Woga Umetudumaza Kifikra Watanzania!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757
Kati ya mambo yanayoweza kumdumaza binadamu kwenye medani ya kujiendeleza na nchi kukua ni woga. Woga umewafanya watanzania kuwa watumwa kwenye nchi yao kwa kutawala mioyo na fikra za wananchi walio wengi kwa kiwango cha kutisha.

Hali ya woga imetanda kama wingu machoni mwetu kiasi cha kutoweza kuona na kuwa na mkakati wowote wa kujinasuru na jinamizi la ujinga na umasikini. Woga unatufanya tusiwe na ubavu wa kupambana na uovu miongoni mwetu kwa kujificha nyuma ya pazia hewa tunayoibatiza bila aibu kuwa ni amani na utulivu.

Woga umetulemaza kiakili kiasi cha kutoweza kufikiria njia mbadala ya kuondokana na serikali za kiimla na kibabe. Woga unalitafuna taifa na kuna hatari kuwa hali ikiendelea hivyo Taifa litaangamia. Kwa nini natamka mambo mazito kama haya na huo woga ni upi ?

Woga uliowafanya watanzania zaidi ya asilimia 80% wapige kura kukataa vyama vingi kwa kuogopa vurugu na vita na mpaka sasa kuna wanaoamini hivyo. Huu ni woga unaoletwa na ujinga.

Woga unaowafanya wananchi kuwa na imani na Rais aliyechaguliwa kwa idadi ya wapiga kura karibu 80% kusita kuchukua hatua madhubuti kupambana na uovu. Woga huu ni utii uliokubuhu (sycophancy).

Woga unaomfanya mbunge ashindwe kutetea maslahi ya wananchi waliomchagua awawakilishe kwa kuogopa kukaripiwa na chama chake cha siasa. Woga huu ni unafiki na ulafi.

Woga unaowafanya wananchi kwa wingi wao wakaridhika na tamko la serikali hadharani kuwa inawaogopa wenye pesa kwa kuwa wana nguvu ya kuiyumbisha nchi . Woga huu nauita uzembe.

Woga unaowafanya wananchi wasione umuhimu wa Raisi kuwajibika anapovurunda mambo ati hii kwa siasa ya bongo haiwezekani. Raisi ni binadamu tu wa kawaida na lazima awajibishwe akikoroga. Woga huu ni ukondoo.

Woga unaomfanya mwananchi aogope kuwalaumu na kuona mapungufu ya walio madarakani lakini yuko tayari kuwanyoshea kidole wapinzani wanaojaribu kutetea maslahi yake. Woga huu ni ukwepaji wa uwajibikaji.

Wananchi kuwapokea mafisadi wanaojiuzulu kwa vifijo na nderemo kunaelezea woga kwa wenye vijisenti. Huu woga hata hivyo unajificha ndani ya ukabila na hata hili hatuna ujasiri wa kuukemea.

Woga unaoifanya serikali kuchukua hatua za zimamoto kwa mambo yanayohitaji maamuzi makini ili kuwafurahisha wahisani. Bila shaka huu ni zaidi ya utumwa - ni usanii.

Woga wa kutoifikiria Tanzania bila CCM au kuisubiri imeguka ndio ati upinzani wa kweli upatikane. Huu ni uelemavu wa kiakili.

Je tufanye nini:
Huu si muda tena wa kukubali kuendelea kupumbazwa, kuzugwa na kudanganywa. Hata paka huweza kukimbizwa lakini akafikia mahali hana usalama tena na njia pekee ni kumparua mtu. Hivyo huu si muda tena wa kuendelea kulipalilia hili shamba la woga na kuliacha linastawi.

Hapana, serikali hii ya kisanii lazima iachie madaraka na isiachiwe nafasi hata ya kupumua kama haitafanya hivyo. Huu si wakati wa kupeana hongera bali kuongeza jitihada za kumtoa nyoka pangoni. Kilichoziba njia yetu kuelekea maendeleo ya kweli ni woga wetu tu ambao unatufanya kuwa wanyonge.

Tusichoweza kukifanya tusikiruhusu kuwa kisiki na kuzuia tunachoweza kukifanya kwa kuwa uwezo tunao, nia tunayo na sasa hivi kuliko wakati wowote mwingine sababu tosha kabisa tunayo.
 
