Ya Viongozi wa Chadema na Kamati kuu, CDM ijipange?

HTML:
Huyo mgombea wa ccm Rukwa alisema yeye ni Yesu, mgombea urais ni Mungu baba na diwani ni Roho Mtakatifu. Kanisa lililaani na kuwakataza waumini kumshabikia mtu nayekufuru
Kama maneno hayo hayo yangesemwa na Mgombea mkristo na akashinda tusingekuwa na khadithi za kutengana na kunyanganywa ukristo kwa baadhi ya waumini

Sina hakika kuna maana gani iliyojificha kwa hayo maneno ya kujifananisha na Yesu, Mungu na Roho Mtakatifu lakini naamini si maneno mazuri kutumiwa kwa mzaha na mwanasiasa.
Kwanini?
kwasababu tunajua kuongelea au kufanya utani katika imani za watu kunaweza kusababisha madhara makubwa sana. Hata hapa Tanzania tuna mfano; Kumbuka yule aliyesema Yesu si Mungu, je tumesahau sakata lililofuatia. Je yule aliyechora katuni ya Mtume Mohamed kule Denmark. Je yule Mchungaji aliyekuwa anataka kuchoma Koran wakati wa maadhimisho ya 11/9. Na je vita ya kidini nchini Nigeria iliyoanzia kwa mchoma mishikaki! Mifano ni mingi, lakini nia nikujaribu kuona jinsi gani kitu kidogo kwenye mambo ya dini kinaweza kusababisha matafaruku mkubwa na hata vita!

Mwisho
Kwa vitu vinavyohusu dini ni bora wote tukajaribu kuviepuka, si rahisi mtu kujua matokeo ya kufanya utani kwenye dini za watu. Nafikiri kwa mifano ya hapo juu tunaweza ku-imagine reaction za watu dini zikihusishwa! Ni vyema dini nyingine na vyama vimeamua kujitenga na malumbano hayo ya Sumbawanga kwasababu hiyo inaweza kuchochea mzozo na kuhusisha hata maeneo mengine!

Mungu ibariki Tanzania!
 
ACHA MAJUNGU IJIPANGE NINI HASA?Kwa faida ya wale ambao hawakuipata TAARIFA KAMILI YA CHADEMA
Najua kuna wengi huenda hawakuipata hii. Nimeitafuta sijaiona jamvini baada ya rafiki kuniambia niitafute. Ila nimeikuta feacebook yake. Wanaoitafuta kama mimi, hii hapa

Msimamo wa Chadema haujabadilika

by Dr. Wilbrod Slaa on Tuesday, December 14, 2010 at 7:29pm



Kuna taarifa ambazo zimekuwa zikiandikwa na kuripotiwa na vyombo vya habari ambavyo zinaashiria kuwa Chadema tumebadili msimamo wetu kuhusu masuala ya uchaguzi.

Hakuna mahali popote Chadema imebadili msimamo wake na kusema kuwa Kura hazijaibiwa au kuchakachuliwa. Taarifa niliyotoa jana kwa TBC ilieleza wazi kuwa Kamati Kuu, ilipokea na kujadili na kuridhia mapendekezo yote yaliyowasilishwa na Sekretariat ya Chama kuwa Chadema imekataa matokeo ya Uchaguzi kutokana na irregularities 15. Chadema inaamini kuwa iwapo Katiba ya nchi isingelikuwa imezuia kuhoji matokeo ya uchaguzi Mkuu wa Rais mahakamani, matokeo hayo yangeliweza kubatilishwa. Kwa vile Katiba inakataza kuhoji matokeo kuhojiwa mahakamani, basi japo Kikwete's Presidency ni Lawful it is Illegitimate.

Chadema ilitumia maneno ya kiingereza kuonyesha tofuati kubwa kati ya maneno hayo mawili. Huo ndio msimamo wa Chadema toka mwanzo na haijawahi kuyumba, japo maneno ya kiswahili yamekuwa yakipewa tafsiri tofauti na watu mbalimbali. Ni kwa msingi huo, Kamati Kuu ikasisitiza " Kuundwa kwa Tume Huru" kuchunguza Dosari " Irregularities" hizo kubwa katika uchaguzi. Nasisitiza, Chadema ni Chama ambacho toka mwanzo ilisisitiza kuwa "Haiko Tayari kuingia Ikulu kwa kumwaga Damu ya Watanzania".

Inawezekana wanaopenda na kufurahia vurugu, Chadema haiko tayari kwa hali hiyo. Tunasukumwa sana na wapenzi na wanachame wetu kutoka mitaani na kuandamana, na ndicho pia wanachotaka ndugu zetu akina Mwanakijiji. Maandamano, (ya amani au ya kushinikiza), kwa watu wanaojua mchakato wa demokrasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kushindikana. Pili, ili Tanzania isiingie katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kwa Katiba na Sheria mbovu kama tuliyonayo leo, Chadema inasisitiza upatikanaji wa Katiba mpya, Shirikishi na ya Wananchi.

Upatakanaji wa Katiba hii utakuwa na mchakato, na kama Serikali haitaki, basi Chadema kwa kushirikiana na wadau na watu mbalimbali wakiwemo wananchi itatutumia njia zote zinazoweza kuipatia nchi Katiba ya Wananchi. Yote haya ni mchakato, na kwa mtu yeyote anayoamini kuwa mchakato huchukua muda, basi atakuwa mvumilivu. Hakuna sababu ya kutumia lugha kali, kukashifiana na kutukanana japo jamvi letu ni mahali ambapo "we dare to speak". Tukivumiliana na kuheshimiana tutafika salama bandarini.

