Ya ITV & RFA NA TANGAZO LA KULAZIMISHA NGONO...

Viongozi wetu, wake kwa waume, ni malaya wakubwa kila dakika ipitayo wanawaza na kuwaka kwa matamanio ya ngono. Je unategemea nini kutoka kwao??
Viongozi wetu wanaifumbia macho ngono kwa sababu ngono ni moja ya vionjo vikuu vya maisha yao.
Mambo hayaendi bila ngono.

Ngono katika TV ni matokeo ya muda mrefu ya kuwaza ngono.
Mawazo yao ya kingonongono yanayo wawasha kila siku sasa wameyaweka hadharani ili kila mtu aambukizwe na ikiwezekana anene na kutenda kama wao.

Ni aibu na uchuro mkuu wa kijamii
 
Hakuna cha aibu wala nini, utitiri wa matatizo ktk ndoa unasababishwa na kubakana ktk ndoa, wanaume wakitanzania hawajuwi kubembeleza hadi mwenz wake ajisikie ila wanalazimisha sm tm hata kwa maandiko, tusinyimane... Ujinga huu tunajenga taifa lisilo na ndoa madhubuti ila malalamiko ambayo mwisho wake kuvunjika ndoa.


Hilo suala siyo kweli kwani katika ualisia ukisikiliza tangazo lenyewe huyo mwamke kama angekuwa na busara hasingelalamika kama anataka kubakwa angeweza kumueleza mwenza wake kwa lugha ya upendo,dear najisikia nimechoka kwahiyo naomba tupumzike mpenzi tuta do baadaye,atasisi wanaume tunaakili si kwamba tunapenda kulazimisha kila wakati.Tatizo la lugha aliyotumia ni kumsababishia kutafuta mbadala
 
hivi vitu vya misaada vina matatizo sana,maana lile tangazo ni msaada wa wamarekani,mimi ndo maana nauchukia umaskini

Kweli hilo ni tangazo kwa msaada wa watu wa wa marekani bado tusubiri matangazo ya ushoga nayo kwa msaada wa watu wa marekani hamtaki wanasitisha misaada.
 
tunawapa wazazi wakati mgumu sana kutazama/kusikiliza hili tangazo wakiwa na watoto wao..
Binafsi hili tangazo linalorushwa itv na redio hasa rfa halina maadili, kuna ulazima gani wa kurusha sauti ya mwanamke akilalamika kwa sauti huku mwanamume akisikika kwa sauti ya kulazimisha kufanya mapenzi.

Kamalengo la tangazo hili ni kutoa uelewa juu ya unyanyasaji wa kijinsia, watoaji wa tangazo hili wamekosa namna nyingine ya kutoa ujumbe huu? Hivi hakuna tume ya maadili na malezi ambayo inaweza kudhibiti matangazo kama haya?

Tafakari!

jamani kama kuna tangazo ambalo nimelichukia ni hilo la kulazimisha ngono. Yaani nimefikiria nakujiiliza hivi kweli hata mheshimiwa mengi anakubali tangazo kama hilo litolewe kwenye tv yake?

Hivi waliolilipia hili tangazo wamefikisha kweli ujumbe huu kwa walengwa au wamewafundisha watoto na vijana waende kujaribu kufanya tendo la ngono. Mimi ninayeandika hapa sina watoto niliopewa na mungu au kuwazaa mwenyewe lakini naishi na watoto wa ndugu zangu na wadogo zangu ambao bado nahitaji niwasaidie wasishiriki tendo hili mpaka waingie kwenye ndoa lakini sina amani ninapokaa sitting room nakuangalia taarifa ya habari nakosa raha na hata watoto wanakosa raha na amani.
Ninaomba sana tena sana mengi toa tangazo hili ni dhambi kwako kuchukuwa hela ya tangazo kama hili, halijengi bali linabomoa maadili ya kitanzania
ninaungana na wenzanu wote kusema litolewe tangazo hili
amina
 
nilijua ni peke yangu nnayetapishwa na tangazo hili, kumbe wengi! Huwa tangazo hilo likianza naona bora niwatume watoto ghafla kwenda dukani kuninunulia konyagi hata kama ipo kwenye stock ndani!
Ni tangazo la aibu na kuzidhalilisha familia na halifundishi kitu!

inatisha sana,kwa namna hii,tunadhalilishwa sana wazazi na tangazo,laiti ningekuwa mkoma tcra ningejiudhuru haraka sana ama kuliban hilo tangazo haraka sana
 
inatisha sana,kwa namna hii,tunadhalilishwa sana wazazi na tangazo,laiti ningekuwa mkoma tcra ningejiudhuru haraka sana ama kuliban hilo tangazo haraka sana

.
Siku hizi hakuna mtendaji anaethubutu kutolea tamko issue inayojitokeza katika jamii. Wanahofia kuwa ikulu inaweza kuja na tamko tofauti na lile walilotoa. Hata polisi hawamkamati fisadi bila idhini ya ikulu. Wala mahakama hazihukumu kesi zinazowahusu waheshimiwa bila maelekezo toka ikulu. Kila kitu kwa sasa kimerudishwa ikulu na ni wazi hakuna rangi tutaacha kuona hadi ifikapo 2015.
.
 
Wandugu,

Nimefatilia kwa makini mjadala huu lakini kikubwa kinacho onekana ni malalamiko tu pasipo kuweka wazi hoja ya msingi. Tunaposema tangazo halina maadili, tuna maanisha nini? Hivi, maadili yetu "watanzania" ni yapi hasa? Kihistoria, 'maadili ya mtanzania' imekuwa ni zaidi ya dhana ya kudhania na kufikirika tu. Hakuna mahala pamepata kuwekwa orodha ya "Haya Ndio Maadili Yetu". Yapo? Yaliwekwa na nani? Kwa maoni yangu, niko tayari kukosolewa kwa hoja sahihi, dhana ya "Maadili Yetu" imekuwa ikitumiwa vibaya na baadhi ya wenzetu, aidha viongozi, wanajamii wa kawaida ama makundi fulani fulani ili kuweza kulinda maslahi ya chochote kile ambacho wataona kuwa hakivutii utashi wao. na kisha kutaka kuaminisha umma mzima wa "watanzania" kuwa kile wasichokifurahia, basi hakistahili kwa umma uliobaki. Hii ni dhana potofu!

Pia tukirejea kwenye ma/tangazo husika, jamani, si linasema wazi kuwa "Kulazimisha mapenzi, hata kwa mke wako ni ukatili!"? Ina maana hatukubaliani na suala hili? Ama ni kwa kuwa tumekua tukiaminishwa kuwa ukiwa na mke unaweza kufanya naye mapenzi wakati wowote, sehemu yoyote hata kama yeye hajisikii hivyo? Sio sahihi jamani, vitendo hivi vimekuwepo, vipo, baadhi yetu wanavifanya na hawana budi kuviacha. Bila shaka, yawezekana ujumbe huu ukawa umegusa maslahi ya baadhi yetu na ndio maana yanatokea mayowe yote haya. Sioni ajabu wala soni eti kwa ujumbe huu kutolewa wakati umekaa aidha na wakwe, wajomba, shangazi, na wengineo, kwani na wao wote na vizazi vyao wanapaswa kulielewa hili na hata kuweza kuwaelimisha wengine. Mbona elimu ya ngono, afya ya uzazi, maambukizi ya VVU n.k inafundisha hata shule ya msingi? Ina maana hata wewe waogopa kujadiliana na mtoto au watoto wako juu ya masuala haya? unasubiri akikua atajifunza mwenyewe "naturally" or as She/He go along in relationships"? OMG, by the time you realize, atakuwa ni "something else"!

Wasalaam!

Bazobonankira Bafakulelawamba
Tunawapa wazazi wakati mgumu sana kutazama/kusikiliza hili tangazo wakiwa na watoto wao..
Binafsi hili tangazo linalorushwa ITV na redio hasa RFA halina maadili, kuna ulazima gani wa kurusha sauti ya mwanamke akilalamika kwa sauti huku mwanamume akisikika kwa sauti ya kulazimisha kufanya mapenzi.

Kamalengo la tangazo hili ni kutoa uelewa juu ya unyanyasaji wa kijinsia, watoaji wa tangazo hili wamekosa namna nyingine ya kutoa ujumbe huu? Hivi hakuna tume ya maadili na malezi ambayo inaweza kudhibiti matangazo kama haya?

TAFAKARI!
 
Haya matangazo yanakuwa kero kwa sbb hawa wanaharaki huwa jikita ku campaign tu bila kuangalia mila na desturi za watu husika hizi fedha za wafadhili zinatudhilisha zinafanya kila kitu tufanye tu bila hata kuchambua!

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Swadakta ndg, yangu ifike wakati watu wajui vipaji nauwezo vinatofautiana sio ktk hilo tangazo
bali nimatangazo kibaotz haya maadili na pia kiwango kwamba kuna mtu kaajiriwa kwa nafasi hilo
mfano tangazo la m- pesa , serengeti la chiu no standard at all na mengine ya mapedi aaah
 
Mbona matangazo mengine mazuri wamejitaid lakin si ili kuna lile la mzee katiri anakaa kwenye siti ya gar kisha anampush mke wake, na lile jingne la watoto kujificha kabatin. Tatizo hapa ni tangazo limegusa sekta nyeti katika ndoa kile kitu cha tendo la ndoa kuongelea tu kweny Tv tayari tena kwa uwaz ambapo hata watoto wanaweza hisi kama sio kulielewa kabisa tangazo kunafanya watu tukose pozi kwa kweli.

Pia tangazo ilo lingekuwa kweny lugha mfano kingereza leo hakuna mtu angelalamika sana hapa. Wameshndwa kufichaficha ili lieleweke kwa wahusika tu mana saiz mpaka watoto wanalielewa vzuri sana.
 
Ni tatizo la serikali legelege. Enzi zile marehemu Remmy Ongala (RIP) alitunga wimbo wa mambo kwa soksi ukapigwa ban...leo kelele za mapenzi halafu kimya...tusishangae ikafuatia kuweka na picha. Ingekuwa kwa Mao tayari kituo kingekuwa kimefungiwa na uongozi mzima uko rumande. Kuzaliwa tz nako sio dili kabisa..inaudhi..inakera. yaani we acha tu!

Mkuu machozi yamenilengalenga kwa kunikumbusha dr Remmy Mtoro Ongala RIP. Ule wimbo wa mambo kwa soksi aliuvisha nguo na wenye umri wa kujua ni soksi ipi aliimaanisha ndio walifahamu, na kwa wengine iliendelea kuwa salamu na ikafiti kwa maudhui ya salamu. poleni kwa mlioliona hilo tangazo, Taarifa nyingi napata jf. Mambo kwa soksi
 
Wandugu,

Nimefatilia kwa makini mjadala huu lakini kikubwa kinacho onekana ni malalamiko tu pasipo kuweka wazi hoja ya msingi. Tunaposema tangazo halina maadili, tuna maanisha nini? Hivi, maadili yetu "watanzania" ni yapi hasa? Kihistoria, 'maadili ya mtanzania' imekuwa ni zaidi ya dhana ya kudhania na kufikirika tu. Hakuna mahala pamepata kuwekwa orodha ya "Haya Ndio Maadili Yetu". Yapo? Yaliwekwa na nani? Kwa maoni yangu, niko tayari kukosolewa kwa hoja sahihi, dhana ya "Maadili Yetu" imekuwa ikitumiwa vibaya na baadhi ya wenzetu, aidha viongozi, wanajamii wa kawaida ama makundi fulani fulani ili kuweza kulinda maslahi ya chochote kile ambacho wataona kuwa hakivutii utashi wao. na kisha kutaka kuaminisha umma mzima wa "watanzania" kuwa kile wasichokifurahia, basi hakistahili kwa umma uliobaki. Hii ni dhana potofu!

Pia tukirejea kwenye ma/tangazo husika, jamani, si linasema wazi kuwa "Kulazimisha mapenzi, hata kwa mke wako ni ukatili!"? Ina maana hatukubaliani na suala hili? Ama ni kwa kuwa tumekua tukiaminishwa kuwa ukiwa na mke unaweza kufanya naye mapenzi wakati wowote, sehemu yoyote hata kama yeye hajisikii hivyo? Sio sahihi jamani, vitendo hivi vimekuwepo, vipo, baadhi yetu wanavifanya na hawana budi kuviacha. Bila shaka, yawezekana ujumbe huu ukawa umegusa maslahi ya baadhi yetu na ndio maana yanatokea mayowe yote haya. Sioni ajabu wala soni eti kwa ujumbe huu kutolewa wakati umekaa aidha na wakwe, wajomba, shangazi, na wengineo, kwani na wao wote na vizazi vyao wanapaswa kulielewa hili na hata kuweza kuwaelimisha wengine. Mbona elimu ya ngono, afya ya uzazi, maambukizi ya VVU n.k inafundisha hata shule ya msingi? Ina maana hata wewe waogopa kujadiliana na mtoto au watoto wako juu ya masuala haya? unasubiri akikua atajifunza mwenyewe "naturally" or as She/He go along in relationships"? OMG, by the time you realize, atakuwa ni "something else"!

Wasalaam!

Bazobonankira Bafakulelawamba

Lazima utakuwa umekulia mazingira ya ngono ngono tena nje nje , haiwezekani kama wewe ni mtanzania huwezi jua maana ya maadili mema nini?
 
Back
Top Bottom