Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,438
- 1,026
Jamaa mmoja anaishi mji kasoro bahari[morogoro].Huyu bwana ni driver wa magari ya kusafirisha mafuta ya kampuni moja maarufu hapa nchini.Huyu jamaa anaishi pamoja na mama yake ambaye ni mjane baada ya kufiwa na mumewe.Lakini kuna jambo limezuka,huyu mama ameunda uhusiano wa kimapenzi na rafiki wa karibu wa mshikaji.Kibaya zaidi,jamaa anadiriki kutangaza kitaa vile anavyomtenda mama wa rafiki yake.Hizi habari zilimfikia jamaa,akaamua kumuuliza bi mkubwa kuhusu hili suala,cha ajabu mama alikuwa mkali.Alimng'akia mshikaji na kumwambia hana jipya la kumfundisha katika maisha haya,yeye ni mtoto na atabaki kuwa mtoto wake,'kama hutaki kunitunza,basi nirudishe kijijini',alisema mama huyo.Kiufupi jamaa kabaki x-road!