Tukikurupuka tunaweza pia tusifikie lengo tunalotaka. Hekima na busara vikitawala na kuongoza matunda yatakuwa mazuri kwa Taifa letu. Taifa ni letu tukilibomoa hatuna pengine pa kwenda, labda tukiamua kulowea penginepo. Tukikurupuka tunaweza kuwaumiza wanaohusika na wasiohusika. Uvumilivu na Busara daima huvuta heri.




Source: Gonga hapa Msimamo wa Chadema haujabadilika | Facebook


NYONGEZA: Kuna thread imewekwa hapa chini na Mwanajamii mmoja (Chapakazi) anauliza tofauti ya maneno haya mawili (Lawful na Legitimate). Kwa uelewa wangu. Naomba niiongeze hapa kwa mtiririko sahihi. Unaweza toa usahihi zaidi


Moja ya tafsiri za legitimate zilizoko kwenye link hii define: legitimate - Google Search


Zinasema kitu legitimate ni kile ambacho kiko affirmed to be just na in accordance with recognized or accepted standards or principles.


Na kitu lawful ni kitu ambacho kiko recognized or sanctioned by law(lawful: meaning and definitions — Infoplease.com.


Kwa upeo wangu hii inamanishaa kitu kinaweza kuwa recognize na sheria lakini kisiwe just kwa sababu hakikiendana na accepted principles


Tukitumia mfano wa tukio lenyewe naweza kusema hivi,

Sheria inasema Raisi ni Raisi kwa kutangazwa na tume (lawful) lakini ili atangazwe lazima kanuni (principle) kadhaa zifuatwe.

Hivyo kama kanuni hazikufuatwa lakini katangazwa (kama sheria inavyotaka) na tume ya uchaguzi basi ni lawful kwa sababu katangazwa kisheria na tume yenye mamlaka ya kisheria kutangaza lakini kama kanuni za kufuatwa ili atangazwe zimevunjwa tunasema ni illegitimate kwa sababu principle s zimekiukwa.


Kwa msaada zaidi gonga hili link uone mfano kule Georgia

http://georgiandaily.com/index.php?o...2829&Itemid=68

DENYO,
Vipi leo mkuu,????
unarusha kitu hii katika kila thread! Tumeiona, mkuu.
 
kwasababu tunajua kuongelea au kufanya utani katika imani za watu kunaweza kusababisha madhara makubwa sana. Hata hapa Tanzania tuna mfano; Kumbuka yule aliyesema Yesu si Mungu, je tumesahau sakata lililofuatia. Je yule aliyechora katuni ya Mtume Mohamed kule Denmark. Je yule Mchungaji aliyekuwa anataka kuchoma Koran wakati wa maadhimisho ya 11/9. Na je vita ya kidini nchini Nigeria iliyoanzia kwa mchoma mishikaki! Mifano ni mingi, lakini nia nikujaribu kuona jinsi gani kitu kidogo kwenye mambo ya dini kinaweza kusababisha matafaruku mkubwa na hata vita!

KAYUMBA NDUGU JAMBO HILO KWA UKRISTO SIO ISSUE
Christian are never sensitive with such issues, kuna miparaganyiko mingi hata kwenye biblia yenyewe sembuse watu kumchagua mtu aliyeyasema hayo, angalia hata mtu hufananishwa na Yesu katika filamu nyingi, leo ukimuuliza mtoto wa sunday school atakwambia sura ya Mungu wao Yesu ipoje kwa kuwa it is normal na picha na sanamu zinashabikiwa sawa na vitu halisi sembuse maneno? angalia mfano kwenye biblia tu unakuta eti Yesu amnamwita mama yake, we mwanamke!,
Angalia pia kitabu kinachoitwa cha Mungu chenu kilivyo na matusi yaliyoandikwa na watu na mnasoma kwa utiifu ule ule halafu leo eti mnawatenga wenzenu waliomchagua mbunge wao
(a) A TALKING ass. NUMBERS 22:27-28

(b)
FOUR footed fowls. LEVITICUS 11:20
(c)


Birth of females a DOUBLE pollution. LEVITICUS 12:1,2,5
(d)


Shamgar KILLS 600 with an ox goad. JUDGES 3:31
(e)


Samson KILLS A THOUSAND with the jaw bone of a donkey.
JUDGES 15:15-16
(f)


A SEVEN HEADED leopard. REVELATION 13:1-2
(g)


To eat SHIT and drink PISS. 2 KINGS 18:27 and ISAIAH 36:12
(h)


DUNG on your faces. MALACHI 2:3
(i)


To eat cake with SHIT. EZEKIEL 4:12-15
(j) Samson has SEX with a ***** in Gaza. JUDGES 16:1
k)


Ruth COHABITS with Boaz in the barn. RUTH 3:4-15
(l) David SLEEPS with a young virgin. 1 KINGS 11:1,3

 
Sishangai, hii ndio aina ya watu wasio na umakini waliojaa Chadema, hii ndio inayoreflect pia uongozi wa juu (mwenyekiti na Katibu wa CDM) huwezi amini hawasomi , hawatafakari lakini mabingwa wa kujenga hoja !

