Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Mwanakijiji,
There will never be a perfect party. But I believe it is much easier to influence and bring change within a young CHADEMA than it is within the colossus CCM.
 
Mi nadhani tumuulize Mwanakijiji anamaanisha nini haswa anaposema "Tukishaiong'oa ccm then what?"Kikawaida,chama kinachoshinda uchaguzi ndicho kinachopewa baraka za kuunda serikali na kuongoza taifa kwa mujibu wa sera na itikadi zako walizozinadi kwa wananchi.
MKJJ ni wazi anafahamu vyema,na tumekuwa tukimpa mifano mingi tu hata ya kuhusu kumg'oa mkoloni,nduli nk.
Mwanakijiji swali kwako una maanisha nini unapouliza whats next?What exactly do you mean?Swali lako linaweza kuwa pana sana,je una maanisha mafisadi wafachukuliwe hatua gani nk?Ama unazungumzia mgawanyo wa madaraka?
Weka wazi coz lugha yetu sometimes tunaweza tukapiga kambi kwenye issue moja kisa utafsiri mbovu.
 
In fact nimekuwa najitahidi sana kuumiza kichwa kufikiria ni nini hasa MKJJ anachokitaka kutokana na maswali yake anayouliza lakini mara zote huwa sipati jibu. Anapouliza upinzani unataka kuitoa CCM halafu ufanye nini anamaanisha kitu gani hasa, ina maana hajui?, jamani nisaidieni labda mimi ni mvivu wa kufikiri.

Ninavyojua kila chama kina itikadi yake, kina strategies zake, kina sera zake, kina ilani yake, kwa hiyo usitegemee maswali yako MKJJ yaje na jibu moja tu kama 2 + 2=4 kokote uendako duniani jibu ni lile lile. Kwa sababu majibu ya maswali yako ni very comprehensive yanahusisha sera, strategies nk ni pamphlet nzima kwa hiyo usitegemee mtu akujibu kwa sentensi moja tu au kwa kutuma post moja humu JF.

Labda nikuulize MKJJ wewe binafisi unataka nini kifanyike, naomba usijibu kwa kuuliza tena maswali ambayo umekuwa ukituuliza ya 'tuungane halafu tufanye nini','baada ya kuitoa CCM then nini', 'halafu kiwe nini', hapana. Ukijibu swali langu hilo moja labda nitakuwa na uwezo wa kuyajibu maswali yako. Otherwise utakuwa unatuchezea mchezo wa tiari bado huku ukituangalia tunakoenda kujificha.
 
Kwa upande mwingine chadema nao wawe makini wasije wakawa kama NCCR mageuzi ya wakati ule ambapo ilisambaratika baada ya uchaguzi. all in all tunawatakia kila lakheri katika michakato yao angalau wapunguze vijembe na majivuno ya CCM ambayo yanatulaza njaa kila siku.

Ebwana signature yako imeniacha hoi, yaani ni ukweli mtupu!! Sijui lini tutabadilika...
 
Mwanakiji

Kuindoa CCM madarakani na Kuongeza idadi ya wabunge ndicho hasa knatakiwa kufanyika. Naweza Kumpa kura Yangu ya Urais Lowasa au Rostam aziz akigombea kwa ticket ya upinzani lakini Siwezi kumpa Mwakenyembe wala Salim Ahmed salim kura yangu ya uarais wakigombea kwa CCM.

Tena kabla ya kuitoa CCM madarakani naamini kuongeza idadi ya wabunge ndo inatakiwa iwe PRIORITY. hili la idadi ya wabunge wa upinzani hata wakiwa ni wale waliokuwa CCM ndilo itakuwa mteremko wa kuindoa CCM.
 
Mwanakijiji, naomba nikutoe woga kuwa Tanzania bila CCM yawezekana kabisa ingawa najua wengi tu mpo wenye woga huu unaotumiwa sana na CCM kama mtaji wa kuvuna wapiga kura. Ni woga unaochangiwa na kusukumwa zaidi na uelewa finyu miongoni mwa jamii kwani yaonekana sasa tunaanza kuuchukulia utawala chini ya CCM kama utamaduni wetu na hivyo kuwa na woga tunapofikiria maisha nje ya CCM. Ukweli ni kuwa tulipofikia chini ya CCM kwa sasa hivi tumegota na mabadiliko yoyote yatakayoweza kutukwamua haiwezekani tena yakaletwa na CCM hiyo hiyo kwa mbinu na sera hizo hizo. Mwanakijiji, kwa mambo mengi tu umeonyesha msimamo usioyumba lakini hapa umenishtua - naona unaanza kuwa na cold feet au ndio umeshughulikiwa kimya kimya ! Tungechukua muda huu kutoa wito vyama vingine vilivyobaki viunge mkono Chadema tuiweke CCM benchi - hivyo swali lako la CCM itolewe ili iwe nini limenitisha kidogo.
 
