HABARI ZENU WANAJAMII WENZANGU
.
Naombeni nafasi nami niwasilishe hoja hii ndani ya jukwaa hili la elimu lenye heshima kubwa ..
Leo nilikuwa maeneo ya ofisi za TCU hapa jijini Dar es Salaam, nilikuwa najaribu kudodosa dodosa kulikoni mbona kimya kimetanda kuhusu hawa wenzetu ambao waliomba second selection na wengine kuandikiwa wamechaguliwa chuo fulani ila unapoingia kwenye chuo husika hukuti jina, wahusika majibu waliyokuwa wakitupa ni kwamba tuwe wavumilivu kila kitu kitakuwa kwenye mtandao hivi karibuni ..
Wanafunzi ambao walikuwa ofisini hapo hawakukubaliana na majibu hayo ndipo ikatokea kama songombingo la aina yake baada ya hapo muhusika alituliza vurugu zilizotaka kutokea na ndipo mwanafunzi mmoja wa chuo cha Mount Meru ambaye alichaguliwa second selection alipotaka kujua zaidi suala hili majibu yalibaki yale yale ya kuwa wavumilivu ila muhusika alichosema ni kwamba kwa wale ambao vyuo vyao vinafunguliwa mwezi huu wa tisa waende wasiwe na hofu kwani taarifa zao zimeshafikishwa katika vyuo husika walivyo omba na kukubaliwa hapa ndipo mwanafunzi mwingine alipotaka kujua zaidi kuhusu mikopo huku akiwa na jazba na muhusika naye akajibu huku akiwa na jazba akasema kwamba : MLIOMBA MIKOPO WOTE MTAPATA IWAPO TU KWENYE COURSE ULIYOOMBEA MKOPO ILIRUHUSU WEWE UPATE MKOPO KUTOKA BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU NA KIWANGO CHA MKOPO PIA KINAPATIKANA KWENYE KILE KITABU CHA TCU AMBACHO KIMEONESHA KILA COURSE NA KIWANGO CHA MKOPO KINACHOTAKIWA KULIPWA NA HESLB NA SI VINGINEVYO hivyo aliwashauri wote ambao wanatakiwa kuanza chuo mapema mwezi huu waende kama ratiba ya chuo husika itakavyoeleza kuhusu maelekezo mengine watapewa watakapo fika huko chuoni waliko chaguliwa .
Baada ya hapo nilijiongeza nikajiuliza inamaana majina kutoka HESLB ndio hayototoka tena au hii kauli ya muhusika ina maana gani .Ndipo nilipo ianza safari ya kwenda ofisi za HESLB ili kupata dodoso za mikopo yetu,, majibu niliyopata kutoka katika ofisi za HESLB ni kwamba iwapo TCU watatoa majina ya waliopata vyuo RASMI basi nao hawatokuwa na pingamizi kutoa majina ya wanafunzi waliopata mkopo Niliona labda hawaelewi kama kuhusu TCU wao wamesha toa majina ya wanafunzi ambao wamepata vyuo, nilipo mkumbusha hilo nae akaniuliza hizo taarifa nimezipata wapi? Nikamjibu zipo kwenye profile zetu ambazo tuliombea vyuo.. Nae akanijibu hiyo siyo RASMI , RASMI WANAYOITAKA HAPA NI KWAMBA LAZIMA HAYO MAJINA YAONEKANE KWENYE WEBSITE YA TCU HIVYO HANA JIBU LINGINE ZAIDI YA HAPO .
Mzee wa dodoso nikaishia hapo hivyo tuendelee kuwa wavumilivu kuhusu HESLB na kuhusu hawa wenzetu ambao wanatakiwa kwenda chuo mwezi huu ushauri wangu ni kwamba kama umejipanga kidogo kiuchumi we nenda tu kwenye chuo husika angalau wakuone wasije wakajua umegoma bure kasha wakakufuta kwenye chaguzi zao wengine tupige goti tusali baba HESLB acheke mapema maana tumejitahidi kumchekesha lakini bado tu amenuna .