hapa imenibidi kulog in na kukosoa kidogo. Huwezi kusema hawasomi lakini wajengaji hoja wakubwa
 
nilikuwa miongoni wa waliolaumu uamuzi wale wabunge wacdm kususa hotuba, niliainisha kwenye moja ya posting zangu kuwa (hapa nanukuu) " madai ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ni ya msingi, kuacha kuingia katika vikao vyote vya bunge hadi madai hayo yatakapotekelezwa ni ujasiri, kutoka bungeni wakati hotuba ya raisi inaanza ni unafiki, uzandiki, roho mbaya, ubinafsi na kuendeleza chuki zisizo na maana, sasa mwenye akili apime kutoka bungeni na kubaki kipi kinajenga heshima,kushawishi hata wabunge wasio wa chama chako kukubali hoja hizo ili ipatikane katiba na tume huru ya uchaguzi? Ninachofahamu madai ni ya msingi lakn njia iliyotumika inaturudisha nyuma sana, tunawategemea wabunge wa ccm katika hili, acheni utoto na siasa za chuki, chadema wamechemsha na lazima waambiwe?' (mwisho wa kunukuu).
yaliyoendelea kuhusu kuvuliwa unaibu upinzani bungeni kwa zitto niliona ni yale yale, nikafikia kutoa maoni kwa formula hapa jf na hapa nanukuu tena.
yr 2010, mh. Zitto(ujana&maendeleo duni kigoma)+ slaa(agenda ya ufisadi &kanisa)=kura mil.2, mp23
yr2015 ‘absence of zito in chadema + ccm kuteua mgombea mkristo = kura laki 3 mp 5.
this marks end of cdm
wenye msimamo mkali hapa jf hawakusita kuchafua hali ya hewa, wakisema asulubiweeeeeeeeee, msalitiiiiiiiiiiiiiiiii, wakasahau mchango wa zitto cdm, wengine wakafikia kusema mh zitto alijiunga na cdm akaikuta na umaarufu iliyonayo leo.no! Navyofahamu alijiunga tokea enzi za dr kabourou na ni mtu ambaye hata alipokuwa udsm alikuwa anashiriki vikao mbalimbali vya chama, personally nilishuhudia hilo.
point yangu hapa nataka ieleweke wazi kuwa baada ya kamati kuu kutoa kauli ya kumtambua rais na kumrudishia zk uongozi hadi uchunguzi utakapofanyika imezidi kumpandisha zk na kuonyesha kuwa alikuwa sahihi katika uamuzi wake, ikimaanisha kuwa ana busara za kushinda mwenyekiti wake na katibu wake pia .viongozi hawa wawili ambao kila siku naona ndio watakaoiangusha cdm kwa ajili ya siasa za fisasi,chuki,ubinafsi, kutaka sifa (hata kama chama kitaathirika) inaonesha hata hawakutaka ushauri wa kamati kuu kususia hotuba ya jk na kutomtambua kama rais(ambapo baadae wakajichanganya eti ilikuwa ni madai ya katiba mpya, tume huru na kutokubali matokeo ya tume, after thoughts???). Kitendo hiki ni udhaifu mkubwa na sasa naona mantiki ya zk kuomba uenyekiti wakati ule ambapo hata mimi nilimlaumu.
sijui mipango walionayo cdm kwa sasa lakini nawasihi wazee hawa wajipange kukisaidia chama kwa ushauri wa mara kwa mara na sio kusubiri wanachemsha, baada ya hili la zk wajitahidi kuondoa dhana ya ukaskazini na udini ambayo wanacdm wapende wasipende imejionesha kwenye uchaguzi uliopita, wakirudishe kuwa chama cha watanzania wote kama wanataka waaminiwe na kupewa dhamana ya kuongoza nchi. Cdm iwe na mipango thabiti na ya muda mrefu nakumbuka kwenye post moja mwana jf mmoja kama ilivyo kwa wengi alijinasibu sana kukusanya wanachama, eti tokea uchaguzi aliwapata 124, na kwamba zk hata akiondoka hakutakua na effect yeyote nakumbuka nilimwambia hivi, nanukuu,
" i dream chama makini chenye mipango , mipango ya miaka at least 20 hivi ijayo. Kiwe na programu maalumu ya kupata wanachama wasomi vijana, kuwe na programme ya semina elekezi kutoka kwa wataalamu waliobobea ktk siasa, waendelee kusoma na kufanya kazi zao,(their proffesionals) huku wakiwaelimisha jamii wanamotoka umuhimu wa mabadiliko, uhusiano kati ya kura na maendeleo ya kijamii na hivyo kujua umuhimu wa kupiga kura na kwa nini kuna vyama vingi, haya yote wayafanye kama volunteers wakibadilishana katika vipindi tofautitofauti vya masomo yao,likizo , pt, disertation na hata wakati wakiwa ktk maeneo yao walimoajiriwa. Aidha viongozi wa juu wawe wanawatambua wanawaenzi na kuwatia moyo, wao wenyewe wawe na programu za kwenda vijijini kwa mwaka si chini ya operation 5, wakafungue matawi na kuwatambulisha vijana wapiganaji katika maeneo yao.mwisho wa kunukuu.
mambo haya hayawezi kufanywa na viongozi wanaotaka uraisi kesho, au kesho kutwa.tulionao sasa, kama ni wazalendo kweli, waanzishe harakati na wakubali kuwa wakati muafaka wa kutwaa nchi hii wao watakuwa wamestaafu, maana watakuwa wamechoka! Ikumbukwe ccm ni chama chenye zaidi ya miaka 40, kina mizizi isiyoweza kungoka kwa agenda moja tu ufisadi, inahitajika mipango ya muda mrefu.
nawasilisha

so you want us to align with your line of thinking. Zk is still a traitor and ccm is based on amassing everything for this country to itself.

Hakuna suluhu ni mapambano ya ana kwa ana kimawazo na vitendo. Cdm haitambua matokeo ya uchaguzi inaelewa na inatambua katiba kandamizi imemtangaza rais hakuna mahahakama pa kupinga hilo huko siyo kumtambua rais.