Kwa kadiri ya kwamba lengo ni kutaka tu kuwang'oa CCM madarakani halafu ndiyo mfikirie mtafanya nini kwa taifa na kutuambia basi mtaendelea kuwa wasindikizaji kama ilivyokuwa kuanzia 1995 hadi sasa na itakavyokuwa milele na milele.

Bila ya shaka, lakini tushikamane kwenye kitu gani? bado naambiwa "kuing'oa CCM madarakani"; nauliza ili kiwe nini? jibu "ili itoke madarakani", nauliza halafu kifuate nini? naambiwa "hilo si la msingi kwa sasa kujua, tukishawatoa madarakani ndiyo tutawaambia"! Well.. mshikamano wa namna ndugu zangu nyie shikamaneni na ng'anganianeni kabisa na mgandane kama yule sungura alivyojagandishwa kwenye sanamu akidhania anaikomoa kule shambani.

Hebu mkuu tueleze kwa lugha nyepesi ya kueleweka.Okay,kama tukiafikiana nawe kuwa ufumbuzi sio kuing'oa CCM,je nini kifanyike ili tusiwe wasindikizaji?Napata shida sana kuelewa kipi hasa kifanyike kulingana na mtazamo wako.Na inaniwia vigumu zaidi kukuelewa kwa vile wewe,mie,na sote tunafahamu UTAMU WA MADARAKA,na hicho ndicho kinaifanya CCM ifanye kila hujuma dhidi ya vyama vingine kwa vile haitaki kutoka madarakani.Sasa kwa mwenendo huu wa CCM kung'ang'ania kuhodhi madaraka (mosi,kwa vile madaraka ni matamu.Napili,kwa vile mafisadi huko CCM wanajua fika kuwa usalama wao pekee ni kuendelea kuwepo madarakani la sivyo wataishia Keko au Segerea) itawezekanaje kwa fikra,sera,mawazo na njia mbadala kupata fursa ya kuleta mabadiliko ya kweli kwenye nchi yetu?

Please,kwa maneno mepesi kabisa tufahamishe NINI KIFANYIKE BADALA YA KUING'OA CCM MADARAKANI?Nauliza hivyo kwa sababu kupinga hoja pasipo kuwa na hoja mbadala hakuwezi kutufikisha popote.Kama unadhani KUNA UFUMBUZI MBADALA wa huu tuodhani wengi (kuwa CCM ing'oke kwanza) tuhabarishane basi.Angalau sie tunaoamini katika ufumbuzi wa kuing'oa CCM tuna ushahidi halisi kuwa dawa ya magugu shambani ni kuyang'oa (refer tulivyong'oa ukoloni na tulivyomng'oa Idi Amin).Sala labda na mwenzetu utupatie hiyo njia bora zaidi (ikiwezekana utupatie na mifano hai ya namna ilivyoleta ufanisi kwingineko).

Nahofia tunaweza kujikuta tunarejea enzi za ujamaa wa njozi: mawazo mazuri lakini impractical.Au kibaya zaidi,kuwa na wishful thinking ambazo zinawezekana tu kugeuka uhalisia kama sote tungekuwa malaika.

Busara ni kitu kizuri lakini hazina maana kama hazileti mazuri yanayokusudiwa.
 
Mzee Mwanakijiji,

Fikira ulizokuwa nazo pamoja na wana CCJ wenzako hazitakiwi kufa ama kufukiwa, zinatakiwa kudumu daima labda iko siku moja zitakuja kufanya kazi huko mbele ya safari ama zitakuwa borrowed na chama kingine cha ushindani ili zitumike kufanya kile ambacho CCJ ilidhamiria kukifanya.

Niliposoma mada yako, nimeona dalili za kukata tamaa na pia kutokuwa tayari kuunga mkono juhudi za wapinzani waliopo katika vita vya kuing'oa CCM madarakani. Mpaka dakika hii CCJ is done kwa kuwa viongozi wa muda wa kitaifa wameishahamia CHADEMA, so kwa maneno mengine hakuna uongozi tena CCJ. Lakini fikira za CCJ ambazo unaonekana unazo, bado zinahitajika ili kuikomboa Tanzania. Tuwekee hapa jamvini hizo fikira ili tuzichambue, may be baadhi ya vyama vya siasa vinaweza kuzichukua na kuzi-modify ili ziendane na sera zao na hivyo zikasaidia juhudi za ukombozi wa Tanzania.

Tumesubiri kwa muda mrefu kuona kile ambacho hakijawahi kufanywa na chama chochote cha kisiasa lakini nahisi wafuasi wengi tumekata tamaa baada ya kuona manahodha wake wakiamua kuachia jahazi na kupanda jahazi jingine. Binafsi ninaomba kujua, what is CCJ's next move baada ya viongozi wa muda wa kitaifa kuhamia CHADEMA. Je, bado kuna viongozi wengine ambao tulikuwa hatuwajui na hivyo watakuja ku-take over?

