Chenge
JF-Expert Member
- Oct 5, 2011
- 1,073
- 377
Habari zenye ukweli 100% ambazo blog hi imezinyaka zinasomeka kuwa Wolper anayejulikana kama Amber Rose wa Bongo amenyanganywa mkoko huo aina ya BMW X6 wenye thamani ya ngawira za kibongo ML 170, sambamba na kupigwa stop kukaribiana na mshefa aliyekuwa amemnunulia ndinga hiyo.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, hatua ya mshefa huyo kuamua kuchukua ndinga yake ni baada ya kugundua kuwa Wolper anatoka kimapenzi na sharobaro mmoja anayemiliki duka maarufu la viwalo pande za Kinondoni.
Aidha chanzo hicho, kimeieleza blog hii kuwa hivi sasa mwanadada huyo ameamua kutembelea ndinga aina ya Noah aliyokuwa anaitumia hapo awali sambamba na kutoka kwa kuvizia kukwepa watu wake wa karibu washitukie mchongo.
Katika kuhakikisha kuwa ukweli unajulikana blog hii iliamua kumsaka na baada ya kupatikana Wolper aligeuka mbongo na kudai kuwa hakuna jambo kama hilo isipokuwa kilichotokea ni kuwa gari limepata matatizo na ameamua kulipeleka garage.
Alipotakiwa kueleza kuwa imekuwaje gari mpya kama ile aipeleke garage tene kwa siku tatu Wolper alisme hivi:
Bwana eeh wee jua liko garage hayo maswali mengine mimi sitaki kuayasikia na kama una taka ugomvi endelea kuniuliza alisema na kuondoka haraka eneo alilokuwa amekaa