everybody
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 337
- 103
Kwa wale wanasheria embu tupeni ufafanuzi na vigezo gani vinaangaliwa katika kutoa hukumu. Nimesoma kwenye habari leo kwamba meya wa zamani wa Rwanda aliyehusika kwenye Mauaji ya Kimbari ya Rwanda amehukumiwa na mahakama huko Arusha kwenda jela miaka 15. Halafu nimesoma kwenye gazeti hilo hilo la Tarehe: 17th November 2011 kwamba "MAHAKAMA ya Wilaya Ruangwa mkoani Lindi, imemhukumu Hamisi Nassoro (31) kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kuchoma moto nyumba" na kadiri ya habari yenyewe inaonekana hakuna mtu aliyepoteza maisha kwenye kuchoma nyumba huko. Anayestahili kupata kifungo cha maisha si huyo aliyeshiriki kwenye mauaji ya maelfu ya watu huko Rwanda???!!!! Hii imekaaje jamani kwa wale wanasheria?