Yaliyonipata Muhimbili baada ya kifo cha mwanangu siku ya tar03.03.2012!!!!!

Shame on us tunaotetea madaktari na shame on us tunaotetea serikali!!! Wamekosea wote kwa pamoja!!!!
 
Pole sana mkuu.
Nashangazwa na jambo moja: mtoto alipofariki ilipaswa kujazwa fomu na certification ya daktari kuthibitisha kweli amefariki. Ilikuwaje ubebe maiti ya mwanao mikononi kupeleka mortuary? Ina maana oksijen dr alijitahidi kumuwekea wakati umempakata?

Pili, elewa kuwa hata kikao cha madaktari hakikufanyikia hapo muhimbili.

Pole sana, wewe na sisi tuna mengi ya kujifunza katika hili.
 
pole sana mkuu kwa hali uliyokutana nayo .. naamini ulijitahidi sana kupigania hali ya mtoto , ila naamini pia sisiwazazi tusiwe tunaridhika sana na matibabu ya dispensary za mtaani kwani ni wengi wanayakuta huko na wanapokuja kugundua na kuhitaji msaada zaidi wanakuwa wamechelewa.. jipe moyo kuwa mvumilivu kubali hali halisi
 
kwa sasa naweza kusema tu, POLE SANA MUNGU AKUTIE NGUVU tupo pamoja.
 
Pole sana mkuu kwa yote yaliyowakuta
ila wakulaumiwa hapa ni hii serikali yetu pamoja na viongozi wake-maana hawataki kusikiliza madai ya wafanyakazi wake ilhali wanajua outcome inakuwaje-kama madaktar wangesolviwa matatizo yao-hali isingekuwa hivyo mkuu.
 
Pole sana mkuu. Muhudumu wa Mochuari alikua anapiga dili gani hasiwepo ofisini kwa masaa 2? Utaratibu wa kuhifadhi mwili ulifuatwa kweli? Kwasababu ilikua ni kazi ya manesi/wahudumu kupeleka mwili mochuari. Kwa mara nyingine pole kwa kumpoteza mtoto wenu kipenzi Mariam
 
pole sana ,mkuu ila umefika wakati tufanye kitu kwajili ya nchi yetu kwni tunaomia ni watu wa chini mkuu,kama wanJF naomab tufanye jambo jamani....,tukoe wenzetu
 
Pole sana mkuu. Muhudumu wa Mochuari alikua anapiga dili gani hasiwepo ofisini kwa masaa 2? Utaratibu wa kuhifadhi mwili ulifuatwa kweli? Kwasababu ilikua ni kazi ya manesi/wahudumu kupeleka mwili mochuari. Kwa mara nyingine pole kwa kumpoteza mtoto wenu kipenzi Mariam
Kwa mara nyingine naomba niwape ufafanuzi kuhusu yaliyomsibu maana mm binafsi jana nilienda kwake,
Ni kwamba baada ya kua mtoto amefariki alipewa document ya kwenda kupeleka maiti mochwari,na aliibeba mwenyewe mikononi baada ya kuona kuna arufu ya rushwa,baada ya kufika mochwari na kukuta muhusika hayupo alimsubili kwa masaa2,alipokuja alimjibu ya kua alikua anakusanya maiti hodini,kuhusu kikao cha madaktari ni kweli kiliisha mapema,but kiliendelea tena baadae nje ya kikao!!
So hiyo ndio nchi yetu,binafsi nimeziona picha alizojipiga mwenyewe nje ya mochwari,kwa mwenye kutaka kuziona aende kwake maeneo ya banana,au ntawapa namba zake za simu maana kanipa jana na humu kaziweka pia.
 
pole sana ,mkuu ila umefika wakati tufanye kitu kwajili ya nchi yetu kwni tunaomia ni watu wa chini mkuu,kama wanJF naomab tufanye jambo jamani....,tukoe wenzetu

Toa wazo mkuu ili tulifanyie kazi!!!
 