Naomba utuvumilie na misimamo yetu kama ambavyo tunatoa changamoto kwa michango yako. Zk kesha jisulubisha ila kama atatubu atafufuka
 
Hapo umeJa**ba ka sio ku**ya kabsa., u cn't b serious umfananishe Zito na Slaa na Mbowe. Ni sawa na ufananishe Burj Dubai na Akiba house.
Great Thnker wengine bana..:(


huyo ndio GT, Atukana ovyo, huo ndio mdomo unaotumia kulia chakula? maana nauona mchafu sawa na back hole

Elimu ya Zitto ilishawafunika na sasa anawafunika kwa msimamo sahihi, kwa taarifa yako mnamtambua rais na hivyo njia iliyomuweka madarakani mnaitambua
 
quote_icon.png
Originally Posted by Aikaotana
Sishangai, hii ndio aina ya watu wasio na umakini waliojaa Chadema, hii ndio inayoreflect pia uongozi wa juu (mwenyekiti na Katibu wa CDM) huwezi amini hawasomi , hawatafakari lakini mabingwa wa kujenga hoja !



hapa imenibidi kulog in na kukosoa kidogo. Huwezi kusema hawasomi lakini wajengaji hoja wakubwa

My friend hapa

Maana yake mtu husomi na hautafakari lakini unaandika sana
 
so you want us to align with your line of thinking. Zk is still a traitor and ccm is based on amassing everything for this country to itself.

Hakuna suluhu ni mapambano ya ana kwa ana kimawazo na vitendo. Cdm haitambua matokeo ya uchaguzi inaelewa na inatambua katiba kandamizi imemtangaza rais hakuna mahahakama pa kupinga hilo huko siyo kumtambua rais.

Naomba utuvumilie na misimamo yetu kama ambavyo tunatoa changamoto kwa michango yako. Zk kesha jisulubisha ila kama atatubu atafufuka

Masikini if these are kind of people present at CDM, misimamo miikali visasi visasi visasi YOU HAVE GONE
 
Naomba niseme tu nilikuwa namfurahia Zitto kwa sana na kisha kumwona kama inspiration kwa vijana lakini sasa amekuwa kijana asiyeeleweka msimamo wake. Na tatizo lake kuu likiwa utata wa kauli zake na kulewa sifa haraka. Anaongea sana hata pale panapohitaji kukaa kimya. Mara sigombei tena ubunge,nataka kusoma ili nifundishe, sijui nigombee jimbo lipi, nataka uwenyekiti wa CHADEMA, Urais wa Tanzania, sikuunga msimamo wa chama wa kutoka nje ya Bunge kwa kuwa ningemdhalilisha rais n.k. Sasa ukimpa uongozi wa chama atatofautiana na Mbatia? Naona atakiuza kabisa kwa SISIEMU. Naona mwanzo wa anguko lake kisiasa umekaribia. Ngoma imevuma sana sasa inakaribia kupasuka! Nafikiri watanzania wamejua his true colours!
 
MaMkwe hiyo CCTP Maendeleo ni chama cha siasa au? Kiko nchi gani? Au ulimaanisha PPT Maendeleo cha Peter Kuga Mziray?
 
Elimu ya Zitto ilishawafunika na sasa anawafunika kwa msimamo sahihi, kwa taarifa yako mnamtambua rais na hivyo njia iliyomuweka madarakani mnaitambua

Inaonekana kuna watu bado wanafuata MTU na siyo sera za chama wala vision ya viongozi kwa ujumla wao, wanaCHADEMA hawafuati MTU tena, maana walikwisha jifunza kwa watangulizi wa mageuzi kama akina Mrema, Mtikila, Seif nk nk. Watu hawa walikuwa na wafuasi wengi ambao walikuwa wanawafuta bila kuangalia sera za chama. Matokeo yake ni wafuasi kugeukwa na viongozi wao na kukosa muelekeo.

Wazalendo wa kweli kweli hawafuati MTU wanafuata sera za chama na msimamo wa uongozi wote kwa ujumla. Zitto ni sawa na bati moja juu ya nyumba linalovuja, dawa ni kuling'oa na kuweka jipya nyumba haita vuja tena. CDM ni watu makini na wafuasi wao ni watu makini hawata yumbishwa hata Zitto akienda kwenye chama cha Baba Mkwe wake.

Watu wenye akili kidogo wasio kuwa na uchungu na nchi hii ndo watakao mfuata huko aendako lakini CDM itabaki imara daima! Kumbuka, wahenga walisema usipoziba ufa.... "watu watakuchungulia". CDM is strong enough cannot weaken by one silly particle jet out to CCM!
Peoples Power will stand for the sake of the Nation.
 
ACHA MAJUNGU IJIPANGE NINI HASA?Kwa faida ya wale ambao hawakuipata TAARIFA KAMILI YA CHADEMA
Najua kuna wengi huenda hawakuipata hii. Nimeitafuta sijaiona jamvini baada ya rafiki kuniambia niitafute. Ila nimeikuta feacebook yake. Wanaoitafuta kama mimi, hii hapa

Msimamo wa Chadema haujabadilika

by Dr. Wilbrod Slaa on Tuesday, December 14, 2010 at 7:29pm

Kuna taarifa ambazo zimekuwa zikiandikwa na kuripotiwa na vyombo vya habari ambavyo zinaashiria kuwa Chadema tumebadili msimamo wetu kuhusu masuala ya uchaguzi.

