hospitali zote hakuna huduma kuanzia jana saasita usiku subirini vyombo vyenu vinavyolipwa na ccm vifunike funike baadae
mungu tunusuru na hili janga katika wakati huu mgumu kwa mtanzania wa hali ya chini. Kwa sababu wao wakiumwa wanakimbia india mungu. Nakushtakia mungu ili uwape wanachostahili hawa mafedhuli. Amina.
Hali sio nzuri mkuu. Halafu cha kushangaza mpaka sasa hv hakuna taarifa yoyote kutoka kwenye vyombo vya habari. TBC ndio Kwanzaa wameweka tamthilia. Hawa jamaa wanatusukuma pabaya.jamani tujuzane, ile haki ya mgomo wakati ule ilikuwa mbaya sana, kweli mkuu wa kaya anatupeleka peleka tu, this life tutajikuta tunakufuru
Daa!watanzania wenzetu wanapokufa nani muuaji ktk hii vita jamani?
Kweli hizi ni siku za mwisho maana ilitabiriwa kuwa Siku za mwisho watu watakuwa ni wenye kupenda fedha, wenye kujipenda wenyewe. Yaani kweli madaktari wanagoma ili kuomba nyongeza tu ya mshahara ili hali watu wanakufa!!! Ajabu na kweli.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
Kama mmeamua kugoma gomeni siyo mnatishiwa nyau mnarudi kazini ni heri kieleweke.
Subiri matusi ila huo ndio ukweli,wabunge wanajiongezea posho na nyinyi mnagoma muongezewe posho kwangu mlalahoi wote greedy tu...maslahi binafsi mbele,mnaacha watu wanakufa kisa mmekosa nyongeza ya posho,mkiongezewa mtarudisha uhai wa waliopoteza maisha?ndio taaluma yenu inavyowafundish?mnagoma ili iweje acheni kazi kabisa!mnagoma ili mpewe mshahra bila kazi?