Kama bado kuna viongozi wa CCJ ambao hawajahama kambi, ninaomba wajiweke wazi ili tuendelee na matumaini yale yale kwamba mkombozi kaja kutupeleka nchi ya asali na maziwa. Bado tunasubiri kuona kile ambacho hakijawahi kufanywa na chama chochote cha siasa katika historia ya Tanzania kwenye mfumo wa vyama vingi.
 
Mwanakijiji,
Nakushauri usome kitabu cha Museveni "Sowing the Mustard Seed." Hakukubaliana na sera za Obote, kama ambavyo hukubaliani na (baadhi ya?) sera za CHADEMA. Lakini ilipokuja suala la kumwondoa Amin alishirikiana na wapiganaji wa Obote. Baada ya Amin kuondolewa alijitahidi kufanya kazi naye ingawa alijua kuwa Obote alikuwa na mapungufu kwa uongozi wa Uganda. Suala la what next baada ya kuiondoa CCM mamlakani linapaswa kujibiwa baada ya kuiondoa CCM, pamoja na ushirikiano wako. Hapo kama unaendelea kutofautiana na CHADEMA unayo haki, kama mwanamapinduzi mshirika, kuwakoromea CHADEMA kuwa mnakokwenda siko kule tunakotaka Tanzania ielekee. Huwezi kuwa na fursa hiyo under the present circumstances, that is a fact. So let us cross that brigde together and help shape what is on the other side of the bridge.
 
Hapa naoana kuna sintofahamu kati ya MM na wachangiaji wengine.MM anachosema kama nimemuelewa vizuri, ni kuwa lengo sio tu kuin'goa CCM bali fikra za kuibadilisha nchi kutoka udhalimu wa CCM akimaanisha sera. Ndiyo maana amesema CCM ikishang'oka then hao waliohamia au muungano wa CCJ na CHADEMA utaleta mabadiliko ya kweli kama hakuna fikra elekezi[sera] tangu awali!!!!!!! Hamaanishi CCM iking'oka what next kama wengi wanavyomuelewa.
Mtazamo wa pili ambao naunga mkono ni kuwa bora CCM ing'oke hata kama hakuna sera maana nchi ina viongozi wengi tu nje ya system wanaoweza kuunda na kusimamia sera na taratibu. Ninasema haya kwasababu CCM kwanza wamebana mabadiliko yawe ya katiba au kitu chochote kwasababu ya kulinda maslahi yao. Hawa wazee wa CC na NEC wakisambaritishwa tunaweza sema ni hatua moja muhimu. Hivi unadhani ni kwanini wanaweza kurithisha watoto wao uongozi, ni mfumo ambao kama upo nje you will never make it. Jiulize kwanini hawataki mgombea binafsi, ni kulinda maslahi yao. Jiulize kwanini hawataki katiba mpya ni kulinda wenzao waliopita na kufanya uchafu na wao kujijengea ulinzi wa baadaye.
Mimi nasema urais si hoja, wapinzani wakiwa na wabunge wakutosha mabadiliko yatatokea tu, lakini la muhimu si kuanza na fikra MM, hii ni emergence ondoa CCM ili uweze kuwa na mwanya. wazungu wanasema ''chase the fox to the bush then warn a hen to move around ''
Kenya wamefanikiwa kwasababu wamevunja mtandao wa KANU kwanza, halafu ndio makundi yenye fikra tofauti yamejitokeza.
Wananchi wasipovunja CCM EL na Rostam watakuwa Rais na PM!! 2015
Hivyo breakdown CCM for any cost first.
 
