Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,789
Kwenye hatua za makuzi ya mwanadamu kuna hatua mbalimbali hupitia kuanzia kutungwa kwa mimba mpaka kifo;
Utotoni
Ujanani
Utu uzima na
Hatimaye uzeeni
Kila hatua hapa huwa na mambo yake ambayo kwa afya ya akili ni lazima mtu apitie, utotoni kuna mambo ya kitoto lazima mtoto ayafanye na hapa ndio penye mzizi mkuu.
Ujanani lazima kuna mambo kijana ayafanye asipoyafanya kwenye hatua hiyo atakuja kuyafanya uzeeni.
Utu uzima- hii ni hatua ambayo haiachani sana na uzee na madhara mengi huonekana hapa. Yani kama kuna mambo hukuyafanya utotoni au ujanani hapa lazima yaombe reverse.
Tunakutana na watu kwenye mizunguko yetu makazini na hata mitandaoni, mambo wanayofanya ni tofauti kabisa na umri wao yanaitwa mambo ya kitoto.
Hatupaswi kuwalaumu bali ni kuwaacha tu hicho kipindi kipite kwakuwa kwasababu zozote zile hawakupitia na hapa kwa sehemu wazazi au walezi wanahusika ukali uliozidi, ama kuwatenga watoto na jamii ama kina Joni kisomo nk.
Kibaya na cha kutia simanzi ni pale mtoto mdogo anapokuwa na mambo ya kikubwa hii si kuruka hatua bali kulazimishwa na malezi au jamii.
Hebu jichunguze hivi hujaruka hatua kweli kwenye makuzi yako? Usinijibu ifanye kuwa siri yako.