Woga woga woga umetufikisha hapa tulipo. Kiongozi anaiba tunaogopa kumwambia...... Mwenyekiti wa mtaa ana Embezzle funds za mtaa au kijiji tunaogopa kusema.........Meneja wa shirika au kampuni ana embezzle funds kila mmoja anaona si shida..... tunaogopa kusema.... tunaona yeye ndiye mjanja na tunampigia makofi tukimsifu kuwa ni mtu mwenye pesa nyingi si mchezo!

Rais anajiuzia shirika la serikali kwa bei poa tunaogopa kusema.........tunasubiri hadi atoke madarakani..... kila kitu tunaogopa kusema. Unatakiwa uwaambie ukweli wanakijiji kwamba serikali imejaa wizi........ unaogopa......
Unatakiwa ugawe kijarida cha cheche za fikra kwa wananchi ili wajue ukweli ni nini na propaganda ni nini..... unaogopa......

Tumeogopa weeeeeeeeeee hadi tumefikia tulipo. Tunahitaji ujasiri na kutupa uoga pembeni. Tuwe tayari kubeba maumivu toka hata kwa vyombo vya usalama ili turejeshe utulivu wa kweli katika nchi yetu na si huu utulivu unaoimbwa wakati haupo maana nchi imejaa uoza unaoondoa amani na utulivu.

Miaka minne nyuma Mramba alisema ni bora tule majani na viongozi wenzie hawa hawa walikuwa wanampigia makofi huku wakijua si sawa ila sababu ya uoga. Leo tuko hapa na sijui kama hasara hiyo tutai recover vipi hata akishindwa kesi yake maana vijisenti anavyo huko majuu.

Penye ukweli tutasema ukweli bila kuogopa. Na tuanze kuwa wakweli kuanzia ngazi ya chini.

MF
 
Hii ni KANSA inayolitafuna taifa letu taratiibu.
Na usopukuwa mwoga unageuka kikwazo kwa walio wengi kiasi cha kutishiwa maisha!
Hivi ni lini tutaacha woga na kuwa tayari kufa kwa ajili ya kusamamia ukweli na rasilimali na taifa letu?
Je WOGA huu unasababishwa na kutokujua haki zetu (wananchi)?
 
Mag3, mara zote huwa sipendezwi hata kidogo namna watu wanavyozungumzia "woga wa watanzania" kwa kujaribu kueleza kuwa ndiyo sababu ya kukwama kwetu, hasa pale "watanzania" wanapowekwa kwenye kundi moja. Why single out FEAR as the problem; cos to me it looks as if it is the only problem.

Nimekuwa mgumu kukubali kwamba woga ni moja ya tatizo kubwa linaloisumbua Tanzania. Baada ya kusoma hoja yako, nimeona kuna haja ya kugawa watanzania katika makundi, halafu tuone wangapi ni waoga na wangapi kinachowakwaza sio woga.

Nionavyo mimi, kuhusu woga, nakubali kwamba kuna asilimia kama 20 hivi ya watanzania tuna ugonjwa huu wa woga (wasomi walio wengi, wafanyabiashara wakubwa na wa kati, members wa JF - hasa waishio mijini, etc).

Kuna kundi lingine, hawa ujinga ndiyo ugonjwa au kizingiti kikubwa hata kupelekea mchango wao kuwa mdogo sana kwa sasa. Wenzangu mnaonaje, ninyi mnaona makundi mangapi?



Woga wa kutoifikiria Tanzania bila CCM au kuisubiri imeguka ndio ati upinzani wa kweli upatikane. Huu ni uelemavu wa kiakili.
 
Hii ni KANSA inayolitafuna taifa letu taratiibu.
Na usopukuwa mwoga unageuka kikwazo kwa walio wengi kiasi cha kutishiwa maisha!
Hivi ni lini tutaacha woga na kuwa tayari kufa kwa ajili ya kusamamia ukweli na rasilimali na taifa letu?
Je WOGA huu unasababishwa na kutokujua haki zetu (wananchi)?