napenda kwanza kabisa kuungana na wenzangu kumpigia saluti ndugu yetu mwanakijiji kwa aliyoyafanya. Lakini hii haitoshi maana mimi si mwana CCM wa mawazo mgando wa zidumu fikra za mwenyekiti. Natangaza kabisa kutokukubaliana na mtazamo huu mpya wa mwanakijiji wakati nikikubaliana na wale wote wanaouliza swali la msingi la kumtaka ndugu yetu afumbue hilo fumbo kama lipo. Vile vile sikubali kwamba ubongo wangu umelala na kutaka kuamini kwamba kwa mara ya kwanza sielewi kinachosemwa. Kwanza kabisa nashindwa kuelewa ni kwa nini frustration za mwanakijiji za CCJ kushindwa ku live up to our expectations atake kuzimalizia CHADEMA. Nakubaliana kabisa na wanaosema huwezi kuwa chama cha siasa na ukawa na wazo la kwanza tofauti na lile la kuking'oa chama kilichoka madarakani katika kuiongoza serikali, hapa ndipo tunapomshangaa Lipumba anapong'ang'ania kuonekana anaelewana na CCM kwenye majukwaa. Lazima CHADEMA kibebe ilani ya kukitoa CCM madarakani hata kama kinajua kinahitaji nguvu za ziada kufanya hivyo. Ndio maana leo hii wengi tunakielewa. Pili labda mzee wetu utueleze unaposame 'kuunga mkono kwa sasa' are you mobilizing people agianst CHADEMA? kwa lengo na faida ya nani given the situation? Pili pia hutaki wakitaka kuingiza wabunge wengi bungeni, sasa unataka nini na iwapo wote tunajua na tumeona umuhimu wa kuwa na sauti katika bunge hata kama serikali ya CCM itaendelea kutosikiliza lakini walau wananchi na marafiki wa demokrasia watafanya hivyo. Je Mwanakijiji nae ni wale wale? mimi sitaki kuamini lakini sitaki pia kushindwa kujiuliza ninapoona dalili kama hizi. Mimi naamini njia pekee ya kusonga mbele ni kuendelea kukiunga mkono chama pekee kinachoonekana walau kimekuwa consistent katika kupigania agenda yake, hao CCJ bado ni concept tu nakama kuna viongozi wenye uwezo waliohamia CHADEMA basi hlo pia ni jambo la ushindi. Mimi naomba ndugu yangu MM usiwategemee sana hao wana CCM waliokwambia watahamia CHADEMA, hao kina Samuel Sitta sio wapiganaji nao pia ni viongozi maslahi. Mimi naona ni aheri kidogo chako kuliku kikubwa cha mwenzio. CHADEMA ndio tunayoijua kwa miaka kumi mizima iliyopita. CCJ hatujawahi hata kuiona wala hatujui kama kweli ni chama basi kama kuna mapungufu ya CHADEMA tuendelee kuwashauri, hatukotayari kuona wakina LYATONGA MREMA ama LAMWAI wengine waliojikita katikati ya engine wakatusambaratisha katika hatua hii ngumu na kali kabisa. NDIO TUNATAKA KUINGIZA WABUNGE IWEZEKANAVYO KATIKA BUNGE LIJALO, NDIO TUNATAKA KUIONDOA CCM MADARAKANI, mkakati wa kuongoza utapatikani kwani hawa CCM wanaotuongoza miaka nenda rudi bila hata dira wana uaheri gani kuliko hawa CHADEMA ambao walau wanapigia kelele miiko. Ndugu yangu Mwanakijiji hatuna tena muda wa 'what ifs' jibu tunalo, forward ever backward never, tusingependa kukuacha ugeuke jiwe,
 
Nadhani itabidi niende ndani zaidi kuelezea kile ninachokiita "Tatizo la Chadema". Natumaini nitaeleweka, na siyotkuwa nimechelewa. Niwatoe hofu kabisa kwangu mimi hata CCM ikiondolewa kesho madarakani sitolia!! Lakini sitorukaruka kwa furaha! Nitauliza swali hili hili ninaloliuliza sasa.. "then what"? Nakataa kabisa kuwa hatuwezi kuwa na ajenda ya uchaguzi inayosema "tuiondoe CCM kwanza"! Hii ni ajenda ya kuondoa chama kimoja na kukiweka kingine. Yatakuwa yale yale ya KANU na RAINBOW coalition! Well RAINBOW walifanikiwa kabisa kuiondoa KANU, lakini is Kenya better today than during KANU's rule? Tutapata majibu tofauti sana kwenye hilo. Je Zambia chini ya Chiluba baada ya kuiangusha ZANU je walikuwa bora zaidi kwa sababu kina Chiluba walitimiza ndoto yao ya kumuangusha Kaunda?


Hili swali hata kama mtalikwepa, mtalibeza au mtajaribu kuonesha kuwa hamlielewi mtalazimika kulijibu tu one of these days. I know you will.

Kwa vile linaonekana ni gumu mno/halielewi au halijaulizwa sawasawa itabidi nilivunje vunje katika vipande vyake vidogovidogo. CHADEMA WAKILIELEWA NA KULIJIBU KABLA YA UCHAGUZI WATASHINDA KWA KISHINDO!
 
Please,kwa maneno mepesi kabisa tufahamishe NINI KIFANYIKE BADALA YA KUING'OA CCM MADARAKANI?

