Ya Mh. Magufuli na Mh. Jery Slaa

Lweye

Senior Member
Apr 15, 2010
149
85
Jana jioni (kwenye saa 11 hivi) nilikuwa nikisikiliza Radio One. Nilimsikia Mh. Jery Slaa akipinga kwa nguvu zote amri ya Dr. Magufuli ya kuondoa mabango kwenye hifadhi za bara bara. Sababu kuu aliyokuwa akito ni kuwa eti, utekelezaji wa amri hiyo utashusha kwa kiasi kikubwa sana mapato ya Manispaa hivyo huduma kwa wananchi zitateteleka. Pamoja na mambo mengine, matamshi yake yalionesha kuwa Mh. Magufuli atumii busara katika maamuzi yake, anatumia madaraka vibaya na hawajali wapiga kula wake.

Baada ya kusilikiza mjadala ule nilijipa muda wa kutafakali na nimeona kuwa hizi kelele wanazopiga waheshimiwa madiwani sio bure kuna faida wanayoipata kutokana na mradi huu wa mabango. Sababu za kusema hivyo ni hizi:-

1. Kama kweli waheshimiwa hawa wanaona mabango yakiondolewa wananchi wataumia sana mbona hatujaona wakitoa hata neno moja wakati nyuma za wananchi hao zikibomolewa tena bila fidia.

2. Kama Sheria ipo na Mh. Magufuli anaitekeleza hapa Mh. Pombe hana kosa labda Mheshimiwa Slaa awashauri wabunge walio katika jimbo lake (ambao tena ni wajumbe wa baraza la madiwani) wakaichakachue bungeni kama ile ya Chama kikuu cha upinzani bungeni. Vinginevyo Magufuli songa mbele.

3. Eti mabango yakiondolewa mapato yatashuka! Duh! Hapa ndio nilichoka kabisa. Sasa kama mapato yenyewe yanapatika kwa biashara haramu anataka Mh. Magufuli afumbe macho tu eti kwa kuwa manispaa inameki! Kama ni hivyo basi mie namshauri Mh. Slaa aishauri manispaa ya Ilala ianze biashara ya Madawa ya kulevya au Walime mashamba ya Bangi kule chanika manake biashara hii inalipa sana. Alafu tutaona kama kamanda Kova akifanya vitu vyake atamwambia unajua tunalima bangi ili tujenge bara bara na hospitali kila kata.

Mie namshauri Mh. Jery Slaa aache kuleta ubishi ambao hauna maana na ajaribu kutafuta vyanzo halali vya mapato.

Big up Mh. Dr. JP Magufuli!
 
Jana jioni (kwenye saa 11 hivi) nilikuwa nikisikiliza Radio One. Nilimsikia Mh. Jery Slaa akipinga kwa nguvu zote amri ya Dr. Magufuli ya kuondoa mabango kwenye hifadhi za bara bara. Sababu kuu aliyokuwa akito ni kuwa eti, utekelezaji wa amri hiyo utashusha kwa kiasi kikubwa sana mapato ya Manispaa hivyo huduma kwa wananchi zitateteleka. Pamoja na mambo mengine, matamshi yake yalionesha kuwa Mh. Magufuli atumii busara katika maamuzi yake, anatumia madaraka vibaya na hawajali wapiga kula wake.

Baada ya kusilikiza mjadala ule nilijipa muda wa kutafakali na nimeona kuwa hizi kelele wanazopiga waheshimiwa madiwani sio bure kuna faida wanayoipata kutokana na mradi huu wa mabango. Sababu za kusema hivyo ni hizi:-

1. Kama kweli waheshimiwa hawa wanaona mabango yakiondolewa wananchi wataumia sana mbona hatujaona wakitoa hata neno moja wakati nyuma za wananchi hao zikibomolewa tena bila fidia.

2. Kama Sheria ipo na Mh. Magufuli anaitekeleza hapa Mh. Pombe hana kosa labda Mheshimiwa Slaa awashauri wabunge walio katika jimbo lake (ambao tena ni wajumbe wa baraza la madiwani) wakaichakachue bungeni kama ile ya Chama kikuu cha upinzani bungeni. Vinginevyo Magufuli songa mbele.

3. Eti mabango yakiondolewa mapato yatashuka! Duh! Hapa ndio nilichoka kabisa. Sasa kama mapato yenyewe yanapatika kwa biashara haramu anataka Mh. Magufuli afumbe macho tu eti kwa kuwa manispaa inameki! Kama ni hivyo basi mie namshauri Mh. Slaa aishauri manispaa ya Ilala ianze biashara ya Madawa ya kulevya au Walime mashamba ya Bangi kule chanika manake biashara hii inalipa sana. Alafu tutaona kama kamanda Kova akifanya vitu vyake atamwambia unajua tunalima bangi ili tujenge bara bara na hospitali kila kata.