Pole mkuu!
Personally najipa moyo one day tutapata suluhisho la yote haya!
RIP Mariam
....Njowepo hapo kwenye one day yes ndipo panapotuharibia watz....anyway inaniuma sana kuona tuna viongozi walipoteza muelekeo na kubaki kulia lia na kusikitika badala ya kuchukua hatua. Hivi kwa nini watanzania tusifanye kweli kwenye sanduku la kura 2015??? Huu utumbo wa CCM unaoendelea kuzamisha nchi lazima ufike mwisho jamani....Pole kwa yote Spika. This is time for CHANGES!!
 
pole sana jaman, hii yote ni coz ya uongozi mbovu. hao madaktari wangesikilizwa yote yacngetokea kbs, wananchi wanakufa viongozi wamekaa kimya wao wanaenda kutibiwa India. Maskin anakosa matibabu na kuambulia kifo. Inauma sana tena sana. jaman tunaamani coz waTanzania 2wavumilivu mno tena sana, vinginevyo swala la madaktari km wameshndwa kulitatua ingetakiwa serikali yote ijivue gamba. Inauma sanaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa tena sana............! POLE KWA KUMPOTEZA MWANAO.
 
Ndg zangu wana JF nadhani niliwapa taarifa juu ya kifo cha mwanangu mpendwa "MARIAM ALLY"aliyefariki siku ya j,mosi usiku.
Mwanangu alikua na umri wa miezi 9 hv,alianza kuugua malaria siku ya tar 29.02,usiku,tukampeleka dispensary alfajiri ya tar 1.3 na akapata vipimo na kuandikiwa doz ya malaria bcoz alikua na malaria "2".

Aliendelea na doz mpaka siku ya tar 3 asubuhi nilipogundua kama anaupungufu wa maji mwilini,tukamrudisha dispensary ile ile kwa ajiri ya kumcheki tena,baada ya kumcheki dk alisema amepungukiwa maji kwahiyo anatakiwa kupewa drip,alitundikiwa drip kuanzia majira ya saa 5 asubuhi,ilipofika majira ya saa 12 jioni dr akatupa rufaa kwenda muhimbili, nilikodi tax na tukafika muhimbili ndani ya muda muafaka,nilipokelewa na dr1 hv bwana mdogo na alijaribu kunisaidia ili tumuwaishe kwenye oxsijen lakini ilishindikana maana madaktari walikua na kikao cha kupanga mgomo mpya.

So mwanangu akawa amefariki kwenye mikono ya mamake,nilishukuru mungu kwa yote, sasa nikaanza utaratibu wa kutoa maiti kuipeleka mochwari,ilituchukua kama dk 40 hv kupewa kibali cha kuipeleka mochwari,still bado haikua problem sana kwangu.

Sasa kilichonikera na kunisikitisha ni baada ya kufika mochwari sikumkuta muhusika wa mochwari na sasa ikanibidi kuzunguka kumtafuta muhusika huku nikiwa nimeibeba maiti ya mwanangu mikononi,punde alifika ndg yangu mmoja niliyekua nimempigia simu aje kunichukua na gari yake bcoz wife tayari alikua ameshachanganyikiwa,so ilibidi mimi nikae kwenye mrango wa mochwari kwa takribani masaa hv ili kumsubili muhusika na ndg yangu huyo pia akaanza kumtafuta na kumpata baada ya masaa 2 hivi.

Baadae niligundua kwamba madaktari walikua bado wanaendelea na kikao cha mgomo uliopangwa kuanza j5 nchi nzima,
Sasa ni swali kwa wana JF, Jee kama hayo yanatokea muhimbili jee sisi tusio na uwezo wa kwenda INDIA tutapona kweli???

Naombeni comments.

Ili tuende sawa na hao wakuu wa nchi wakiomba rufaa ya kwenda kutibiwa nje wawabanie, japo najua haitasaidia maana watakimbilia hospitali za private ambazo naamini haitasaidia
 
Mkuu pole sina la kusema hapa. Muachie mungu ila inasikitisha sana, maliza msiba urudi suala hili lijadiliwe kwa mapana.
 
pole sana mzee,kwa ujumla inaonekana ulichelewa muda mwingi pale dispensary,ilitakiwa umuwahishe moja kwa moja muhimbili maana inaonekana alikua katika hali mbaya sana
Sidhani kwamba ni busara kulaumu maamuzi yaliyofanywa na mfiwa. Hakuna mzazi anayechelewesha kumpatia mtoto wake tiba..
 
Back
Top Bottom