Nadhani labda unafikiria namaanisha CCM ising'olewe madarakani. Mbali kutoka hilo. Ninachomaanisha ni kuwa CCM kuondolewa madarakani haliwezi kuwa lengo na ajenda ya uchaguzi kwa sababu kuondolewa kwa CCM kunakuwa ni matokeo ya kukubalika kwa sera, mipango, na ahadi za CHADEMA. Sera, mipango na ahadi hizo ni lazima ziweze kuwashawishi wananchi kuwa CCM ni mbaya na hafai; ni lazima ziwe bora na zinazowezekana kuliko zile za CCM. Nje ya hapo CCM haiwezi kuondolewa madarakani kwa kuunganisha chuki dhidi yake. Kwa sababu kama mnavyoona kuna watu wanaoipenda CCM kwa kiasi cha ajabu zaidi na wengine licha ya kujua ubovu wa CCM bado wanajipanga mstari na kuishangilia.

Hivyo, ni mambo gani Chadema inaahidi kuyafanya na kwa muda gani ambayo ni bora kuliko ya CCM ambayo yatafanya wananchi waikatae CCM na hivyo kuing'oa madarakani? Maana kama leo JK anasema atajenga Chuo Kikuu kingine, Hospitali, barabara na akaonesha "mafanikio" ya CCM Chadema wataonesha nini au kuahidi nini zaidi ya kile cha CCM?

Kwa mfano, mkisema ufisadi JK atasema wamepeleka watu kadhaa mahakamani, fedha za EPA zimerudishwa, watu wamefukuzwa kazi n.k Chadema itasema nini juu ya hilo ambalo ni bora kuliko hilo? Si tumeona wapinzani kama kina Mrema wakisifia juhudi hizo na hata baadhi ya wana Chadema wenyewe?
 
Kuindoa CCM madarakani na Kuongeza idadi ya wabunge ndicho hasa knatakiwa kufanyika.

Halafu mkishakuwa na wabunge wengi wamejazana huko Bungeni na wote wanasimama na kuimba kumbaya, and then what? Wabunge hao wengi wanatakiwa kufanya nini kwanza na kwanini? Au wakishajazana kama walivyojazana wale wa CCM leo hii ndio mwisho? Well.. I know.. "tutajua wakishajazana"!
 
Mkuu Nguruvi,

Naona wewe ndiyo hujamwelewa Mwanakijiji. Tatizo kubwa la kwanza la Mwanakijiji ni kwamba amesema hana imani na siasa ya ushirikiano wa wapinzani. Hoja yake ninaiunga mkono ukizingatia historia za ushirikiano wa wapinzani hapa kwetu. Mara nyingi umekuwa ni ushirikiano wa kisanii. Tatizo ni kwamba ikifika wakati wa uchaguzi ndio utasikia hoja za kushirikiana, na kila chama kinataka kusimamisha mgombea wake kila jimbo hata kama hakubaliki/hauziki kwa wapiga kura.

Wangekuwa na nia ya kweli ya kushirikiana wangekuwa wanaanza mjadala wa kushirikiana miaka 2 au 3 kabla ya uchaguzi ili kuepusha migogoro ya kusimamisha wagombea. Lazima kuwe na makubaliano ya namna ya kumpata mgombea strong wa kuwakilisha wapinzani wote walioamua kushirikiana. Hii ni pamoja na kuandaa sera ambazo zitatumiwa na muungano wa wapinzani kwenye kampeni. Ushirikiano wa kukurupuka pindi uchaguzi unapokaribia, sioni kama unaweza kuleta ushindi kwa wapinzani.

Mwanakijiji alikuwa anaamini kwamba CCJ ingekuwa a very strong party ambayo ingeweza kuing'oa CCM bila kushirikiana na wapinzani wengine. Kitendo cha viongozi wa muda kuhama kimeacha ombwe, na sasa wale wazito ambao tuliambiwa wako nyuma ya hao vijana hatutakuja kuwaona tena.

Ndugu yangu Mwanakijiji, kwenye politics lazima kuna ku-compromise mambo fulani fulani ili angalau wapiganaji wawe na common ground ambayo itawakusanya kwa ajili ya kupambana na adui aliye mbele. Huwezi kupata watu 1000 na wote wakawa wana mawazo na msimamo ulio sawa katika kila kitu. Ili watu hao waweze kuendelea kuwa pamoja ndipo kuna ku-compromise baadhi ya mambo. Mfano hai ni hilo tukio la jana, kama viongozi wa muda wa CCJ wangekuwa wana mawazo na msimamo kama wa kwako, nina uhakika kwamba hata baada ya CCJ kukosa usajiri wa kudumu, wangebaki ili wahakikishe wanakijenga chama na kukilea ili kikue na hatimaye kiweze kutwaa dola.

Tatizo la CCJ ni kwamba kama kuna big shots ambao walikuwa nyuma ya viongozi wa muda wa CCJ, basi hao vigogo ni ma-opportunists na sioni kama wana tofauti yeyote na mtu anayekomaa na CCM na huku akiona ni chama cha mafisadi ama kinalea ufisadi. "Vigogo" hao walitaka CCJ isajiriwe ili iwe soft landing iwapo CCM ingekata majina yao kwenye kura za maoni.

