ya zanzibar ni haki kuamuliwa na wabara

Godwine

JF-Expert Member
Jan 15, 2010
1,371
281
Je ni vema watu wa bara kuhusika moja kwa moja kuchagua mgombea wa urais wa zanzibar kama CCM wanavyofanya? au wawaachie wenyewe mahamuzi yote?
 
Je ni vema watu wa bara kuhusika moja kwa moja kuchagua mgombea wa urais wa zanzibar kama CCM wanavyofanya? au wawaachie wenyewe mahamuzi yote?

Mkuu Godwine, jambo hilo limekaa kiutaratibu wa chama zaidi na kamati zake.
 
Mkuu Godwine, jambo hilo limekaa kiutaratibu wa chama zaidi na kamati zake.
lakini mkuu sasa huoni ni wakati wa kukuza demokrasia ndani na nje ya vyama kwa mfano rais aliyepita alikuwa anakubalika kwa asilimia 30 tuu ya wajumbe wa zanzibar lakini huku bara ndio tukalazimisha wazanzibar awe mgombea wao hatuoni tunawanyang'anya uhuru wao, au tunafanya znz kama kamkoa ka kisiasa?
 
Kama sehemu ya muungano zanzibar inapaswa kuwashirikisha Watanzania (wote) kwenye suala la kumpata kiongozi wake, otherwise wanaweza kujisahau wakamchagua mtu mwnye negative effect kwa muungano...
 
Kama sehemu ya muungano zanzibar inapaswa kuwashirikisha Watanzania (wote) kwenye suala la kumpata kiongozi wake, otherwise wanaweza kujisahau wakamchagua mtu mwnye negative effect kwa muungano...

Yup..Zenji inATUMIKA tu na bara kwa maslahi ya kisiasa(remotely controlled)!...Ndio maana hata Muungano unang'ang'aniwa zaidi na watu wa Bara wakati wazenji hawana mpango nao!...Ni ushenzi wa toka zamani ambapo hata mikataba ya Muungano haijulikani iko wapi, na hata ridhaa yenyewe ya Muungano haikutafutwa!
 
Lakini Wazenj wenyewe si wanapenda kutawaliwa!, baada ya kujikombowa kutoka mkoloni wa kiarabu, sasa wacha watawaliwe na MKOLONI TANGANYIKA. Muungano utakuwa huu! Endeleleni kuwatia utumwani, wenyewe si wanashindwa kujitawala na Ujinga wao huo. physsx ghrrrrh!..
 
Yup..Zenji inATUMIKA tu na bara kwa maslahi ya kisiasa(remotely controlled)!...Ndio maana hata Muungano unang'ang'aniwa zaidi na watu wa Bara wakati wazenji hawana mpango nao!...Ni ushenzi wa toka zamani ambapo hata mikataba ya Muungano haijulikani iko wapi, na hata ridhaa yenyewe ya Muungano haikutafutwa!

Sisi watu wa bara kwa kweli hatuwatendei haki wenzetu wa visiwana hasa pale inapotokea wao wanampenda mtu wao halafu sie kwa sababu tunazozijua sisi tunamkataa na kuwachagulia mtu tunaedhani anawafaa!!Hii imetokea mara kadhaa; na hakuna sababu za msingi zinazothibitisha kuwa maamuzi hayo huwa ya busara.Kitu kinachonishangaza mimi ni kwanini wazanzibari wamekuwa wanakubali hali hii ya kuchaguliwa viongozi na wabara iendelee? Wazanzibari ni watu jasiri sana kuliko wabara na hili limedhihilika kwa wao kujitoa mhanga kwa kuwaondoa viongozi wakatili kwa kumwaga damu yao; mara hii itabidi wawaoneshe watu wa bara kuwa sasa imetosha na wao ndio watakaoamua nani awe kiongozi wao. Kama wabara hawatakubali wawe radhi kurudi visiwani na Aro Shirazi yao!!
 
Kama wabara hawatakubali wawe radhi kurudi visiwani na Aro Shirazi yao!!

Unajua vitu vingine unaongea halafu unakuja kufikiria baadaye badala ya kufikiria kwanza ndio uongee! Ok, tuambie kama wakirudisha Afro-Shiraz ndio itajenga barabara, italeta maji safi ya kunywa, itajenga shule, nk? Au kwa kuwa unadhani kwamba jina linatamkika vizuri vinywani mwa watu ndio maendeleo?
 
