Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,834
- 155,782
KHARTOUM, Sudan
MWANAMUME mmoja raia wa hapa ameripotiwa kumrushia kiatu Rais Omar al Bashir akiwa kwenye mkutano katika jengo moja lililopo mjini hapa.
Walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa hata hivyo Rais al-Bashir alinusurika na askari wa usalama walimkamata mrusha kiatu huyo na kumtia mbaroni ingawa maofisa kutoka ofisi ya Rais al Bashir walikanusha madai ya kiongozi huyo kurushiwa kiatu na badala yake walidai kuwa mhalifu huyo alizuiwa alipokuwa akijaribu kumkaribia Rais huyo.
Mmoja wa mashuhuda hao ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa tukio hilo lilotokea jana kwenye ukumbi wa Friendship uliopo mjini hapa ambako kiongozi huyo alikuwa akizungumza na wageni wake.
Chanzo hicho kimesema baada ya mtuhumiwa kurusha kiatu hicho wanausalama walimkamata na haikufahamika wazi chanzo cha mwanamume huyo kumrushia kiatu Rais huyo.
Rais Bashir alianza kuitawala Sudan tangu alipotwaa madaraka katika mapinduzi ya kijeshi mwaka 1989 na anatarajiwa kusimama katika kinyanganyiro cha uchaguzi mkuu wa Aprili mwaka huu Sudan itakapokuwa ikifanya uchaguzi wake mkuu wa kwanza baada ya miaka 24.
Tukio kama hilo lilitokea Desemba 2008 wakati mwandishi wa habari nchini Irak, Muntazer al-Zaidi, alimrushia kiatu aliyekuwa Rais wa Marekani, George Bush, alipokuwa ziarani mjini Baghdad.
MWANAMUME mmoja raia wa hapa ameripotiwa kumrushia kiatu Rais Omar al Bashir akiwa kwenye mkutano katika jengo moja lililopo mjini hapa.
Walioshuhudia tukio hilo wamesema kuwa hata hivyo Rais al-Bashir alinusurika na askari wa usalama walimkamata mrusha kiatu huyo na kumtia mbaroni ingawa maofisa kutoka ofisi ya Rais al Bashir walikanusha madai ya kiongozi huyo kurushiwa kiatu na badala yake walidai kuwa mhalifu huyo alizuiwa alipokuwa akijaribu kumkaribia Rais huyo.
Mmoja wa mashuhuda hao ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa tukio hilo lilotokea jana kwenye ukumbi wa Friendship uliopo mjini hapa ambako kiongozi huyo alikuwa akizungumza na wageni wake.
Chanzo hicho kimesema baada ya mtuhumiwa kurusha kiatu hicho wanausalama walimkamata na haikufahamika wazi chanzo cha mwanamume huyo kumrushia kiatu Rais huyo.
Rais Bashir alianza kuitawala Sudan tangu alipotwaa madaraka katika mapinduzi ya kijeshi mwaka 1989 na anatarajiwa kusimama katika kinyanganyiro cha uchaguzi mkuu wa Aprili mwaka huu Sudan itakapokuwa ikifanya uchaguzi wake mkuu wa kwanza baada ya miaka 24.
Tukio kama hilo lilitokea Desemba 2008 wakati mwandishi wa habari nchini Irak, Muntazer al-Zaidi, alimrushia kiatu aliyekuwa Rais wa Marekani, George Bush, alipokuwa ziarani mjini Baghdad.