Woga wa wananchi unachochea kiburi cha serikali iliyoko madarakani kwa kuiachia ishike mpini wananchi wakikamata makali. Kwa kawaida kwenye nchi zenye uelewa serikali kama mwajiriwa ndiyo inapaswa kumwogopa mwananchi ambaye ndiye mwajiri wake. Tuliogopa kudai mabadiliko wakati wa Marehemu Mwalimu mpaka alipoamua kwa hiari yake kuachia madaraka na bado nchi iliweza kuwapo bila Mwalimu. Woga ulitaka kujipenyeza mwaka 1994 kwa baadhi ya wananchi kutaka Mwinyi aongezewe kipindi kingine, kwa bahati Mwalimu aliyekuwa bado hai aliweza kulivalia njuga hii hoja na ikafa kifo cha mende. Hivi mtu mmoja alikuwa na sauti kiasi gani ikilinganishwa na sauti za watu milioni 40 !!!.

Tulishuhudia historia kama hiyo ikijitokeza kwa Salmin Amour na mwaka 2004 woga wa Tanzania bila Mkapa nao ukaibuka tena - woga wa mabadiliko unatutafuna. Wananchi wanatakiwa kumheshimu Raisi wao na kamwe si kumwogopa na akishindwa kutimiza wajibu wake heshima hiyo hupotea na hatufai tena. Serikali inayodumu kiujanja ujanja kwa uwongo na kuitumbukiza nchi katika mikataba isiyoweka mbele maslahi ya wananchi wake ni mufilisi. Serikali inayochukua nafasi kama ya mtazamaji hali huduma muhimu kwa wananchi zikizidi kudorora ni haki kung'olewa madarakani bila chembe ya huruma. Tanzania yenye heri yawezekana bila Kikwete wala CCM na katika hili wengine katu hatunyamazi - tuachane na woga, period.
 
- I beg to differ, sisi wa-Tanzania ni wajinga wa elimu ya siasa na besides Upinzani hawajatupa sababu ya kutopigia kura CCM,

Zitto, Dr. Slaaa, na Ndesamburo walichaguliwa na nani? Wananchi waoga au wenye elimu ya juu kisiasa?

- Tunalaumu mno mpaka tunaishiwa hoja za malalamiko. Katika maisha kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, kwa wa-Tanzania huu sasa ni wakati wa kushirikiana na serikali kutafuta ushahidi wa kuwatokomeza mafisadi kisheria, serikali imeanza sisi ni kufuatia tukiongozwa na uzalendo wa taifa letu, bila kujali anayetuongoza ni CCM au Upinzani, taifa mbele shime wananchi tuhsirikiane sasa tushikamane kama tulivyofundishwa na baba wa taifa letu Mwalimu Nyerere.

Umoja ni Nguvu, utengano ni udhaifu.
 
- I beg to differ, sisi wa-Tanzania ni wajinga wa elimu ya siasa na besides Upinzani hawajatupa sababu ya kutopigia kura CCM,

Zitto, Dr. Slaaa, na Ndesamburo walichaguliwa na nani? Wananchi waoga au wenye elimu ya juu kisiasa?

- Tunalaumu mno mpaka tunaishiwa hoja za malalamiko. Katika maisha kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, kwa wa-Tanzania huu sasa ni wakati wa kushirikiana na serikali kutafuta ushahidi wa kuwatokomeza mafisadi kisheria, serikali imeanza sisi ni kufuatia tukiongozwa na uzalendo wa taifa letu, bila kujali anayetuongoza ni CCM au Upinzani, taifa mbele shime wananchi tuhsirikiane sasa tushikamane kama tulivyofundishwa na baba wa taifa letu Mwalimu Nyerere.

Umoja ni Nguvu, utengano ni udhaifu.

Marshall:

Nakubaliana na wewe kimsingi. Hili suala ya kuwa watanzania ni woga sioni kuwa lina umuhimu wake.

Wakati nchi ina matatizo ya ajira kitu cha kwanza nilichukua visa na kuja kuishi Marekani.

Kuna matatizo ya shule za serikali, kila mwenye nacho anapeleka mtoto kwenye shule za kulipia zingine zikiwa Kenya.

Kuna matatizo ya maji kila mwenye uwezo ananunua simtank.

