Malunkwi
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 339
- 79
Baada ya Mbunge wa Bahi(CCM) kupandishwa kizimbani kwa kosa la kuomba rushwa ya Tsh8ml kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mkuranga, Mjumbe wa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa Bw.Iddi Azan alizungumza kwa niaba ya Kamati kuwa swala la rushwa kwa mbunge huyo ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo ni lake binafsi na si la kamati. Ushahidi wa kimazingira unaonesha kuwa Badwel aliomba fedha hizo za rushwa ili akagawane na wajumbe wenzake wa kamati yake kwa madhumuni ya kupitisha hesabu za halmashauri husika, kumbe picha tunayoipata hapa ni kuwa hesabu hizo huwa hazipitishwi bila wajumbe wa kamati kuhongwa
Suala hili limekuwa likienda hadi kwenye zoezi la uandaaji wa bajeti za Idara mbalimbali za serikali na hatimaye bajeti nzima ya nchi kwani mwaka jana tulishuhudia aliyekuwa katibu mkuu wa wizara ya nishati na madini Bw. David Jairo akichangisha fedha kutoka ktk idara zilizo chini ya wizara yake ili kufaninisha zoezi la bajeti. Lengo likiwa ni kupata fedha kwa ajili yha kuwahonga wajumbe wa kamati ili wapitishe Bajeti ya wizara husika.
My take: Azan aache kumbebesha zigo la kamati Badwel kwakuwa utaratibu huo unaonekana kuwepo miaka mingi na ndiyo Culture ya utawala uliopo madarakani na ndiyo maana wabunge wamekuwa wakipigana vikumbo kupata huo ujumbe wa hizo kamati zao huko bungeni.