Kuruka hatua (stage) kwenye makuzi

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,789
1469557192610.jpg


Kwenye hatua za makuzi ya mwanadamu kuna hatua mbalimbali hupitia kuanzia kutungwa kwa mimba mpaka kifo;

Utotoni
Ujanani
Utu uzima na
Hatimaye uzeeni

Kila hatua hapa huwa na mambo yake ambayo kwa afya ya akili ni lazima mtu apitie, utotoni kuna mambo ya kitoto lazima mtoto ayafanye na hapa ndio penye mzizi mkuu.

Ujanani lazima kuna mambo kijana ayafanye asipoyafanya kwenye hatua hiyo atakuja kuyafanya uzeeni.

Utu uzima- hii ni hatua ambayo haiachani sana na uzee na madhara mengi huonekana hapa. Yani kama kuna mambo hukuyafanya utotoni au ujanani hapa lazima yaombe reverse.

Tunakutana na watu kwenye mizunguko yetu makazini na hata mitandaoni, mambo wanayofanya ni tofauti kabisa na umri wao yanaitwa mambo ya kitoto.

Hatupaswi kuwalaumu bali ni kuwaacha tu hicho kipindi kipite kwakuwa kwasababu zozote zile hawakupitia na hapa kwa sehemu wazazi au walezi wanahusika ukali uliozidi, ama kuwatenga watoto na jamii ama kina Joni kisomo nk.

Kibaya na cha kutia simanzi ni pale mtoto mdogo anapokuwa na mambo ya kikubwa hii si kuruka hatua bali kulazimishwa na malezi au jamii.

Hebu jichunguze hivi hujaruka hatua kweli kwenye makuzi yako? Usinijibu ifanye kuwa siri yako.
 
Ni kweli mshana, kitaani kwetu kuna mzee wa makamo ila mambo anayoyafanya hayaendani na umri wake wakati mwingine unawezamkuta hata kavaa mlege na naskia watu wakisema huenda huyu mzee ujana wake hakuutumia ipasavyo
alifungiwa ama kuchungwa sana
 
Watu huwa wananiambia kuwa nimeruka stage cz wakat nasoma nilikua sina muda wa kwenda club na kufanya mambo ambayo wadada wengine wanafanya.

Lakin niliwaambia hakuna kuruka stage na wala hakitanirudia hata mara moja labda Mungu wangu aliye hai awe amekufa kwa muda huo

Nipo nadundika tu na nipo young kuliko wao ingawa umri umeenda

Ukiwaona wao sasa kama wazeee; et walikua ktk stage; sio kila kitu wanachopitia inabid upitie cz vingine ni hatari

Marafiki wanaweza kukufanya ukapitia vitu sivyo kabisa et usiruke stage kwenye ndoa utakua utarudia maliza vyote.

Inategemea na stage ipi.

Mm sitegemei kurudia stage mbovu nasonga mbele tu
 
Watu huwa wananiambia kuwa nimeruka stage cz wakat nasoma nilikua sina muda wa kwenda club na kufanya mambo ambayo wadada wengine wanafanya.

Lakin niliwaambia hakuna kuruka stage na wala hakitanirudia hata mara moja labda Mungu wangu aliye hai awe amekufa kwa muda huo

Nipo nadundika tu na nipo young kuliko wao ingawa umri umeenda

Ukiwaona wao sasa kama wazeee; et walikua ktk stage; sio kila kitu wanachopitia inabid upitie cz vingine ni hatari

Marafiki wanaweza kukufanya ukapitia vitu sivyo kabisa et usiruke stage kwenye ndoa utakua utarudia maliza vyote.

Inategemea na stage ipi.

Mm sitegemei kurudia stage mbovu nasonga mbele tu
Aaaamen nakuaminia my sister
 
Ni kweli mshana, kitaani kwetu kuna mzee wa makamo ila mambo anayoyafanya hayaendani na umri wake wakati mwingine unawezamkuta hata kavaa mlege na naskia watu wakisema huenda huyu mzee ujana wake hakuutumia ipasavyo
Yaani katika Umri huo anapiga mlege??Kama ndio hivyo hatoweza kuwapiga marufuku watoto/wajukuu zake akikuta nawenyewe pia wanavaa legesha:D:D
 
Watu huwa wananiambia kuwa nimeruka stage cz wakat nasoma nilikua sina muda wa kwenda club na kufanya mambo ambayo wadada wengine wanafanya.