Hakuna mahali popote Chadema imebadili msimamo wake na kusema kuwa Kura hazijaibiwa au kuchakachuliwa. Taarifa niliyotoa jana kwa TBC ilieleza wazi kuwa Kamati Kuu, ilipokea na kujadili na kuridhia mapendekezo yote yaliyowasilishwa na Sekretariat ya Chama kuwa Chadema imekataa matokeo ya Uchaguzi kutokana na irregularities 15. Chadema inaamini kuwa iwapo Katiba ya nchi isingelikuwa imezuia kuhoji matokeo ya uchaguzi Mkuu wa Rais mahakamani, matokeo hayo yangeliweza kubatilishwa. Kwa vile Katiba inakataza kuhoji matokeo kuhojiwa mahakamani, basi japo Kikwete's Presidency ni Lawful it is Illegitimate.

Chadema ilitumia maneno ya kiingereza kuonyesha tofuati kubwa kati ya maneno hayo mawili. Huo ndio msimamo wa Chadema toka mwanzo na haijawahi kuyumba, japo maneno ya kiswahili yamekuwa yakipewa tafsiri tofauti na watu mbalimbali. Ni kwa msingi huo, Kamati Kuu ikasisitiza " Kuundwa kwa Tume Huru" kuchunguza Dosari " Irregularities" hizo kubwa katika uchaguzi. Nasisitiza, Chadema ni Chama ambacho toka mwanzo ilisisitiza kuwa "Haiko Tayari kuingia Ikulu kwa kumwaga Damu ya Watanzania".

Inawezekana wanaopenda na kufurahia vurugu, Chadema haiko tayari kwa hali hiyo. Tunasukumwa sana na wapenzi na wanachame wetu kutoka mitaani na kuandamana, na ndicho pia wanachotaka ndugu zetu akina Mwanakijiji. Maandamano, (ya amani au ya kushinikiza), kwa watu wanaojua mchakato wa demokrasia ni hatua ya mwisho kabisa baada ya njia zingine zote kushindikana. Pili, ili Tanzania isiingie katika uchaguzi mkuu ujao wa 2015 kwa Katiba na Sheria mbovu kama tuliyonayo leo, Chadema inasisitiza upatikanaji wa Katiba mpya, Shirikishi na ya Wananchi.

Upatakanaji wa Katiba hii utakuwa na mchakato, na kama Serikali haitaki, basi Chadema kwa kushirikiana na wadau na watu mbalimbali wakiwemo wananchi itatutumia njia zote zinazoweza kuipatia nchi Katiba ya Wananchi. Yote haya ni mchakato, na kwa mtu yeyote anayoamini kuwa mchakato huchukua muda, basi atakuwa mvumilivu. Hakuna sababu ya kutumia lugha kali, kukashifiana na kutukanana japo jamvi letu ni mahali ambapo "we dare to speak". Tukivumiliana na kuheshimiana tutafika salama bandarini.

Tukikurupuka tunaweza pia tusifikie lengo tunalotaka. Hekima na busara vikitawala na kuongoza matunda yatakuwa mazuri kwa Taifa letu. Taifa ni letu tukilibomoa hatuna pengine pa kwenda, labda tukiamua kulowea penginepo. Tukikurupuka tunaweza kuwaumiza wanaohusika na wasiohusika. Uvumilivu na Busara daima huvuta heri.


Source: Gonga hapa Msimamo wa Chadema haujabadilika | Facebook



Itakuwa vizuri kama tutajikumbusha kauli hizi hapa chini ambazo zilitolewa hapa Jamiiforum kwa kutumia ID ya Dr Slaa...

Ya kwanza ni hii ambayo ilitolewa siku ya pili baada ya wabunge wa CHADEMA kususia hotuba ya JK yaani tarehe 18/12/2010. Hi ilikuwa kama transcription ya taarifa ya Dr Slaa redioni jioni tu ya siku ile ya kumsusia JK.



Ndugu zangu Watanzania, pamoja na ndugu zangu wote waliokuwa wanafuatilia matukio ya bungeni leo. Aaah... ni kweli nimepata watu wengi wakiulizia, aah.. ni kwanini wabunge wa CHADEMA walitoka ndani ya ukumbi wa bunge, wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano alipoanza kutoa hotuba yake. Eeenh... moja ni kwamba CHADEMA ni chama chenye msingi, kinachofuatilia, eenh na kuhakikisha kwamba daima kiko consinstent yaani kinatekeleza kile ambacho kinasimamia, aah kwa kuwa tulikwisha kukataa kutambua matokeo ya uchaguzi, na vilevile baada ya kukataa kutambua matokeo tulikataa vilevile kumtambua rais aliyepatikana kwa mchaka.. eenh kutokana na mchakato huo ambao hatuutambui, basi ni dhahiri kabisa aah matendo yetu yaendane na kile tunachoamini.

Wabunge wetu wapo kwenye forum ambayo inasimamia kile ambacho CHADEMA inakiamini. Bunge ni mahali ambapo wabunge wana nafasi ya kubeba bendera ya CHADEMA, na mahali pa kwanza pa kuonyesha kwamba hatumtambui rais ni dhahiri basi ni kwamba ni ndani ya bunge. Kitendo cha leo kilianzia asubuhi, kwa wabunge wetu kutohudhuria hafla ya kumuapisha Waziri Mkuu, kwa sababu isingekuwa na maana kwenda kuhudhuria hafla ambayo inasimamiwa na rais ambaye kimsingi hatumtambui, lakini vilevile ni ishara kwa watanzania kwamba bado eenh tunataka maelezo ya kina kutoka serikali kuhusu kauli tulizokwishakuzitoa.