***********************ASANTENA WANA JF*******************
Naombeni nafasi nami niwasilishe hoja hii ndani ya jukwaa hili la elimu lenye heshima kubwa ..
Leo nilikuwa maeneo ya ofisi za TCU hapa jijini Dar es Salaam, nilikuwa najaribu kudodosa dodosa kulikoni mbona kimya kimetanda kuhusu hawa wenzetu ambao waliomba second selection na wengine kuandikiwa wamechaguliwa chuo fulani ila unapoingia kwenye chuo husika hukuti jina, wahusika majibu waliyokuwa wakitupa ni kwamba tuwe wavumilivu kila kitu kitakuwa kwenye mtandao hivi karibuni ..
Wanafunzi ambao walikuwa ofisini hapo hawakukubaliana na majibu hayo ndipo ikatokea kama songombingo la aina yake baada ya hapo muhusika alituliza vurugu zilizotaka kutokea na ndipo mwanafunzi mmoja wa chuo cha Mount Meru ambaye alichaguliwa second selection alipotaka kujua zaidi suala hili majibu yalibaki yale yale ya kuwa wavumilivu ila muhusika alichosema ni kwamba kwa wale ambao vyuo vyao vinafunguliwa mwezi huu wa tisa waende wasiwe na hofu kwani taarifa zao zimeshafikishwa katika vyuo husika walivyo omba na kukubaliwa hapa ndipo mwanafunzi mwingine alipotaka kujua zaidi kuhusu mikopo huku akiwa na jazba na muhusika naye akajibu huku akiwa na jazba akasema kwamba : MLIOMBA MIKOPO WOTE MTAPATA IWAPO TU KWENYE COURSE ULIYOOMBEA MKOPO ILIRUHUSU WEWE UPATE MKOPO KUTOKA BODI YA MIKOPO YA ELIMU YA JUU NA KIWANGO CHA MKOPO PIA KINAPATIKANA KWENYE KILE KITABU CHA TCU AMBACHO KIMEONESHA KILA COURSE NA KIWANGO CHA MKOPO KINACHOTAKIWA KULIPWA NA HESLB NA SI VINGINEVYO hivyo aliwashauri wote ambao wanatakiwa kuanza chuo mapema mwezi huu waende kama ratiba ya chuo husika itakavyoeleza kuhusu maelekezo mengine watapewa watakapo fika huko chuoni waliko chaguliwa .
Baada ya hapo nilijiongeza nikajiuliza inamaana majina kutoka HESLB ndio hayototoka tena au hii kauli ya muhusika ina maana gani .Ndipo nilipo ianza safari ya kwenda ofisi za HESLB ili kupata dodoso za mikopo yetu,, majibu niliyopata kutoka katika ofisi za HESLB ni kwamba iwapo TCU watatoa majina ya waliopata vyuo RASMI basi nao hawatokuwa na pingamizi kutoa majina ya wanafunzi waliopata mkopo Niliona labda hawaelewi kama kuhusu TCU wao wamesha toa majina ya wanafunzi ambao wamepata vyuo, nilipo mkumbusha hilo nae akaniuliza hizo taarifa nimezipata wapi? Nikamjibu zipo kwenye profile zetu ambazo tuliombea vyuo.. Nae akanijibu hiyo siyo RASMI , RASMI WANAYOITAKA HAPA NI KWAMBA LAZIMA HAYO MAJINA YAONEKANE KWENYE WEBSITE YA TCU HIVYO HANA JIBU LINGINE ZAIDI YA HAPO .
Mzee wa dodoso nikaishia hapo hivyo tuendelee kuwa wavumilivu kuhusu HESLB na kuhusu hawa wenzetu ambao wanatakiwa kwenda chuo mwezi huu ushauri wangu ni kwamba kama umejipanga kidogo kiuchumi we nenda tu kwenye chuo husika angalau wakuone wasije wakajua umegoma bure kasha wakakufuta kwenye chaguzi zao wengine tupige goti tusali baba HESLB acheke mapema maana tumejitahidi kumchekesha lakini bado tu amenuna .
***********************ASANTENA WANA JF*******************