Kuna matatizo umeme mwenye uwezo ananunua generator.

Kuna matatizo ya barabara mbovu mwenye uwezo ananunua SUV.

Kuna uhaba wa sukari, watu watakunywa uji wa chumvi.

Kuna uhaba wa bia, watu watakunywa chibuku.

Hatuwezi kujenga nchi kwa kutafuta ufumbuzi wa binafsi kwenye masuala yanayotakiwa masuala ya jumla.
 
..ni waoga na wavivu tuu na hawajitumi kwa chochote,unaweza kupita sehemu na mtaa ni mchafu ile mbaya lakini wananchi wanaoishi karibu hawawezi hata kujipanga wakashirikiana wakasafisha mtaa wao na kuziba madimbwi machafu kuzuia mbu karibu na milango yao madai yao eti sio kazi yao,can you imagine sehemu kama chuo kikuu walikuwa wanakosa maji huku engineers wote wa nchi wamejaa hapo...aibu kubwa sana,shule kama ya Pugu yenye wanafunzi karibu 1000 na community kubwa ya walimu na wafanyakazi haina maji kwa karibu miaka 20 na haina hata vyoo wameshindwa kujisaidia kuondoa hilo tatizo? kama sio uzembe,uvivu,uwoga wa kufanya mambo makubwa na akili ndogo ni nini?
 
Woga na hisia zote zinazoendana nazo ni hatarishi kwa usatawi wa mtanzania kuliko tunavyoona.

Soma kipande kidogo cha makala hii ya : Ni ujinga wa kiutu na si Kiakili. From Duniahai - Home

Ni ujinga kujitolea nafsi zetu kuondoa maadui umasikini, ujinga, maradhi, na dhuluma(ufisadi) kwa kutumia silaha ya woga, wasiwasi, mashaka, ubinafsi na hisia hasi zote zanamna hiyo.

Hisia hizi hazijawahi kutumika kama silaha na kuleta ushindi zaidi ya
kumjenga adui na hata kujikuta akisujudiwa na kutumikiwa. Hisia hasi sio kinga wala siosilaha popote!

Uko ushahidi kuthibitisha kuwa maadui hao wa nne waliogunduliwa tangu enzi ya kuasisiwa taifa hili wana rutubishwa, kudumishwa na kuendelezwa na nguvu ya hisia zetu ambazo ni hasi kiutu na kibinadamu. Nguvu ambayo anaizalisha askari yuleyule aliye vitani kupambana na maadui hao wa maendeleo, afya na ustawi wa jamii.

Utu ni utambuzi uliopevuka dhidi ya mkondo wa hisia hasi. Rasilimali Utu ni uwezo wakumomonyoa ubinafsi wa hisia hasi na kusitiri heshima, imani, upendo na matumainiambazo ni nguzo kuu za maadili ya ubinadamu dhidi ya unyama au Utu hasi.

Hivyowerevu wa kina dhidi ya hisia hizi angamizi kwa Utu ndio unaotafsiriwa kama kuerevukana kueleimika Kiutu (emotional intelligence: EI); ni kufuta ujinga Kiutu. Hii ni tofauti nawerevu wa kiakili (intelligence quotient: IQ)

Kutoelimika juu ya dhana nzima ya Utu na sheria za mfumo mzima wa hisia hasi kwenyeustawi wa jamii, ni ujinga wa Kiutu unaozidi ujinga wa kiakili katika nafasi hiyohiyo.Ukweli na ugunduzi unaoedelea kumiminika duniani kote kwa takribani miaka 10-15 hivi unadhihirisha kuwa ujinga wa kutokuelimika kuhusu hisia hasi dhidi ya Utu wetu unaigharimu dunia matatizo sugu kwa kiwango kikubwa licha ya kuwa wanadamu wa leowameelimika kiakili kuliko wakati mwingine wowote.

Kwa mfano ufisadi na dhuluma kwenye jamii: Ni kosa la kijinga na lisilosamehekakukabiliana na adui fisadi kwa kutumia woga, wasiwasi,mashaka, ubinafsi na hisia hasinyingine zote.