Baada ya kususia hafla ya leo asubuhi , hatua ya pili ilikuwa kususia hotuba ya rais, na jambo hilo lilifanyika, na hatua ya tatu ni kususia hafla ambayo inatokea leo usiku, ambayo tulikubaliana pia wabunge wetu wasihudhurie. Hizi ni ishara muhimu katika siasa, kupelekea kuipeleka kwa serikali kwamba kuna malalamiko ya msingi ambayo tunayo kuhusu mchakato wa uchaguzi, na ni dhahiri kwamba kama serikali ni makini, kama serikali ni sikivu basi itasikiliza kauli hiyo ya wenzetu ambao huko bungeni. Lakini kauli hizo hazitaishia pale, kama tulivyokwishakutoa katika press conference yetu, tulisema tutatumia forum ndani ya bunge, na forum inje ya bunge kupiga kelele mpaka serikali itusikilize.

Ni nini tunachokihitaji ? Tunahitaji, aah, demokrasia ya kweli katika nchi yetu, tunahitaji uchaguzi ambao utaendeshwa kwa misingi ya misingi ya demokrasia ya kweli. Tunahitaji tume huru ya uchaguzi. Eenh.. tunahitaji sheria mbovu ziweze kurekebishwa, ili chaguzi zisiendelee kuchakachuliwa kama ilivyotokea safari hii. Kwa hiyo haya ni mambo ya msingi ambayo hakuna mtu yeyote atatuambia tusiyadai, kwa sababu tumelalamika mara nyingi juu ya kat.. ya marekebisho ya katiba, serikali imekuwa si sikivu haitaki kusikiliza, tumedai kuhusu tume huru, serikali imekataa kutusikiliza, tumedai marekebisho ya sheria mbalimbali ambazo ni kandamizi serikali haitusikilizi, tumedai serikali iache kutumia vyombo vya dola hasa polisi na FFU katika uchaguzi serikali haitusikilizi. Kwa hiyo namna pekee ya kudai haki, ukiona mazungumzo ya kistaarabu hayafanyiki basi unapiga kelele. Na hii ni namna mojawapo ya kupiga kelele.Tukumbuke kwamba CHADEMA tumesema hatuhitaji vurugu, hatuhitaji kuwaambia wananchi waende mitaani kwa maandamano - hata kama ni ya amani kwa hatua ya awali - tukitegemea kwamba serikali itatusikiliza, tukae pamoja au ituahidi kwamba itafanya haya marekebisho kabla ya uchaguzi wa 2015. Bila ya kuchukua hatua kama hizi, 2015 tutarejea kwenye mchezo huo huo mchafu, kura zitaendelea kuchakachuliwa, vyombo vya dola vitaendelea kutumika, watanzania wataendelea kunyanyasika, na ukombozi ambao tumewaahidi watanzania hautaweza kupatikana.

Kwa hiyo kimsingi yaliyotokea ni tafsiri ya press conference ambayo tulifanya siku chache zilizopita pale Dodoma, inawezekana Watanzania wengi hawakuelewa ile press conference. Sasa hii ni tafsiri ya ile press conference, na tunawaomba Watanzania watuelewe kwamba tuliposema tutatumia ukumbi wa bunge, na tutatumia eenh.. fora nyingine nje ya bunge, hii ndiyo maana yake. Inje ya bunge tumesusia hafla mbalimbali, ikiwemo hii ya waziri mkuu kuapishwa, kikiwemo ya chakula cha rais, lakini nahafla zingine zitakazoendelea ambapo rais ataendelea kuwa ndiye mwenye hafla hiyo. Eenh, lakini vilevile tumesema kwamba tutakwenda kwa wananchi kuwaeleza sasa ni nini kimetokea.

Kwa hiyo watu wasishangae kwamba tunafanya mikutano yenye sura ya kufafanua zaidi hatua zetu maana yake ni nini, nadhani hii ni kitu ambacho kila mtanzania anaielewa, na kwa simu tulizopokea mpaka sasa hivi, sms ambazo nimekuwa nikizipokea mpaka sasa hivi, watanzania wengi sana wametusifu , wamepongeza wabunge wetu. Ninaomba Watanzania wote wenye nia njema watuunge mkono katika kilio hiki, lakini tukizingatia kwamba yote tunayofanya yawe kwa msingi ya amani, tusitoke mitaani kama tulivyokwishakuwaomba. Watanzania kama wa Shinyanga ambao wamechakachuliwa kura za mbunge wao waziwazi, Watanzania kama wa Mbozi ambao wamechakachuliwa kura zao waziwazi, Watanzania kama Segerea ambao wamechakachuliwa kura zao waziwazi, tunaendelea kusisitiza kwamba, mazungumzo daima ni njia bora ya kuondoa migogoro. Kwa hiyo tusingependa katika hatua hii eeenh yale yaliyotokea yaendelee kutokea.

Ninawaomba amani, ninawaomba utulivu lakini tuendelee kudai haki zetu kwa njia ambazo zinaweza kuzaa matunda.


Ya pili, ni hii iliyotolewa tena katika ID ya Dr Slaa siku iliyofuata yaani tarehe 19/12/2010......


Mkandara,

Thanks. Nadhani message ya Wabunge na ya kwangu iko very clear isipokuwa kwa mtu anayetaka tu kui spin au kuibadilisha kwa sababu anayoitaka mwenyewe. Naomb kurejea mambo ya msingi kwa wale ambao kwa bahati mbaya yamewapita na wana nia ya kuelewa ili spinning hii isiwabughudhi.

