Yaliyonikuta Leo

Haha!! Mbona hii tayari ilishaigizwa na ze comedi? Next time nafikiri akishakukomalia umpeleke hospitali unampakia kwenye gari halafu unampeleka polisi. Ilimradi unauhakika kwamba amejigongesha mwenyewe na hajaumia. Mimi ilinitokea Tandika, jamaa akajigongesha kwenye side mirror na akajifanya ameanguka. Halafu jamaa wengine wakaanza kuja mbele ya gari ili kunizuia nisiondoke, nilichofanya ni kukanyaga mafuta wenyewe wakanipisha barabarani.

Itabidi nianze kuangalia ze comedi sasa , sikuwa nimeiona!
 
Nikiwa naendesha kariakoo kaja mwanaume wa makamo hivi namuona makusudi anajigongesha kwenye kioo
cha gari cha pembeni.

Mie nikasimama mara anadai nimpeleke hospital kaumia nikamwambia umeumia wapi na gari haikuwa kasi sanasana umegusa kioo .
Kashupaa nimpeleke hospital au nimpe pesa akatibiwe.

Nikampa 10,000.00 ili yaishe bwana wee nimeenda kupaki nazunguka kariakoo na kutana naye anadunda swafi kabisa!

Jamani hali ya uchumi hii itatupeleka pabaya mtu mzima kama yeye nimesikitika sana.
so ukiwa kariakoo uwe mwangalifu sana.
Watu wanabuni njia mbalimbali za kujipatia pesa kiurahisi.
Pole mie nilikutana na maswahiba kama hayo yako Pale Magomeni Karibu na Nyumbani Kwa Marehemu Sheikh Yahaya,bahati kuna mdada mmoja anamjua huyu mzee alikuwa amevaa kanzu,akajigongesha Akawa analalamika mgu wake wenye chuma nimeivunja tena wakati sikumgonga na ata speed ya gari langu ilikuwa kama 20 KMm kwa saa.

Yule dada akinipa signal kuwa nnatapeliwa,so nilimwambia ngoja nipaki gari vizuri upande twende hospital then nikaweka speed nikatokomea.

Pole sana
 
Pole sana kwa mkasa huo, maisha yamekuwa magumu sana ndio maana watu wanatafuta namna ya kuishi..
 
Sipati picha ungeamua kukomaa hadi hospitali halafu ijulikane hajaumia. Ila jamani kariakoo, kweli twende kwa uangalifu, kuna watu ndiyo kazi yao hiyo, pole sana Nata
 
jamani sijui hali hii tutaendelea nayo mpaka lini. Unaweza ukamwona kuwa alikuwa jeuri, lakini ukitafakari, ni heri afanye hivyo ili aine siku pamoja na wenzake ingawa inaumiza wasiohusika. Mungu atusaidie
 
ulimuuliza nini baada ya kumkuta? au ulikaa kimya kama ni hivyo nyie ndio mnaofuga maradhi.

Ndugu yangu we, nilikaa kimya kama nimemwagiwa maji na kumpita kama cjawahi muona
 
Nikiwa naendesha kariakoo kaja mwanaume wa makamo hivi namuona makusudi anajigongesha kwenye kioo
cha gari cha pembeni.

Mie nikasimama mara anadai nimpeleke hospital kaumia nikamwambia umeumia wapi na gari haikuwa kasi sanasana umegusa kioo .
Kashupaa nimpeleke hospital au nimpe pesa akatibiwe.

Nikampa 10,000.00 ili yaishe bwana wee nimeenda kupaki nazunguka kariakoo na kutana naye anadunda swafi kabisa!

Jamani hali ya uchumi hii itatupeleka pabaya mtu mzima kama yeye nimesikitika sana.
so ukiwa kariakoo uwe mwangalifu sana.
Watu wanabuni njia mbalimbali za kujipatia pesa kiurahisi.
Siku nyingine ikitokea hivyo usikubali kumpa chochote paki gari lako pembeni ita Trafiki mweleze kilichotokea, kama kuna kesi ya kujibu mahakama ndiyo nitakayofafanua kosa lako na ikitoea kuna haja ya kumpeleka Hospitalini wewe kama mwenye gari huwajibiki kumtibia majeruhi, vinginevyo hiyo insurance yako itakuwa haina kazi kwenye gari.

Hao madapeli dawa yao ni hiyo maana ukilegea hapa mjini utaonewa kila kukicha.
 
Back
Top Bottom