Fisadi aliyefuzu kikamilifu somo la ufisadi darasani alielimishwa
kinaganaga nguvu na mamlaka iliyobebwa na hisia hizi. Jukumu lake la msingi ni jinsi yakuichochea na kuivuna kwa kiasi cha kutosha ili kukamilisha dhuluma yake kwa jamiiatakayoiteka, kuitumikisha na kuitawala.

Fisadi mdhulumu anatumia ujinga wa jamii kutokujua kanuni kuu mbili za hisia na Utuhasi. Jamii haina werevu kuwa hisia hasi kama nguvu imebeba mamlaka ya usumaku kwakile kilichoichochea kutokea. Na pia jamii imelala usingizi mzito, haina utambuzi kuwahisia hasi ina uwezo wa kumpumbazisha (hypnotic emotions) muadhirika kuliko vilevivyote duniani ukiviweka pamoja.

Fisadi anachukua fursa ya ujinga huu kuwapumbazishawanajamii na kuwatumia kama kitoweo. Anawatawala na kuwadhulumu haki zao hata kama wameerevuka kiakili lakini wajinga kiutu.Katika adhma yake ya kuudhulumu umma, adui

Malizia makala hii: Ni ujinga wa kiutu na si kiakili kwenye pdf ya Duniahai - Home

au: http://www.duniahai.com/Articles/Ni ujinga wa kiutu si wa ki akili.pdf
 
Marshall:

Nakubaliana na wewe kimsingi. Hili suala ya kuwa watanzania ni woga sioni kuwa lina umuhimu wake.

Kuna matatizo ya shule za serikali, kila mwenye nacho anapeleka mtoto kwenye shule za kulipia zingine zikiwa Kenya.

Kuna matatizo ya maji kila mwenye uwezo ananunua simtank.

Kuna matatizo umeme mwenye uwezo ananunua generator.

Kuna matatizo ya barabara mbovu mwenye uwezo ananunua SUV.

Kuna uhaba wa sukari, watu watakunywa uji wa chumvi.

Hatuwezi kujenga nchi kwa kutafuta ufumbuzi wa binafsi kwenye masuala yanayotakiwa masuala ya jumla.

Chief Zakumi, bado unaamini katika hayo uliyoyaandika?

Kama ndiyo,napingana nawe. Kwani katika hayo yote uliyoyasema juu ya utatuzi wa matatizo ya jamii katika mitizamo ya kibinafsi,lawama bado zinarudi kwetu sisi watanzania kwa kuendelea kuwa waoga na wazito wa kutaka kuiwajibisha na kuishurutisha serikali itatue matatizo hayo ili utatuzi huo uweze kuleta tija kwa mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Uwoga wetu ndiyo umepelekea kukubaliana na mipango ya isiyo endelevu ya serikali katika elimu -hususani shule za kata,mikopo katika vyuo vikuu,mitaala ya elimu n.k. - mipango isiyolenga kumwezesha mtoto wa kitanzania apate elimu itakayomwezesha aweze kukabiliana na matatizo yanayomzunguka yeye na taifa kwa ujumla.

Ni uwoga wetu pia wa kuziwajibisha serikali za CCM,ndiyo umepelekea tatizo la ukosefu wa maji safi na salama kuimbwa kwa miaka 50. Haiwezekani katika taifa lililozungukwa na mito,maziwa na bahari kuwa na ukosefu huo,na wananchi wake wakubaliane na hali hiyo. Ni uwoga tu ndiyo unaweza kuelezea chanzo.

Vivyo hivyo kwenye umeme na barabara. Serikali imepewa dhamana na wananchi kukusanya kodi na kuzitumia kuleta ustawi wa maisha wa wananchi. Sasa kama hali haiko hivyo,ni nini chanzo cha kuendelea kuwa na serikali hiyo;uoga wa uthubutu ndiyo jibu.

Nafurahi kwa kiasi fulani,watanzania tumeanza kuwa wathubutu na kuachana na zama za uwoga. Ingawa jitihada zaidi zinahitajika.
 
Last edited by a moderator:
Marshall:

Nakubaliana na wewe kimsingi. Hili suala ya kuwa watanzania ni woga sioni kuwa lina umuhimu wake.

Kuna matatizo ya shule za serikali, kila mwenye nacho anapeleka mtoto kwenye shule za kulipia zingine zikiwa Kenya.

