMA ili wale wasioifahamu basi waifahamu.

1.Freeman Aikael Mbowe -Mwenyekiti
2.Said Amour Arfi (MB)- M/Mwenyekiti Bara
3.Said Issa Mohamed- M/mwenyekiti Zanzibar
4.Dr Wilbrod Peter Slaa- Katibu Mkuu
5. Zitto Zuberi Kabwe- Naibu Katibu Mkuu Bara
6.Hamad Mussa Yusuph-Naibu Katibu Mkuu Zanzibar
6. Edwin Mtei- Mwenyekiti Mstaafu
7.Bob N Makani- Mwenyekiti Mstaafu
8.Philemon Ndessamburo(MB)
9.Mhonga Said Ruhanywa (MB)
10.Shaban Mambo-Mwenyekiti Umoja wa Madiwani
11.Lazaro Massai-Mwenyekiti wa Halmashauri Karatu
12.Philip Shelembi
13.Susan Lyimo(MB)
14.Mwanamrisho Abama-Zanzibar
15.Prof Mwesiga Baregu
16.Dk Kitilla Mkumbo
17.Nassor Ally Salim -Zanzibar
18.Regia Estelatus Mtema- Mjumbe mdogo kuliko wote kwa kuchaguliwa
19.Shida Salum Bitaliho
20.Leticia G Mosore-Mwenyekiti -Baraza la Wanawake CHADEMA(BAWACHA)
21.Susan H Kiwanga
22.Grace Kiwelu(MB)
23.Paul Herman Sule- Katibu wa Umoja wa Madiwani
24.Charles Mwera(MB) na Mwenyekiti wa Halmashauri Tarime
25.Nyangaki Silungushela- Mwenyekiti Baraza la Wazee CHADEMA
26.John Mnyika-Mkurugenzi
27.John Mrema-Mkurugenzi
28.Benson Kigaila-Mkurugenzi
29.Msafiri Mtemelwa-Mkurugenzi
30.Victor P Kimesera-Mkurugenzi

N.B
Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA
1.Viongozi sita wa mwanzo wanaingia kwa kofia zao
2.Wenyeviti wastaafu wanaingia kwa kofia zao
3.Wenyeviti wa halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA wanaingia kwa kofia zao
4.Mwenyekiti na Katibu wa Umoja wa Madiwani wanaingia kwa kofia zao
5.Wawakilishi watano wa wabunge-wanajichagua miongoni mwa wabunge
6.Wenyeviti wa Mabaraza ya chama yaani Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA),Baraza la wazee na Baraza la Wanawake
7.Wakurugenzi wanaingia kwa kofia zao lakini ni wajumbe wasio na kura.
8.Waliobaki kwa upande wa wanaume waligombea kupitia baraza kuu-hizi ni nafasi tatu tu Bara na moja Zanzibar
9.Waliobaki kwa upande wa wanawake waligombea kupitia baraza kuu-nazo ni nafasi tatu tu Bara na moja ni Zanzibar-Kati ya hao watatu wawili ni watu wenye ulemavu yaani Regia Mtema na Shida Salum
 
Muundo wa hiyo kamati kuu itafikiri unasoma kamati ya CCM.

Kwanini vyama vya upinzani viige muundo ule ule wa CCM? Ningetegemea hii kamati ingelikuwa na watu wachache sana ambao ndio wangelikuwa vichwa wa CHADEMA.

Mafanikio mema kamati kuu mpya ya CHADEMA.
 
Asante, good composition, inapunguza kidogo ile dhana ya Uchagga Chadema, ila I'm not comfortable kwa Kichwa Wilfred Lwakatare kuachwa nje just as ordinary member, wakati kwenye timu yao ni vichwa kadhaa na makapi kibao!.
 
Nimeleta taarifa hizi kwa kuwa ndio habari nilizonazo na chama pekee kilichoifanya uchaguzi hivi karibuni.

Ni Habari njema sana .Nangojea kusikia wale wanaosema kwamba Chadema ni kampuni mali ya wachaga . Sasa kamati kuu ni hiyo hebu tuanze sasa .
 
Asante, good composition, inapunguza kidogo ile dhana ya Uchagga Chadema, ila I'm not comfortable kwa Kichwa Wilfred Lwakatare kuachwa nje just as ordinary member, wakati kwenye timu yao ni vichwa kadhaa na makapi kibao!.