Ndiyo maana baada ya kukosa usajiri wa kudumu viongozi wa muda wa CCJ wamehamia Chadema kwa kuwa kazi waliyotumwa na vigogo haikukamilika. Kama kweli walikuwa na nia ya kuanzisha chama strong, why wakianzishe mwaka wa uchaguzi? Kama hiyo haitoshi, kwanini baada ya kunyimwa usajiri wa kudumu wameamua kukitelekeza chama?

Hayo maswali 2 yanaweza kutoa hint ya malengo ya CCJ na kwamba tulioshangilia na kufurahia uanzishwaji wa CCJ tumeachwa solemba na hatukujua agenda hasa za hao wapiganaji walionzisha CCJ kwa mbwembwe na kelele nyingi na kwamba wana support ya vigogo nyuma yao.

Politics za Tanzania wakati mwingine zinasikitisha sana, maana unaweza ukahisi kwamba sasa huyu ndio mkombozi tuliyekuwa tunamsubiri na ukaja kukuta ni kikundi kingine cha opportunists ambao wanataka kutumia migongo ya wakesha hoi ili waendelee kujineemesha.
 
Nadhani itabidi niende ndani zaidi kuelezea kile ninachokiita "Tatizo la Chadema". Natumaini nitaeleweka, na siyotkuwa nimechelewa. Niwatoe hofu kabisa kwangu mimi hata CCM ikiondolewa kesho madarakani sitolia!! Lakini sitorukaruka kwa furaha! Nitauliza swali hili hili ninaloliuliza sasa.. "then what"? Nakataa kabisa kuwa hatuwezi kuwa na ajenda ya uchaguzi inayosema "tuiondoe CCM kwanza"! Hii ni ajenda ya kuondoa chama kimoja na kukiweka kingine. Yatakuwa yale yale ya KANU na RAINBOW coalition! Well RAINBOW walifanikiwa kabisa kuiondoa KANU, lakini is Kenya better today than during KANU's rule? Tutapata majibu tofauti sana kwenye hilo. Je Zambia chini ya Chiluba baada ya kuiangusha ZANU je walikuwa bora zaidi kwa sababu kina Chiluba walitimiza ndoto yao ya kumuangusha Kaunda?


Hili swali hata kama mtalikwepa, mtalibeza au mtajaribu kuonesha kuwa hamlielewi mtalazimika kulijibu tu one of these days. I know you will.

Kwa vile linaonekana ni gumu mno/halielewi au halijaulizwa sawasawa itabidi nilivunje vunje katika vipande vyake vidogovidogo. CHADEMA WAKILIELEWA NA KULIJIBU KABLA YA UCHAGUZI WATASHINDA KWA KISHINDO!

Mkuu MM,

Ndio maana tumekuwa tuna-advocate kuondoa vikwazo na mizizi waliyojiwekea CCM..............wengine bado hatuelewi.........kaazi kubwa sana ipo mbele yetu.............trust me............kusema chagua chama mbadala pekee haitoshi..........kuna mambo zaidi tunatakiwa kufanya.............hapa hapa JF tukianza hiyo mijadala ambayo inatishia uwepo wa CCM utawaona vijana wa MAJAMBAZI CCM wanavyokuja juu..............halafu sisi wenyewe hapa JF tunawaunga mkono...................mwananchi wa kawaida anayeisikia JF tunam-contradict........na mapambano yetu ya kifikra............................. tunaosema tunataka mabadiliko bado tuko gizani....................my point is......we are screwing ourselves............

We are very poor in finishing up stuffs.................hata World Cup 2010 timu zetu zimedhihirisha hilo............
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu bado unakwepa swali uloulizwa wewe. Unataka Chadema wafanye nini?.. maanake yaonyesha wewe unauliza swali ukiwa na jibu tayari kichwani. Chadema wameeleza itikadi yao sera zao ilani zao bado kitu gani haswa ambacho wewe kinakukwaza? Je hukubaliani na itikadi zao kama ndivyo nakumbuka ulishindwa kutueleza kule ktk mada iliyopita kuhusiana na sera za Chadema wapi unapingana nao pamoja na kwamba niliposoma sera za CCJ walichotofautiana zaidi ni kimaandishi tu.