Mara baada ya uchaguzi, tarehe 3 November, 2010 Dr. Slaa alifanya Press Conference Makao Makuu ya Chadema kama Mgombea Urais ambaye hakuridhika na mchakato wa uchaguzi na Matokeo yaliyokuwa yakitolewa kupita Vituo vya TV na Jaji Lewis Makame, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi. Katika Press Conference hiyo Dr. Slaa alitaja dosari nzito katika mchakato wa uchaguzi na hasa katika hatua ya kujumlisha na kutangaza Taifa ambapo matokeo yaliyokuwa yakitangazwa na NEC yalitofautiana kwa kiwango kikubwa sana na yale yaliyotangazwa na Wasimamizi wa Uchaguzi (W) pale ambapo zoezi hilo lilifanyika. Nikatoa Mfano wa Geita.

Pili, nilieleza kuwa Katika majimbo takriban 25 zoezi la majumlisho halikufanyika kama inavyotakiwa na sheria na hivyo matokeo kutangazwa na wasimamizi kwa utaratibu kinyume na sheria na kanuni za uchaguzi. Tatu, nilieleza kuwa katika maeneo mengine kama Kinondoni masanduku yapatayo 25 ambayo tunayo namba zake tunazo yalipatikana katika ghala la Shule ya Sekondari ya Biafra Jijini Dar-Es-Salaam ambayo hayajahesabiwa na matokeo yamekwisha kutolewa.Nne, Siku ya tarehe 28 October, Tume ya Taifa ya uchaguzi ilialika Wataalam wa IT wa vyama, na kuwa mbele ya Wataalam hao mfumo wa computer uliokuwa unatumika uli "collapse" na Tume kuwajulisha Wataalam kuwa wataita LapTop zote kutoka nchi nzima zirejeshwe Dar kwa matengenezo ya program husika. Ni kuwa wataitwa tena kujulishwa kama zimetengenezwa. Hawakuitwa tena. Hivyo mfumo wa Computer uliotumika kukusanya matokeo na upeleka Taarifa NEC unatia mashaka makubwa.Hata hivyo,baadaye tulipokea Barua kutoka NEC ya tarehe 28/10 ambayo ililetwa kwa Dispatch Makao Makuu Chadema tarehe 5 November, ikisema " Watalaam walikuwa na kukagua mfumo wa IT unaotumika na Tume na waliridhika" .

Ni dhahiri barua hii inatia mashaka kwanini barua ya tarehe 8/10 iletwe kwa dispatch na ifike siku takriban 8 baadaye? Hali hii inatia mashaka kuwa barua hii imekuwa backdated kwa Tume kuficha ukweli wa Scandal kubwa iliyotokea katika mfumo ambao uligharimiwa kwa fedha nyingi na UNDP. Iwapo Tume inaweza kudanganya katika swala kama hili tutatukuwa na imani gani na Tume tena. Kutokana na dosari hizo kubwa (pamoja na mambo hayo yaliyojitokeza baadaye)

Dr. Slaa, kama Mgombea aliitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi ifanye mambo yafuatayo:

i) Kusimamisha Zoezi la Kutangaza matokeo hadi uchunguzi kamili utakapokuwa umefanyika ili kuondoa hisia na tofauti zilizoanza kujitokeza. Ikumbukwe kuwa Tofauti hizi kimsingi ziligundulika na Wananchi wenyewe kutokana na Tarakimu alizosoma Jaji Makame kutofautiana na zile zilizotangazwa na Wasimamizi katika maeneo yao. Matokeo yake wananchi waliingia mitaani kupinga hali hiyo. Hayo yalitokea Geita, Shinyanga, Mbozi Mashariki na kadhaa. Matokeo yake wananchi hao waliokuwa wanadai haki zao walipigwa mabomu na polisi. Njia ya Busara ilikuwa kuitaka Tume kusitisha zoezi hili ili lisilete athari zaidi, japo hawakufanya hivyo. Chadema tulifanya jitihada za ziada kuwasihi wananchi wetu wasiingie mitaani kuepusha shari.

ii) Kuitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufuta uchaguzi na kutangaza upya marudio ya uchaguzi kwa kuwa Tofauti zilizoko ni kubwa sana, na nikatoa mfano wa Tarakimu za Geita CCM 17,792 CDM 3,789 ( Iliyotangazwa na RO Geita CCM 30,960 CDM 22031) Ni wazi kilichotokea hapa ni kuchakachua kwa lengo la kupunguza kabisa kura za Dr. Slaa, japo za JK nazo zimepunguzwa). Jimbo la Hai CCM 35,910 CDM 18,513 (Iliyotangazwa Hai na RO CCM 20,120 CDM 26,724 = Uchakachuaji uliofanyika hapa ni wa kumwongezea JK kwa zaidi ya kura 15,000 na kupunguza za Dr. Slaa kwa zaidi ya 8,000). Nilitoa pia mfano wa Ubungo ambapo kwa mujibu wa CCM 68,727 CDM 65,450(iliyotangazwa na RO CCM 70,472 CDM 72,252 hapa nako uchakachuaji ulioafanyika ni wa kupunguza kura za Dr. Slaa kwa Takriban 8,000 na kupunguza za CCM kwa kama 2000 hivi) Katika Jimbo la Bunda CCM 20,836 CDM 571 ( Iliyotangazwa na RO CCM 20,836 CDM 18,445 = Tarakimu za Bunda zimerekebishwa katika Taariffa ya mwisho ya NEC. Taarifa hii inaonyesha kuwa Dr. Slaa alipewa kura za Lipumba). Jimbo la Karatu ni kichekesho zaidi kwani kwa mujibu wa Taarifa ya awali ya NEC iliyonukuliwa na Mwananchi CCM 24,364 CDM 41 ( iliyotolewa na RO CCM 24,364 CDM 43,137. Taarifa ya mwisho ya NEC imerekebishwa kufanana na ya RO Karatu. Tume ilikiri kuwa imekosea Taarifa ya Geita japo hadi leo haijarekebisha Taarifa hiyo.