Kuna matatizo ya maji kila mwenye uwezo ananunua simtank.

Kuna matatizo umeme mwenye uwezo ananunua generator.

Kuna matatizo ya barabara mbovu mwenye uwezo ananunua SUV.

Kuna uhaba wa sukari, watu watakunywa uji wa chumvi.

Hatuwezi kujenga nchi kwa kutafuta ufumbuzi wa binafsi kwenye masuala yanayotakiwa masuala ya jumla.

Chief Zakumi, bado unaamini katika hayo uliyoyaandika?

Kama ndiyo,napingana nawe. Kwani katika hayo yote uliyoyasema juu ya utatuzi wa matatizo ya jamii katika mitizamo ya kibinafsi,lawama bado zinarudi kwetu sisi watanzania kwa kuendelea kuwa waoga na wazito wa kutaka kuiwajibisha na kuishurutisha serikali itatue matatizo hayo ili utatuzi huo uweze kuleta tija kwa mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Uwoga wetu ndiyo umepelekea kukubaliana na mipango ya isiyo endelevu ya serikali katika elimu -hususani shule za kata,mikopo katika vyuo vikuu,mitaala ya elimu n.k. - mipango isiyolenga kumwezesha mtoto wa kitanzania apate elimu itakayomwezesha aweze kukabiliana na matatizo yanayomzunguka yeye na taifa kwa ujumla.

Ni uwoga wetu pia wa kuziwajibisha serikali za CCM,ndiyo umepelekea tatizo la ukosefu wa maji safi na salama kuimbwa kwa miaka 50. Haiwezekani katika taifa lililozungukwa na mito,maziwa na bahari kuwa na ukosefu huo,na wananchi wake wakubaliane na hali hiyo. Ni uwoga tu ndiyo unaweza kuelezea chanzo.

Vivyo hivyo kwenye umeme na barabara. Serikali imepewa dhamana na wananchi kukusanya kodi na kuzitumia kuleta ustawi wa maisha wa wananchi. Sasa kama hali haiko hivyo,ni nini chanzo cha kuendelea kuwa na serikali hiyo;uoga wa uthubutu ndiyo jibu.

Nafurahi kwa kiasi fulani,watanzania tumeanza kuwa wathubutu na kuachana na zama za uwoga. Ingawa jitihada zaidi zinahitajika.
 
Last edited by a moderator:
...Nakubaliana na Marehemu Shaaban Robert aliposema, "binadamu anahitaji ubongo wenye HEKIMA, moyo wenye USHUPAVU na ulimi (kauli) yenye UFASAHA" (tazama KUSADIKIKA). Kwa mtazamo wangu (na kwa mujibu wa Shaaban Robert) wananchi wa Tanzania (Watanzania) tunahitaji mapinduzi ya fikra. Kwa nini? Wengi, ubongo wetu (au bongo zetu) zimelala kwa uzezeta na hata tumekuwa wapinzani wa maendleeo yetu kwa ujinga na kutokujujua na kujijua kwamba hatujui. Huu ni msiba mkubwa kwa taifa la watu masikini ambao tumezongwa na UJINGA wa akili yenye uzezeta! Tazama; watu wanapinga hata maendeleo yao wenyewe kwa ujinga wa kudanganya pasipokuwa na utafiti na ithibati ya utafiti.

Pili, mioyo yetu imezama kwenye woga na kwa woga wetu wa kijinga tunawaacha watu wachache wafanye badala yetu huku wakifanya ubadhirifu wa aina zote. Tunatunga sheria huku tunazivunja kwa inda, chuki na kedi huku watu wachache wakitafuna vya umma na wengine wakishangilia utafunaji huo...halafu wanajifanya wao ni wanaharakati (tena kwa kutumia imani zao) tumekuwa kama misukule tusiojua nani aliyetoroga; kama tumerogwa na woga wa kijinga na tumekuwa kama watu wasiyokuwa na imani ya kujitambua na utambuzi.

