Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,385
Si umeanzisha thread unasema upo Mbagala saizi tena upo Kilwa Road.
Tusubiri mkuu kina Wasira wanaweza kutoa sera nzuri leo za maendeleo ya Mtanzania.
Sheria zetu za Usalama barabarani zinasemaje kuhusu magari ya mizigo kubeba abiria??
Tusubiri mkuu kina Wasira wanaweza kutoa sera nzuri leo za maendeleo ya Mtanzania.
Mkuu Chadema wakichukuwa nchi tutakuwa tunakula mara ngapi kwa siku?
Nani kasema ? ww huijui dar hii, cdm siku ya mkutano wao watu kibao waliletwa na malori
Sheria zetu za Usalama barabarani zinasemaje kuhusu magari ya mizigo kubeba abiria??
Nasubiri kwa hamu hicho watakachokisema kuhusu UAMSHO...!By peter tumaini
Wanabodi,
kwa sasa nimeshawasili hapa jangwani kuangalia kinachojiri,pilikapilika za upangaji wa viti vya plastic vyeupe unaendelea na uandaaji wa jukwaa umepamba moto huku mabango nayo yakiandikwa.
Mpaka sasa kuna bango kubwa la kitambaa limewekwa junction ya Morogoro road na kawawa limeandikwa;"KUHUSU VURUGU ZA UAMSHO CCM KUTOA TAMKO LEO SAA SITA''
Ugawaji wa T-shirt unaendelea hapa Jangwani na mambo mengine mtapata jinsi time inavyojiri.
Natumia laptop ndogo nimeificha kiaina staweza kutupia picha.
wassira? Labda sera za maendeleo ya jamii yake aliyoitoroka gombe,lakini kwa mtanzania sahau
Ushabiki wa kipumbavu,kwa vile baba yako anapata kidogo kupitia chama lenu hili unadhani na wenzio tukutaneLeo mtasema mengi sana sana, ila kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji. Mpaka sasa CCM 3-CDM 0, na hapo mkutano haujaisha, mpaka ukiisha ni TWELVE NIL
CHAMA CHA MAPINDUZI TAARIFA KWA VYOMBO VYA HAHARI:
Tarehe 9/6/2012:
Wote mnatambua kuwa leo ni mkutano wetu pale Jangwani,
Napenda nichukue fursa hii kuwaeleza mambo muhimu, ya kufanya na yaliyojitokeza jana!
Wenzetu wa chama cha makonda wa mkoa wa dar es salaam wameamua kuwazuia wanachama wetu kutopanda magari yao wakiwa na sare za chama tawala, hili si jambo jema na tunalilaani vikali!
Ninawasihi CHACHAMUDA waache kutafuta ugomvi na serikali, kuwazuia kupanda daladala watu waccm ni kinyume cha sheria za nchi
Baada ya hapo tumeamua kuweka utarati wa wanachama wetu kufika mkutanoni ambapo tutawapa usafiri!
Maroli ya kubeba wanaccm yapo tayari:
kimara, Ukonga, Kigamboni,Mbagala,Tegeta, na kwingneko,
Chama kinahela hivyo kukodi watu sio dhambi tunawapa usafiri wa kuja na kurudi sisi tunarudisha hela kwa wananchi, wakati wenzetu chadema wao wananyang'anya wananchi masikini hela zao,
Tuna siri nzito za wapinzani, tutazimwaga hapa zote, tutadili na upinzani tu maana uhakika wa kuendelea kushika dola upo!
CCM ni taasisi kubwa haimtegemei mtu wala kikundi, hatutamfukuza mtu, ila shughuli iliyo ndani ya chama ndio itakayomkimbiza mtu.
TWangapi waliopita ccm na bado chama kipo? Kuondoka kwa mtu mmoja hakutakiangusha chama, aliondoka baba wa taifa na chama bado kipo.
Chama kikishindwa uchaguzi wa 2015 mimi nipelekwe jela kwa kifungo cha maisha bila kuisumbua mahakama, yani nitoke lumumba moja kwa moja Segerea
Mwisho nawaomba wote mtakaokosa usafiri pandeni daladala njoo jangwani, chakula na vinywaji vitakuwepo bila kusahau bendi yenu ipo!
Nape M. Nnauye
Tupunguze ukali wa maneno tunachotaka ni habari za mkutano wa magamba na kama atatokea mtu akatuwekea picha itakuwa bora zaidi.
Ni asubuhi tulivu ya Jumamosi na hali ya hewa ni nzuri kabisa.
CCM wanatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara katika viwanja vya Jangwani ambavyo wapinzani wao wakuu walivibatiza kwa jina la viwanja vya CDM SQUARE.
Tayari shamrashamra zimeshaanza hapa uwanjani na shughuli za ujenzi na kupamba majukwaa zinaendelea.Mkutano huu utarushwa live na vituo kadhaa vya Television.
Tutakuwa hapa uwanjani kuwapa updates kila kitakachoendelea.