Hadi leo hii tarehe 19/11 Tume haijatangaza matokeo ya Geita, Tumbe, Tunduru Kaskazini, na Vunjo kwenye Website yake. (Tume ilikiri siku ya kujumlisha matokeo Taifa kuwa Vunjo kulikuwa na Taarifa mbili na ikaamua kutumia ile ambayo haikusainiwa na mawakala na kutumia ambayo haina saini ya mawakala. Ni akili ya kawaida tu kujua kuwa kuna jambo hapo.
Hivyo basi kutokana na Dosari hiyo kubwa mgombea yeyote anayekubali kupokea matokeo atakuwa mwendawazimu. Ndiyo maana nikakataa kutambua matokeo na kumtambua Rais aliyepatikana kwa matokeo hayo.

2:Tarehe 15 November, katika Press Conference iliyofanyika Dodoma, Dr. Slaa, alikabidhi rasmi majukumu kwa Chama kwa kuwa kazi ya Mgombea Urais imefikia mwisho wake Baada ya Rais kutangazwa kwa mujibu wa Katiba (Mbovu) ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa chombo ambacho kilikasimiwa madaraka na Kamati Kuu ya Chama ( Sekretariat) mbele ya Wabunge wa Chama. Chama kilipokea majukumu na kuelekeza utekelezaji na ufuatiliaji maazimio hayo ya kukataa matokeo na kumkataa Rais kufanyika kuanzia siku hiyo na Vyombo mbalimbali na ngazi mbalimbali za Chama, na Wabunge wa Chama. Hivyo kilichotokea Bungeni ni utekelezaji wa maamuzi ya Chama hadi pale ngazi za juu za Chama zitakapobariki au kubadilisha msimamo huo. Ni dhahiri basi,

i) Wabunge wetu wala Dr. Slaa, hawakuhitaji kurudia madia ya msingi ikiwa ni pamoja na kurudia uchaguzi. Madai ya Mabadiliko ya Katiba au Katiba ya Wananchi na kudai Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kujiuzulu na Kuundwa kwa Tume ya uchunguzi ni madai yaliyotolewa katika Press Conference ya Tarehe 15/11. Hata hivyo, msisitizo wa awali ni kwa kuundwa kwa Tume ya Uchunguzi ambayo inaweza kutupelekea kwenye yote hayo. Mtu yeyote asiyemakini kufuatilia mtiririko huo anaweza kupotosha na kusababisha vurugu na uchochezi ambao Chadema, pamoja na jitihada zake za kudai haki zake na za wananchi waliochakachuliwa kura zao inapenda kufuata njia za kistaarabu na za amani. Ni vema yeyote anayetaka kufanya analysis ya hatua za Chadema kwanza akajielimisha vizuri badala ya kuweka hisia zake (hakuna sababu ya kuandika na mate wakati wino upo, na wakati wowote Chadema tuko tayari kutoa ufafanuzi utakao hitajika, isipokuwa ule unaopaswa kupitia kwenye vyombo vyetu vya maamuzi kama chama cha kidemokrasia.


Jamani. Uungwana nao waweza kuwa mtaji mkubwa kisiasa. Jaribuni hili la kukubalia kuwa tulikosea na sasa tupo tayari kujisahihisha. Hapa sio Kabwe tu atakayekuwa mshindi, Chadema na haswa Dr Slaa atarudisha na kulinda heshima yake lakini sio huu mchezo unaofanyika sasa ambao ni tofauti na fikira zetu kuhusu Dr Slaa.

 
Itakuwa vizuri kama tutajikumbusha kauli hizi hapa chini ambazo zilitolewa hapa Jamiiforum kwa kutumia ID ya Dr Slaa...

Ya kwanza ni hii ambayo ilitolewa siku ya pili baada ya wabunge wa CHADEMA kususia hotuba ya JK yaani tarehe 18/12/2010. Hi ilikuwa kama transcription ya taarifa ya Dr Slaa redioni jioni tu ya siku ile ya kumsusia JK.





Ya pili, ni hii iliyotolewa tena katika ID ya Dr Slaa siku iliyofuata yaani tarehe 19/12/2010......




Jamani. Uungwana nao waweza kuwa mtaji mkubwa kisiasa. Jaribuni hili la kukubalia kuwa tulikosea na sasa tupo tayari kujisahihisha. Hapa sio Kabwe tu atakayekuwa mshindi, Chadema na haswa Dr Slaa atarudisha na kulinda heshima yake lakini sio huu mchezo unaofanyika sasa ambao ni tofauti na fikira zetu kuhusu Dr Slaa.


Bora wewe umekuwa muungwana naomba uendelee kutoa elimu kwa kina Denyo wanaotaka kutumia hoja ya nguvu kuhalalisha makosa ya SLAA , kutangazan kutomtambua rais na kuwalisha sumu wabunge ambayo ina negative effect inayoendelea
 
Sifa ya kiongozi makini hawezi kuwa kigeugeu, leo hili kesho lile, tunachojua huku uraiani ni kuwa CDM wameufyata mkia kwa CCM na wamemkubali rais, ikitokea hotuba nyingine yha jk popote CDM front sit......teh...teh...teh
 
Back
Top Bottom