Pili sidhani kama hao CCJ wengine waliojiunga na Chadema ni wajinga kiasi hicho, hawakutazama mapungufu uloyaona, wao wakaenda kukaa na viongozi wa Chadema wakjayaweza wazi maswala yao hadi imefikia wao kujiunga.Huu ndio ustraabu lakini kuja hapa JF ukaendelea kuuliza kitu ambacho hakieleweki ati Then What?
Kisha umetoa mfano wa KANU na Coalition, sijui kama unajua kwamba hata hiyo Kanu yenyewe ilikuwa coalition ya vyama vitatu kama tunavyoizungumza CCM leo hii. Kanu ilitokana na vyama vitatu - chama cha Jomo Kenyatta - KAU,Tom Mboya - NPCP na Oginga Odinga -KIM hawa ndio waliungana pamoja ku form KANU na kama unakumbuka vizuri..CCM pia haina tofauti toka TANU hadi CCM yenyewe ni coalition zilizowezesha umoja wa jumuiya zetu kutokana na WATU na MAZINGIRA tulokuwa nayo.

Huwezi kutumia mifano ya US ya kiitikadi kujenga UMOJA katika nchi ambayo wewe mwenyewe unakubali hakuna haki. Nitarudia kusema tazama South ANC na PAC hawa wote walikuwa na itikadi tofauti lakini ilipofikia swala la kumwondoa mkoloni na Apartheid that became priority number one..Tazama Zimbabwe, Zambia yenyewe wakati wa Kaunda mbinu zilizotumika ni sawa na hizi tunazotangaza hapa leo hii..

Mkuu wangu huwezi kuvuta umati wa kiafrika kwa kutumia itikadi isipokuwa kwa kumwondoa adui aliyepo madarakani na zipo nchi nyingi sana zimefanikiwa ikiwa unataka kutumia mifano kama hii.. South Afrika chini ya Mandela ni mfano mmoja mkubwa sana wa mafanikio ambao dunia nzima wanawapongeza hivyo hata hao Yankees walijiunga state hadi state kupambana na ukoloni wa Malkia wasijue itikadi gani wataitumia kutawala lakini baada ya kumwondoa Malkia ndipo fikra za itikadi zinakuja...

What next? haina mwisho mkuu wangu na kwahakika naweza kujibu kuwa -Tutahakikisha Mafisadi wanafikishwa mbele ya sheria na ukaendelea kuuliza what next?.. nikajibu Tutarudisha uhuru na haki mikononi mwa wananchi - what next? hivyo hivyo tukajaza kurasa na kurasa za maswali ya kufikirika kuandika hadithi ndefu kwa mkono wa Binadamu..

It's ONLY God knows mambo ya What next itazaa kitu gani, sisi tunapanga tunayoyaweza leo kulingana na mazingira tuliyopo. Hatuwezi panda mbegu zetu kwenye jiwe tukitegemea mavuno bora wala hatuwezi panda mahindi tukitegemea kuvuna mpunga sisi hatuko huko kabisa...isipokuwa tunachozungumza hapa ni kupata kwanza hati milki ya ardhi ambayo itatumika kwa kilimo. Kilimo ambacho kila mmoja wetu anakubali kwamba ndio uti wa mgongo wa uchumi wetu hayo ya kulima mpunga, mahindi au chochote unachofikiria wewe yatajulikana mbele ya meza kuu baada ya kupata haki miliki ya ardhi..

Hizo then what - tutalima kinachoweza kustawi - then what, then what - then what.. yoote itakuwa ktk historia ya nchi kama vile historia ya maisha yako ulitaka kuja Marekani -then what? - umefika US - then what?. haya maswali ya aina hii hatutamaliza leo wala kesho..
Leo hii hatuna hata kiwanja mkuu wangu unataka tufikirie kujenga maghorofa!
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu bado unakwepa swali uloulizwa wewe. Unataka Chadema wafanye nini?.. maanake yaonyesha wewe unauliza swali ukiwa na jibu tayari kichwani. Chadema wameeleza itikadi yao sera zao ilani zao bado kitu gani haswa ambacho wewe kinakukwaza? Je hukubaliani na itikadi zao kama ndivyo nakumbuka ulishindwa kutueleza kule ktk mada iliyopita kuhusiana na sera za Chadema wapi unapingana nao pamoja na kwamba niliposoma sera za CCJ walichotofautiana zaidi ni kimaandishi tu.

Pili sidhani kama hao CCJ wengine waliojiunga na Chadema ni wajinga kiasi hicho, hawakutazama mapungufu uloyaona, wao wakaenda kukaa na viongozi wa Chadema wakjayaweza wazi maswala yao hadi imefikia wao kujiunga.Huu ndio ustraabu lakini kuja hapa JF ukaendelea kuuliza kitu ambacho hakieleweki ati Then What?
Kisha umetoa mfano wa KANU na Coalition, sijui kama unajua kwamba hata hiyo Kanu yenyewe ilikuwa coalition ya vyama vitatu kama tunavyoizungumza CCM leo hii. Kanu ilitokana na vyama vitatu - chama cha Jomo Kenyatta - KAU,Tom Mboya - NPCP na Oginga Odinga -KIM hawa ndio waliungana pamoja ku form KANU na kama unakumbuka vizuri..CCM pia haina tofauti toka TANU hadi CCM yenyewe ni coalition zilizowezesha umoja wa jumuiya zetu kutokana na WATU na MAZINGIRA tulokuwa nayo.

