Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Baada ya mtifuano uliotokea hivi karibuni ambapo wanasiasa wakongwe nchini Joseph Butiku na Matei Qaresi kueleza udhaifu wa raisi kikwete katika uongozi wake kwa kushindwa kufanya maamuzi magumu,na baadae JK kudai kuwa atafanyia kazi yaliyozungumzwa na hatimaye kuwajibu wanasiasa hao.
Nimekuwa nikifikiria busara na hasa kwa JK kutaka kujibu hoja za akina Butiku badala ya kuona kuwa ana bahati watu wanamshika sikio kuwa gari analoendesha linaacha barabara na kuingia porini, sidhani kama ni sahihi kwa kwake kuanza kufanya majibizano. Nilidhani kma kiongozi wa nchi ashukuru kuwa wananchi wake wanafatilia uongozi wake kwa umakini na wako tayari kumuamsha usingizini pindi akilala wakati muda wa kulala bado.....Kuna ule msemo wa kichaa akikuvua taulo ukaanza kumkimbiza ukiwa uchi sijui watu watajua tofauti???...Ni mtazamo wangu tu.
Nimekuwa nikifikiria busara na hasa kwa JK kutaka kujibu hoja za akina Butiku badala ya kuona kuwa ana bahati watu wanamshika sikio kuwa gari analoendesha linaacha barabara na kuingia porini, sidhani kama ni sahihi kwa kwake kuanza kufanya majibizano. Nilidhani kma kiongozi wa nchi ashukuru kuwa wananchi wake wanafatilia uongozi wake kwa umakini na wako tayari kumuamsha usingizini pindi akilala wakati muda wa kulala bado.....Kuna ule msemo wa kichaa akikuvua taulo ukaanza kumkimbiza ukiwa uchi sijui watu watajua tofauti???...Ni mtazamo wangu tu.