Mie namshauri Mh. Jery Slaa aache kuleta ubishi ambao hauna maana na ajaribu kutafuta vyanzo halali vya mapato.

Big up Mh. Dr. JP Magufuli!

Kama Magufuli ana ubavu na anayoyafanya aachane na ujenzi wa barabara inayoanzia Mwenge kupitia Lugalo jeshini bali ipanuliwe barabara ipitiayo Sam Nujoma - cocacola - Kawe. HAlafu tumuone!!
 
Hapa ndio inaonesha wazi kuwa hawa viongozi wa hizi manispaa hawafikirii kabisa au uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana:A S 13:, sasa issue niya kisheria na huwezi kuipinga kwa kupiga makelele... Namshauri Mh. Dr. Magufuli ang'oe yote ili watanzania tujifunze kuheshimu sheria!!
 
Kama Magufuli ana ubavu na anayoyafanya aachane na ujenzi wa barabara inayoanzia Mwenge kupitia Lugalo jeshini bali ipanuliwe barabara ipitiayo Sam Nujoma - cocacola - Kawe. HAlafu tumuone!!

Mkuu tunapoandika humu tuwe tunajua tunachoandika ni nini.. kwa taarifa yako new bagamoyo inapita katikati ya kambi ya jeshi lile ni eneo la jeshi na linasimamiwa na sheria za jeshi, ilipita kwa makubaliano maalum ndo maana kama unakumbuka zamani ile barabara ilikuwa mwisho kupita saa 2 usiku... Barabara ya serikali ni ile ya old bagamoyo lakini hata yenyewe haikuwa barabara kuu ndo maana bado haina nafasi ya kutosha.... Lakini pamoja na hayo yote hiyo haizuii sheria isichukue mkondo wake, wabongo tujifunze kufuata sheria... kama kiongozi mkubwa kama maya anafanya mambo ya ki***zi vipi kwa sisi tulomchagua!!!!:A S 13:
 
Yale mazungumzo niliyasikia saana ya redio one unajua sikuweza kujua mara moja kuwa rafiki yangu Jerry upeo wake ndio ule, walionesha ufinyu wa fikra na sijui kwa nini waliomba kwenda redio one maana naona kama walijichoresha sana . kwa Mtanzania wa sasa unamwambia eti pindisha sheria hapa kwa sababu hii ni manispaa na inapata mapato, mtoa mada katoa mfano mzuri sana wa shamba la bangi. Na alichokisema Jerry ni typical serikali ilivyo hii na ndo maana kila Rostam wameiweka tz na rais wake mfukoni.

Jerry na mwenzako hampati tena udiwani tena i swear ! Swala hapo ambalo mlikuwa mnazunguka ni kuwa mnapata ulaji wenu binafsi toka kwenye mabango ndo maana mlikuwa hamna point kabisa.
 
Kama sheria yetu inasema mabango yasiwepo, basi tunashukuru kwa kiongozi asieogopa kutekeleza sheria.
Ni watu wachache wanaoweza kuitekeleza,
Nadhani ata wengi wetu hapa tuna vigugumizi, inapokuja swala la popularity vs sheria, au kulamba miguu ya wakubwa vs kutekeleza wajibu.
Hongera sana MAgufuli tuko nyuma yako, nadhani hautaishia kwa wakazi hizo barabara, bali ZOTE. Je mabango, ujenzi, biashara kwenye barabara ZOTE vitakuwa ndio mwisho???
 
Labda hizo manispaa hazina wataalam wa kubuni njia za mapato!!
 
Hawa Halmashauri hoja yao haina msingi mambago yametolewa kwenye hifadhi za barabara za Tanroads, bado wanaweza kuweka sehemu ambazo si hifadhi za barabara za Tanroads na kwenye barabara zote za halmashauri lakini kwa kupenda ulaji na mapato wanakomaa waweke kwenye hifadhi za Tanroads. Vyanzo vya mapato wanavyoving lakini wameshindwa kuviutilise ili waongeze mapato mjini hawajajenga parking hata moja kutwa kukmbizana na magari kukusanya mapato ya parking kwenye hifadhi za barabara badala kujenge majengo ya parking, kutwa kukimbizana na machinga badala ya kuwajengea maeneo na wao wakusanye kodi kwa ulaini nk.
 
Harafu ukitazama hao kina Jerry wanataka pesa hizo za mabango kwa manufaa yao binafsi kwa sababu wananchi wangapi wanabomolewa nyumba na hali wanalipa kodi za majengo manispaa mbona hatujawasikia walalamike? ni wapuuuzi kweli kweli hawa, harafu sijui niwaweke kundi gani. Nakwambia hampati tena hizo sit.
 
Back
Top Bottom