Pasco
Moja Asante kwa maoni mazuri. Kama nilivyoeleza kwenye thread yangu kwamba kuna walioingia kwa kofia zao na kuna waliogombea,Mpaka sasa sijafahamu kama Lwakatare ananafasi yeyote ndani ya CHADEMA itakayomfanya aingie kwa kofia yake kwani hakugombea kwenye uchaguzi uliopita labda alihofia kuwa mgeni ndani ya CHADEMA hivyo kama angegombea ingeleta picha mbaya kisiasa kwake na kwa chama. Pili naomba unifafanulie hapo nilipoweka RED sijakupata.
 
wakuu nimeona nivema nikawapa majina ya kamati kuu mpya ya chadema ili wale wasioifahamu basi waifahamu.

1.freeman aikael mbowe -mwenyekiti
2.said amour arfi (mb)- m/mwenyekiti bara
3.said issa mohamed- m/mwenyekiti zanzibar
4.dr wilbrod peter slaa- katibu mkuu
5. Zitto zuberi kabwe- naibu katibu mkuu bara
6.hamad mussa yusuph-naibu katibu mkuu zanzibar
6. Edwin mtei- mwenyekiti mstaafu
7.bob n makani- mwenyekiti mstaafu
8.philemon ndessamburo(mb)
9.mhonga said ruhanywa (mb)
10.shaban mambo-mwenyekiti umoja wa madiwani
11.lazaro massai-mwenyekiti wa halmashauri karatu
12.philip shelembi
13.susan lyimo(mb)
14.mwanamrisho abama-zanzibar
15.prof mwesiga baregu
16.dk kitilla mkumbo
17.nassor ally salim -zanzibar
18.regia estelatus mtema- mjumbe mdogo kuliko wote kwa kuchaguliwa
19.shida salum bitaliho
20.leticia g mosore-mwenyekiti -baraza la wanawake chadema(bawacha)
21.susan h kiwanga
22.grace kiwelu(mb)
23.paul herman sule- katibu wa umoja wa madiwani
24.charles mwera(mb) na mwenyekiti wa halmashauri tarime
25.nyangaki silungushela- mwenyekiti baraza la wazee chadema
26.john mnyika-mkurugenzi
27.john mrema-mkurugenzi
28.benson kigaila-mkurugenzi
29.msafiri mtemelwa-mkurugenzi
30.victor p kimesera-mkurugenzi

wote ni wachagga hao!!! Du si wanasemaga... Wote wachagga!!...propaganda bwana is another thing...!
 
Wakuu nimeona nivema nikawapa majina ya kamati kuu mpya ya CHADEMA ili wale wasioifahamu basi waifahamu.


3.Said Issa Mohamed- M/mwenyekiti Zanzibar

6.Hamad Mussa Yusuph-Naibu Katibu Mkuu Zanzibar

14.Mwanamrisho Abama-Zanzibar

17.Nassor Ally Salim -Zanzibar

N.B
Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA

8.Waliobaki kwa upande wa wanaume waligombea kupitia baraza kuu-hizi ni nafasi tatu tu Bara na moja Zanzibar
9.Waliobaki kwa upande wa wanawake waligombea kupitia baraza kuu-nazo ni nafasi tatu tu Bara na moja ni Zanzibar-Kati ya hao watatu wawili ni watu wenye ulemavu yaani Regia Mtema na Shida Salum

Nini nafasi ya Chadema Zanzibar?
 
Kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA
1.Viongozi sita wa mwanzo wanaingia kwa kofia zao
2.Wenyeviti wastaafu wanaingia kwa kofia zao
3.Wenyeviti wa halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA wanaingia kwa kofia zao
4.Mwenyekiti na Katibu wa Umoja wa Madiwani wanaingia kwa kofia zao
5.Wawakilishi watano wa wabunge-wanajichagua miongoni mwa wabunge
6.Wenyeviti wa Mabaraza ya chama yaani Baraza la Vijana CHADEMA(BAVICHA),Baraza la wazee na Baraza la Wanawake
7.Wakurugenzi wanaingia kwa kofia zao lakini ni wajumbe wasio na kura.
8.Waliobaki kwa upande wa wanaume waligombea kupitia baraza kuu-hizi ni nafasi tatu tu Bara na moja Zanzibar
9.Waliobaki kwa upande wa wanawake waligombea kupitia baraza kuu-nazo ni nafasi tatu tu Bara na moja ni Zanzibar-Kati ya hao watatu wawili ni watu wenye ulemavu yaani Regia Mtema na Shida Salum

Hicho kipengele cha wenyeviti wa halmashauri kinahitaji mabadiliko. Tanzania tuna Halmashauri zaidi ya 100, suppose CHADEMA wakishinda kwenye halmashauri 10 tu kati ya hizo zote, je, wote wataingia kwenye Kamati Kuu kwa kofia zao?