Zanzibar si nchi. nchi ni Tanzania, kama kwa hiyari yao waliamua kuungana na Tanganyika ni dhahiri walikuwa tayari kwa maamuzi ya kichama kufanyika na chama. Kwani walipo shindwa chaguzi zote visiwani (tokea 1995 mpaka 2005) walikuwa wanatangazwa washindi kwa maelezo ya watu toka Bara kwani ndiyo walioshika vyombo vya dola. Nina uhakika kama bara wataachia wanzanzibar wenyewe watauana kama senene. Ila bado wana-nafasi ya kujikwamua kama wote wataamua kutomchagua mgombea wa CCM atakayewekwa na bara na kumchagua Maalim Seif kwa 100% na kudemand atangazwe, baada ya hapo CCM bara watajifunza kuwa wanzibar wakichaguliwa mtu na wabara hawampigii kura.
 
Zanzibar si nchi. nchi ni Tanzania, kama kwa hiyari yao waliamua kuungana na Tanganyika ni dhahiri walikuwa tayari kwa maamuzi ya kichama kufanyika na chama. Kwani walipo shindwa chaguzi zote visiwani (tokea 1995 mpaka 2005) walikuwa wanatangazwa washindi kwa maelezo ya watu toka Bara kwani ndiyo walioshika vyombo vya dola. Nina uhakika kama bara wataachia wanzanzibar wenyewe watauana kama senene. Ila bado wana-nafasi ya kujikwamua kama wote wataamua kutomchagua mgombea wa CCM atakayewekwa na bara na kumchagua Maalim Seif kwa 100% na kudemand atangazwe, baada ya hapo CCM bara watajifunza kuwa wanzibar wakichaguliwa mtu na wabara hawampigii kura.
Point. wazanzibar ni watu wa ajabu. wanalalamika kama vile hawana njia mbadala.
 
Rais wa zanzibar angeteuliwa na rais wa Jamhuri ya Muungano kama wateuliwavyo wakuu wa mikoa...siona sababu ya kupoteza hela kumchagua mkuu wa mkoa mmoja wakati mikoa mingine wanateuliwa tu! hii Zanzibar kuwa nchi ni danganya toto...sijui hawa wazenj hawaoni au? si unaona Karume anaumendea u VP wa muunagano...yaani alikuwa mkuu wa mkoa tu sasa natanga ngazi ya kitaifa.
 
wazenji n i kama watoto wetu kwa hiyo c busara luwaachia kujiamulia mambo yao wenyewe ni lazima na muhimu sana kwa cc wabara kuingilia mambo ya kule la sivyo0 kitakuwa kisiwa cha kuzaliasha magaidi.....
 
wazenji n i kama watoto wetu kwa hiyo c busara luwaachia kujiamulia mambo yao wenyewe ni lazima na muhimu sana kwa cc wabara kuingilia mambo ya kule la sivyo0 kitakuwa kisiwa cha kuzaliasha magaidi.....
lakini lengo la muungano si kuitawala zanzibar bali kushirikiana katika mambo muhimu kwa hiyo kitendo cha kuwatawala kwa mambo yao ya ndani ni aina ya ukandamizaji
 
.................. ni kama koti,, likikubana unalivua tu. muda muafaka utafika
 
Unajua vitu vingine unaongea halafu unakuja kufikiria baadaye badala ya kufikiria kwanza ndio uongee! Ok, tuambie kama wakirudisha Afro-Shiraz ndio itajenga barabara, italeta maji safi ya kunywa, itajenga shule, nk? Au kwa kuwa unadhani kwamba jina linatamkika vizuri vinywani mwa watu ndio maendeleo?

Kama wewe unaongea halafu unakuja kufikiria baadae hiyo ni tabia yako mimi nafikiri kwanza kabla ya kuongea; nadhani umenipata! Hebu tuambie kitu gani ambacho wazenj watashindwa kukitimiza bila kusaidiwa na wabara? The cold war is over and Zanzibar could easily be another Singapore given the chance to decide for itself without the intervention of Kikwete and his gang.Zanzibar has immense potential waiting for some wise leadership to tap it!
 
Je ni vema watu wa bara kuhusika moja kwa moja kuchagua mgombea wa urais wa zanzibar kama CCM wanavyofanya? au wawaachie wenyewe mahamuzi yote?

Wagombea urais wa Bara na Visiwani wanachaguliwa na vikao vya chama vya kitaifa. kama Kamati kuu na mkutano mkuu wa chama

Si sahihi kusema wanachaguliwa na wabara.

vikao hivi vingeweza kufanyika Zanzibar au popote, na katika vikao hivi kuna uwakilishi kutoka pande zote kwa ratios walizokubaliana nazo.
 
Back
Top Bottom