Tatu, na tunapozungumza na au kusema (tunapohambarara) tunaropoka kama KASUKU bila ufasaha wa kile tunachozungumza! Hali hii imenifanya nijistukie; na nijichunguze na kuwachunguza wenzangu tumekosa nini? Nadhaani tunahitaji kujitafakari na au kujitazama upya. Mapinduzi ya fikra ni muhimu katina kuzigeuza fikra zetu ili ziwe chanya na zikubali mabadiliko ya HEKIMA, USHUPAVU na UFASAHA. Lazima tuone mbele kwa macho angavu!
 
kitendo cha waislamu kugomea sensa ni rais wa tz ndiye wa kulaumiwa sababu sheikh ponda ni muumini mwenzake rais na anashindwa kuwachukulia hatua kama alivyofanya kwa mgomo wa madaktari na walimu huu ni uzembe na udhaifu wa kikkwete kama rais anaweka dini mbele kuliko taifa anaamini katika hilo ushahidi upo mwingi.na kama taifa hili litaingia kwenye vita ya kidini kiongozi atakayebeba mzogo huu ni jakaya kikwete.kama angelikuwa ni mchungaji mtikila kasema wakristo wasusie sensa basi manyang'au wa usalama wa taifa na polisi wangeshamuweka ndani mtikila sasa kikwete acha udini na ongoza taifa kwa misingi ya uongozi na si vinginevyo ubaguzi wa kidini utazikwa nao hata ukienda kaburini maan wewe ndie muanzilishi n​a unaendekeza.
 
hawa watu kwa sababu ccm na ye mwenyewe wamekuwa wakiwatumia waislamu kwa manufaa ya ccm sasa anogopa siri kuwekwa hadharani tumeone waislamu wengi viongozi mzee mwinyi aliwadhibiti akina ponda mzee makamba aliwadhibiti pale magomeni sasa kikwete kwa nini tusikuone wewe ni swahiba na unawafurahia kwa sababu wanafanya kazi abayo ndani ya moyo wako unachekelea lakini kumnuka vita ya kidini haitamuacha salma ridhiwani wala ndugu yako yeyote acha udini ongoza nchi nyerere aliyuonya watanzania kukuchagua sasa tunaona faida zake
 
Chief Zakumi, bado unaamini katika hayo uliyoyaandika?

Kama ndiyo,napingana nawe. Kwani katika hayo yote uliyoyasema juu ya utatuzi wa matatizo ya jamii katika mitizamo ya kibinafsi,lawama bado zinarudi kwetu sisi watanzania kwa kuendelea kuwa waoga na wazito wa kutaka kuiwajibisha na kuishurutisha serikali itatue matatizo hayo ili utatuzi huo uweze kuleta tija kwa mtu mmoja na taifa kwa ujumla.

Uwoga wetu ndiyo umepelekea kukubaliana na mipango ya isiyo endelevu ya serikali katika elimu -hususani shule za kata,mikopo katika vyuo vikuu,mitaala ya elimu n.k. - mipango isiyolenga kumwezesha mtoto wa kitanzania apate elimu itakayomwezesha aweze kukabiliana na matatizo yanayomzunguka yeye na taifa kwa ujumla.

Ni uwoga wetu pia wa kuziwajibisha serikali za CCM,ndiyo umepelekea tatizo la ukosefu wa maji safi na salama kuimbwa kwa miaka 50. Haiwezekani katika taifa lililozungukwa na mito,maziwa na bahari kuwa na ukosefu huo,na wananchi wake wakubaliane na hali hiyo. Ni uwoga tu ndiyo unaweza kuelezea chanzo.

Vivyo hivyo kwenye umeme na barabara. Serikali imepewa dhamana na wananchi kukusanya kodi na kuzitumia kuleta ustawi wa maisha wa wananchi. Sasa kama hali haiko hivyo,ni nini chanzo cha kuendelea kuwa na serikali hiyo;uoga wa uthubutu ndiyo jibu.

Nafurahi kwa kiasi fulani,watanzania tumeanza kuwa wathubutu na kuachana na zama za uwoga. Ingawa jitihada zaidi zinahitajika.

Nzi !!!!!!!!!,

Holy ****. I posted that one long time before the 2010 election and the Arab Spring. To be honest with you, my position have shifted.
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Marshall:

Nakubaliana na wewe kimsingi. Hili suala ya kuwa watanzania ni woga sioni kuwa lina umuhimu wake.