Kufanya mabadiliko baada ya kuona kuna wenyeviti wengi hiyo ndiyo huwa inapelekea kusabisha migogoro kwenye chama kwa kuwa njia ya kuwapata representatives wa hao wenyeviti inaweza "kuonekana inawapendelea" watu/mtu fulani na kuwaonea wengine. Ni vyema mabadiliko hayo yakafanyika mapema ili kuondoa hiyo notion.
 
Hicho kipengele cha wenyeviti wa halmashauri kinahitaji mabadiliko. Tanzania tuna Halmashauri zaidi ya 100, suppose CHADEMA wakishinda kwenye halmashauri 10 tu kati ya hizo zote, je, wote wataingia kwenye Kamati Kuu kwa kofia zao?

Kufanya mabadiliko baada ya kuona kuna wenyeviti wengi hiyo ndiyo huwa inapelekea kusabisha migogoro kwenye chama kwa kuwa njia ya kuwapata representatives wa hao wenyeviti inaweza "kuonekana inawapendelea" watu/mtu fulani na kuwaonea wengine. Ni vyema mabadiliko hayo yakafanyika mapema ili kuondoa hiyo notion.

Samahani labda sikufafanua vizuri.Ni hivi katika kipengele cha wenyeviti wa halmashauri....Inasomeka hivi Wawakilishi watano wa Madiwani,wawili wakiwa ni madiwani wa kawaida na watatu wawe ni wenyeviti wa halmshauri zinazoongozwa na CHADEMA.Wajumbe hawa watachaguliwa na Umoja wa Madiwani wa CHADEMA....Nadhani nimeeleweka vizuri...
 
Chadema ina watu potential wengi, ila mwambieni Mtei akae kimya, Bob makani katulia na ukimya wake unaheshima, akina Baregu poa ila hawezi kujibu mswali magumu!.Kitila naye aache kuwa biased wote wanatakiwa kuwa neutral kabisa , hata kama wana lao it is better to keep silent to let party moving.
 
Samahani wakuu nina swali. Kamati kuu ina members thelathini. Je hao wote wana lipwa mshahara na chama? Je members ambao wana vyeo vingine kama ubunge na wao wana mshahara wa kamati kuu?
 
Chadema ina watu potential wengi, ila mwambieni Mtei akae kimya, Bob makani katulia na ukimya wake unaheshima, akina Baregu poa ila hawezi kujibu mswali magumu!.Kitila naye aache kuwa biased wote wanatakiwa kuwa neutral kabisa , hata kama wana lao it is better to keep silent to let party moving.

Kwanini wawe hivyo kwani hawana haki?kwanini Mtei awe kimya?Sio kweli kwamba Prof Baregu hawezi kujibu maswali magumu...anyway huo ni mtazamo wako.....Sidhani kama kuna mwanaharakati au mwanasiasa yeyote anayeweza kuwa neutral labda awe anafanya unafiki,kwa vyovyote vile atakuwa na upande tu...Any way Kitilla ni mwezetu humu JF naomba nisimsemee....Ataeleza mwenyewe.
 
Chadema ina watu potential wengi, ila mwambieni Mtei akae kimya, Bob makani katulia na ukimya wake unaheshima, akina Baregu poa ila hawezi kujibu mswali magumu!.Kitila naye aache kuwa biased wote wanatakiwa kuwa neutral kabisa , hata kama wana lao it is better to keep silent to let party moving.

Yaani wakae kimya au neutral kwa sababu waberoya amesema au kwa sababu ni kiongozi mmoja tu anayetakiwa kuongea chadema (zitto wa dowans)?
 
Samahani wakuu nina swali. Kamati kuu ina members thelathini. Je hao wote wana lipwa mshahara na chama? Je members ambao wana vyeo vingine kama ubunge na wao wana mshahara wa kamati kuu?

MwanaFalsa1

CHADEMA hailipi mishahara viongozi wake mishahara.Si wajumbe wa Kamati Kuu,si Baraza Kuu wala si Mkutano Mkuu isipokuwa hulipwa posho ndogo sana za vikao kwaajili ya kujikimu na nauli. Wabunge na Viongozi Wakuu wale wa Bara hawalipwi hata hizo posho za vikao kwa kuwa wameamua kujitolea ingawa ni haki yao kupata. CHADEMA ni chama chenye mapato kidogo hivyo hakina budi kupunguza matumzi yasiyo ya lazima..Viongozi wote wa CHADEMA katika ngazi zote hakuna anyelipwa mshahara kwa sasa isipokuwa watendaji wa Makao Makuu tu.ndio wanapata posho kidogo za kujikimu kwa mwezi.
 
Back
Top Bottom