Lakin niliwaambia hakuna kuruka stage na wala hakitanirudia hata mara moja labda Mungu wangu aliye hai awe amekufa kwa muda huo

Nipo nadundika tu na nipo young kuliko wao ingawa umri umeenda

Ukiwaona wao sasa kama wazeee; et walikua ktk stage; sio kila kitu wanachopitia inabid upitie cz vingine ni hatari

Marafiki wanaweza kukufanya ukapitia vitu sivyo kabisa et usiruke stage kwenye ndoa utakua utarudia maliza vyote.

Inategemea na stage ipi.

Mm sitegemei kurudia stage mbovu nasonga mbele tu
Hahaha sijakusahau my dear. Hivi kutokwenda club ni kuruka stage kumbe?
 
View attachment 371539kwenye hatua za makuzi ya mwanadamu kuna hatua mbalimbali hupitia kuanzia kutungwa kwa mimba mpaka kifo
Utotoni
Ujanani
Utu uzima na
Hatimaye uzeeni
Kila hatua hapa huwa na mambo yake ambayo kwa afya ya akili ni lazima mtu apitie
Utotoni kuna mambo ya kitoto lazima mtoto ayafanye na hapa ndio penye mzizi mkuu
Ujanani lazima kuna mambo kijana ayafanye asipoyafanya kwenye hatua hiyo atakuja kuyafanya uzeeni
Utu uzima- hii ni hatua ambayo haiachani sana na uzee na madhara mengi huonekana hapa...! Yani kama kuna mambo hukuyafanya utotoni au ujanani hapa lazima yaombe reverse
Tunakutana na watu kwenye mizunguko yetu makazini na hata mitandaoni, mambo wanayofanya ni tofauti kabisa na umri wao...yanaitwa mambo ya kitoto
Hatupaswi kuwalaumu bali ni kuwaacha tu hicho kipindi kipite kwakuwa kwasababu zozote zile hawakupitia ...na hapa kwa sehemu wazazi au walezi wanahusika
Ukali uliozidi, ama kuwatenga watoto na jamii ama kina joni kisomo nk nk..!
Kibaya na cha kutia simanzi ni pale mtoto mdogo anapokuwa na mambo ya kikubwa hii si kuruka hatua bali kulazimishwa na malezi au jamii
Hebu jichunguze hivi hujaruka hatua kweli kwenye makuzi yako?usinijibu ifanye kuwa siri yako
Mimi nipo makini sana...kila sekunde naitumia ipasavyo utadhani natembea na script mkononi....wale waliopandishwa yellow bus na kushinda na mabeki tatu ndio hao wanaotuletea usumbufu ukubwani.
 
Hahaha sijakusahau my dear. Hivi kutokwenda club ni kuruka stage kumbe?
Mwezangu mm hostel nilikua naonekana mshamba nahiv nilikua nakaa nje

Bas watu wote wanaondoka nabak mm tu au wawil hostel nzima.

Yaan utasikia watu hufany haya mambo sa hz ukiwa kwako utarudia tu;
Na hao wanaume utakua nao ukiolewa utachepuka.

Bas mm nawaangalia natafuta kitanda nilale

Sasa cjaona tofaut kat yangu na yao zaid tu kuwa wamechakaaa nw kumbe ni kujichosha tu

Nikajisemea bora niwe mshamba kuliko kuruka ruka sa hz
 
Kuna jamaa yng mmoja alikua na mambo yakitoto ad michezo na watt ujinga ujinga kuja kuchunguza kumbe aliugua sana utotoni kuna stage aliruka "
 
Mwezangu mm hostel nilikua naonekana mshamba nahiv nilikua nakaa nje

Bas watu wote wanaondoka nabak mm tu au wawil hostel nzima.

Yaan utasikia watu hufany haya mambo sa hz ukiwa kwako utarudia tu;
Na hao wanaume utakua nao ukiolewa utachepuka.

Bas mm nawaangalia natafuta kitanda nilale

Sasa cjaona tofaut kat yangu na yao zaid tu kuwa wamechakaaa nw kumbe ni kujichosha tu

Nikajisemea bora niwe mshamba kuliko kuruka ruka sa hz
Mmh Mungu atusaidie na hawa marafiki. Sema hakuna kitu kizuri kama kujitambua wewe ni nani na unataka nini, basi hutoyumbishwa
 
Lakini hapa kuna kitu kimoja lazima kieleweke kwamba hatua zote za makuzi zinapoisha, huwa na tabia kujirudia tena! Ndio maana wazee wengi huwa, hupenda ama hufanya mambo ya kitoto kabisa
Hii haijalishi kama aliruka stage ama la uzeeni mambo huanza upya katika hatua ile ya utotoni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom