OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 428
Lile sakata la kada wa chama cha mapinduzi (CCM) Hussei Bashe kuenguliwa katika nafasi ya kugombea ubunge katika jimbo la Nzega mkoani Tabora kwa kisingizio kuwa si raia ,limechukua sura Mpya baada ya waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Lawrence Masha ,sasa kaandika barua rasmi kusisitiza kuwa ni rahia halali
Kwa mujibu wa barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho "'yah: upotoshwaji juu ya uraia wa wako:Masha anamuandikia Bashe akisisitiza juu ya uhalali wa uraia wake huku nakala zikipelekwa kwa katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na katibu Mkuu ,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba SAB.27/75/01/18, Masha alisisitiza kuwa tamko la uhalali wa uraia wa Bashe ,uliwahi kuthibitishwa katika barua ya wizara yake yenye kumbu kumbu namba DN 109758 ya Agosti mwaka huu,iliyoandikwa kupitia Idara ya Uhamiaji.
'' Kwa mara nyingine nachukua fursa hii kuthibitisha kwa mujibu wa kifungu namba 5(1) au 7(8)cha sheria ya urahia namba 7 ya mwaka 1995 wewe ni raia wa Tanzania wa kuzaliwa"Alisema
Kwa mujibu wa barua hiyo yenye kichwa cha habari kisemacho "'yah: upotoshwaji juu ya uraia wa wako:Masha anamuandikia Bashe akisisitiza juu ya uhalali wa uraia wake huku nakala zikipelekwa kwa katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba na katibu Mkuu ,Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Barua hiyo yenye kumbukumbu namba SAB.27/75/01/18, Masha alisisitiza kuwa tamko la uhalali wa uraia wa Bashe ,uliwahi kuthibitishwa katika barua ya wizara yake yenye kumbu kumbu namba DN 109758 ya Agosti mwaka huu,iliyoandikwa kupitia Idara ya Uhamiaji.
'' Kwa mara nyingine nachukua fursa hii kuthibitisha kwa mujibu wa kifungu namba 5(1) au 7(8)cha sheria ya urahia namba 7 ya mwaka 1995 wewe ni raia wa Tanzania wa kuzaliwa"Alisema