Huwezi kutumia mifano ya US ya kiitikadi kujenga UMOJA katika nchi ambayo wewe mwenyewe unakubali hakuna haki. Nitarudia kusema tazama South ANC na PAC hawa wote walikuwa na itikadi tofauti lakini ilipofikia swala la kumwondoa mkoloni na Apartheid that became priority number one..Tazama Zimbabwe, Zambia yenyewe wakati wa Kaunda mbinu zilizotumika ni sawa na hizi tunazotangaza hapa leo hii..

Mkuu wangu huwezi kuvuta umati wa kiafrika kwa kutumia itikadi isipokuwa kwa kumwondoa adui aliyepo madarakani na zipo nchi nyingi sana zimefanikiwa ikiwa unataka kutumia mifano kama hii.. South Afrika chini ya Mandela ni mfano mmoja mkubwa sana wa mafanikio ambao dunia nzima wanawapongeza hivyo hata hao Yankees walijiunga state hadi state kupambana na ukoloni wa Malkia wasijue itikadi gani wataitumia kutawala lakini baada ya kumwondoa Malkia ndipo fikra za itikadi zinakuja...

What next? haina mwisho mkuu wangu na kwahakika naweza kujibu kuwa -Tutahakikisha Mafisadi wanafikishwa mbele ya sheria na ukaendelea kuuliza what next?.. nikajibu Tutarudisha uhuru na haki mikononi mwa wananchi - what next? hivyo hivyo tukajaza kurasa na kurasa za maswali ya kufikirika kuandika hadithi ndefu kwa mkono wa Binadamu..

It's ONLY God knows mambo ya What next itazaa kitu gani, sisi tunapanga tunayoyaweza leo kulingana na mazingira tuliyopo. Hatuwezi panda mbegu zetu kwenye jiwe tukitegemea mavuno bora wala hatuwezi panda mahindi tukitegemea kuvuna mpunga sisi hatuko huko kabisa...isipokuwa tunachozungumza hapa ni kupata kwanza hati milki ya ardhi ambayo itatumika kwa kilimo. Kilimo ambacho kila mmoja wetu anakubali kwamba ndio uti wa mgongo wa uchumi wetu hayo ya kulima mpunga, mahindi au chochote unachofikiria wewe yatajulikana mbele ya meza kuu baada ya kupata haki miliki ya ardhi..

Hizo then what - tutalima kinachoweza kustawi - then what, then what - then what.. yoote itakuwa ktk historia ya nchi kama vile historia ya maisha yako ulitaka kuja Marekani -then what? - umefika US - then what?. haya maswali kweli tutafika!.
Leo hii hatuna hata kiwanja mkuu wangu unataka tufikirie kujenga maghorofa!

well, nyinyi endeleeni kulikwepa swali la "then what" na mimi nitaendelea kuliuliza. Kwa sababu naamini mabadiliko tunayoyataka lazima yajaribu kujibu swali hilo. Kwa upande wa Chadema wafanye nini well, sidhani kama wako tayari kusikia. So, nyinyi endeleeni kuwatia shime wasijaribu kujibu swali hili na mimi nitaendelea kuwauliza. Hata kama siyo popular kuuliza swali hilo ambalo si gumu kama wengi wanavyotaka liwe.
 
well, nyinyi endeleeni kulikwepa swali la "then what" na mimi nitaendelea kuliuliza. Kwa sababu naamini mabadiliko tunayoyataka lazima yajaribu kujibu swali hilo. Kwa upande wa Chadema wafanye nini well, sidhani kama wako tayari kusikia. So, nyinyi endeleeni kuwatia shime wasijaribu kujibu swali hili na mimi nitaendelea kuwauliza. Hata kama siyo popular kuuliza swali hilo ambalo si gumu kama wengi wanavyotaka liwe.
Tunakuuliza wewe utajibu vipi?.. au wataka hao Chadema wakujibu vipi.. frankly kama mimi ni kiongozi wa Chadema sintakuwa na jibu, ikiwa wewe hukupata jibu toka ktk katiba,sera, na ilani za chama - sijui unategemea jibu litoke wapi kujibu swali lisilojulikana..
 
Tunakuuliza wewe utajibu vipi?.. au wataka hao Chadema wakujibu vipi.. frankly kama mimi ni kiongozi wa Chadema sintakuwa na jibu, ikiwa wewe hukupata jibu toka ktk katiba,sera, na ilani za chama - sijui unategemea jibu litoke wapi kujibu swali lisilojulikana..

ni kweli ndiyo ninaitta "TATIZO LA CHADEMA"!
 
Back
Top Bottom