X wangu anataka nikutane nae!

Mkuu ulishawahi kumtafuna kama ndio msikilize anataka nini akisema anarudisha mapenzi kimbia.Ila kama hukuwahi kumtafuna basi fanya mambo halafu kimbia.
 
Female crime uliyocommit ni kumsomesha kaka.mara zote wanawatosaga wanaowasomesha.labda anataka umtafutie kazi halafu akupige kibuti tena
 
Lol! I love jf, kipimo cha akili yako ndo majibu utakayopata!

Naongezea kaka, uende na gf wako wa sasa ili mshauriane chuo cha kumsomeshea, she might know better. Lol
kaka kamsikilize huwezi jua labda anataka mrudiane tena ili umsomeshe masters alafu akutose tena
 
Cha msingi ni kwamba usikatae wito ILA usikubali ukutane nae nyumbani kwako,tafuta open area mkutane hapo umsikilize anachosema.kukutana nyumbani ni hatari you never know bwana ninyi ni jinsia tofauti,na ni muda mrefu umepita hali sasa hivi sio nzuri,usije shawishika. Ila kama anataka arudi tena kwako usikubali,hakupendi huyo mwanamke,kwa vyovyote vile kama atataka kurudi kwako ni kwa kuwa yatakuwa yameshinda.
 
Binti atakuwa anajiamini na anahisi kuwa baada kukuacha,wewe umepagawa maana ulimpenda sana huna hamu tena ya kupenda na kuanza upya,anajiamini akiwa karibu na ww utabadili mawazo,muendelee na umsamehe!!kosa kubwa sana hapo!!maana yeye pia amedoda huko aliko ndio maana anakutafuta!!nakushauri ukae nae mbali maisha yamemfua labda wewe kidogo uko vizuri ndio anajuta na kutubu!!!kazi ni kwako!!!!
 
Kubali appointment yake mpeleke kwenye restaurant ya gharama ya kawaida then ukifika mwambie awe huru kutumia chochote atakacho wewe tumia maji yanatosha then ukikaa nae kidogo fanya mchakato mtoroke bill iwe juu yake.usimuonee huruma mkuu mi nilishamfanyia m1 hadi leo akiniona heshima depe wanapenda kula vya bure,then tafuta msichana mwingne mkali zaidi yake .dawa ya mwanamke ni mwanamke mwanzake
dah we noma.
 
Hapo pekundu na hasa kwenye mstari ni jibu tosha kwamba unapaswa wewe mwenyewe uzingatie hayo.
1. alikuambia yeye shida yake kwako ilikuwa ni mali yako na hakuwahi na wala hakupendi.
2. Alikukashfu sana.

Mimi binafsi, ni kwamba katika yote fanya lkn suala la kunikashfu ni fedheha sana. Hivyo, nakupa pole sana kwa yaliyokukukuta. Ulijinyima kwa kiasi kidogo ulichokuwa nacho badala ya kuwasaidia ndugu zako au kufanya mambo ya maendeleo, lkn kwasababu ulisikumwa na upendo kwa huyo dada ulijinyima kwa vyote ili afanikiwe kufikia malengo yake. Si ajabu hata wewe labda hayo mafanikio ya elimu haukujaliwa kama ulivyomfanikisha (samahani kama nitakuwa nimekukwaza hapa, lkn ni hasira ya kutokana na alivyokutenda huyo dada). Lkn katika yote mwishowe ulikuja kuambulia Fedhea na si ajabu hata matusi ya nguoni.


Ndugu yangu, mimi nakuambia jibu moja tu kwamba huyo dada HAKUWAHI KUKUPENDA NA HATATOKEA KUKUPENDA, lkn sasa mambo yake hayajanyooka na anakumbuka ulivyojitoa kile kipindi anasoma, hivyo anaamini kwamba utampokea tu.Hivyo mimi nakupa ushauri ufuatao,
1. Kamwe usionane naye, kwani hakuwahi kukuhitaji na kama anakuhitaji sasa ni kwasababu kakwama au katoswa na sasa kwako ndiyo pakumalizia stress na matatizo yake.
2. Na kama utaamua kuonana naye, jitahidi sana isiwe kwako unapohishi.
3. Kuwa na tahadharii zaidi, kwani si ajabu ana matatizo hata ya kiafya anataka akugawie. Hili likitokea itakuumiza zaidi, kwani itakutonesha kidonda ambacho kilishaanza kupona.
4. Kuwa na msimamo kama mwanaume na usikubali kurudi nyuma,kwani kuna hatari mabo yake yakishamnyokea ATAKUMWAGA TENA:

hii nimeipenda sana kaka,asante sana kwa ushauri
 
hahahaaa! hanipati tena
Usiseme hivyo mkuu.....nadhani wewe bado hujawaelewa vizuri hawa viumbe......wanaweza hata kusababisha baraza la mawaziri kuvunjwa... kwa kifupi kama ulikuwa na furaha ulivyokuwa naye basi mrudie upesi....haya mambo huwa hayana ushauri sana kutoka kwa watu wengine.... cha msingi ni kujiuliza mwenyewe kwamba una furaha au la....kisha unajiamulia.....basi.....isije siku moja ikawa bahati mbaya mkakutana na sister halafu ukamwambia " huyu ndiyo alitaka kunishauri nikuteme"......ha ha ha
 
we mshamba nini onana nae ujue anataka kukueleza nini alafu pia unavyosema hivyo inamaanisha wewe mwenyewe hujiamini inaonyesha kuwa bado unampenda so kuwa muwazi kama bado unampenda na yeye anakutafuta sasa hivi maana hana kazi hivyo anataka apatekazi akutose tena so kazi kwako kama alishakuchana live kuwa alikuwa hakupendi wakat anasoma sasa tegemea pia atakuchana live kuwa alikuwa hakupendi yeye kashakugeuza kuwa wewe ni mtafutaji wake tuu wa vitu
 
Anataka kukutumia tena umsomeshe "masters" yake, achana nae mjomba, achana nae


Sent from my NOKIA 3310 using Tapatalk HD
 
Nahis kama bado unampenda hadi sasa na ndio maana unakosa uamuzi wa kumsikiliza au kutomsikiliza.
Kaa chini usikilize moyo wako, ila kama bado una hamu nae nenda tu kamsikilize anachotaka kusema kwani huyo anataka tu kukuomba msamaha mrudiane. Kama humhitaji tena mtolee nje hata kumsikiliza usiende!!
 
Back
Top Bottom