Wakati nchi ina matatizo ya ajira kitu cha kwanza nilichukua visa na kuja kuishi Marekani.

Kuna matatizo ya shule za serikali, kila mwenye nacho anapeleka mtoto kwenye shule za kulipia zingine zikiwa Kenya.

Kuna matatizo ya maji kila mwenye uwezo ananunua simtank.

Kuna matatizo umeme mwenye uwezo ananunua generator.

Kuna matatizo ya barabara mbovu mwenye uwezo ananunua SUV.

Kuna uhaba wa sukari, watu watakunywa uji wa chumvi.

Kuna uhaba wa bia, watu watakunywa chibuku.

Hatuwezi kujenga nchi kwa kutafuta ufumbuzi wa binafsi kwenye masuala yanayotakiwa masuala ya jumla.

Maneno mazito
 
Duh, watu kwa kuchimbua! Haya nimeyaandika mwaka 2008 lakini bahati mbaya kama wote tunavyoshuhudia leo hii hakujabadilika kitu. Wachache wetu tulioupa uwoga mgongo na kuweza kupata ujasiri wa kuiasi CCM hivi sasa tumegeuziwa kibao; eti sisi ndio tunaitwa misukule! Tunaitwa hivyo na nani? Tunaitwa hivyo na wale wale ambao bado ni watiifu wa kwa Raisi dhaifu na serikali dhaifu chini ya chama cha kifisadi CCM, wanaendelea kuuenzi uongozi ule ule, mfumo ule ule na sera zile zile zilizosababisha hali hiyo. Bado wana matumaini na BRN...kweli usukule umepewa maana nyingine kabisa!
 
Watanganyika daima hujifanya wao ni Taifa teule na limepewa amri na Mungu ya kukutawala

Utasikia wakisema"tutawatawala mpaka Kiama"
Katika hali halisi wao wenyewe ni watu wasiojielewa wala kujitambua
Tukio la hivi juzi ndio wameiwacha vinywa wazi Dunia baada vichwa maji hawa kuanda walicho kiita Maandamano KUISHINDIKIZA SERIKALI YA S.A iiwachie Ndege yao
Tangannyika THINKING CAPACITY yao ipo chini sana kuliko Nchi yoyote ktk Bara hili

Kisha mpuzi mmoja anakuja kisema hapa "Tukiwaachia mjitawale mtaa CHINJANA KM KUKU"
Wakati kumbe akilizenu zipo chini kuliko KUKU
Hamjui Duniani ktk Nchi zinazojielewa kuna mihmili mitatu
1 SERIKALI
2 BUNGE
3 MAHAKAMA
ZidIsheni kuidai haki zenu kwa kuandamana.
Duh twaona aibu kunasibishwa na nyinyi munafanya sote tuonekane VICHWA PANZI
MUNAFELI WAPI WADANGANYIKA?
 
Watanganyika daima hujifanya wao ni Taifa teule na limepewa amri na Mungu ya kukutawala

Utasikia wakisema"tutawatawala mpaka Kiama"
Katika hali halisi wao wenyewe ni watu wasiojielewa wala kujitambua
Tukio la hivi juzi ndio wameiwacha vinywa wazi Dunia baada vichwa maji hawa kuanda walicho kiita Maandamano KUISHINDIKIZA SERIKALI YA S.A iiwachie Ndege yao
Tangannyika THINKING CAPACITY yao ipo chini sana kuliko Nchi yoyote ktk Bara hili

Kisha mpuzi mmoja anakuja kisema hapa "Tukiwaachia mjitawale mtaa CHINJANA KM KUKU"
Wakati kumbe akilizenu zipo chini kuliko KUKU
Hamjui Duniani ktk Nchi zinazojielewa kuna mihmili mitatu
1 SERIKALI
2 BUNGE
3 MAHAKAMA
ZidIsheni kuidai haki zenu kwa kuandamana.
Duh twaona aibu kunasibishwa na nyinyi munafanya sote tuonekane VICHWA PANZI
MUNAFELI WAPI WADANGANYIKA?
Bashite aka makonda aliyefail hana vyeti ndo anamshauri jiwe.jiwe anamwona bashite ndo jembe
 
Back
Top Bottom