Wizi wa wanyama kutumia ndege ya kijeshi: Hili ni suala la Rais kutueleza kilichojiri

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,129
18,743
Jambo moja linaloniudhi kila siku ni jinsi watanzania tunavyochukuliwa kuwa malofa na mataifa mengine. Habari iliyopo katika magazeti ya Guardian Ltd ni kwamba Qatar walitumia ndege ya kijeshi kuiba wanyama toka Tanzania, ndege iliyotua pale KIA na kuondoka majira ya alfajiri na mapema na wanyama 116.

Hili si jambo ndogo. Ni uhaini wa hali ya juu kwamba ndege ya jeshi la nchi nyingine inaweza kuingia kinyemela nchini na kuondoka. Nani katika jeshi alitoa kibali cha ndege hiyo si tu kuingia anga la Tanzania bali hata kutua, kwa mamlaka ya nani? Ina maana ndege kubwa ya jeshi jingine inaweza kutua nchini bila JK, raisi wa nchi kuwa na taarifa? Na kama raisi alijua aliambiwa inakuja kufanya nini? Na huko Qatar, nani aliruhusu hiyo ndege ya jeshi kuja Tanzania kuchukua wanyama? Nani katika jeshi au serikali za Tanzania na Qatar walijua? Au labda Maige amesema kweli kwamba katolewa kafara?

Inakuwaje nchi inaruhusu hali ambayo inaweza hata kuingiza askari mamluki (mercanaries) kwa kutumia ndege kubwa ya kijeshi na wala lolote lisifanyike? Viongozi wanatenda kulingana na kiapo cha ofisi walichofanya?

Kweli Tanzania tumefikia hatua kama hii ambapo nchi inakuwa kama haina wenye nayo?


attachment.php


Ndege ya kijeshi ya Qatar iliyotumika kuiba wanyama Tanzania pale KIA

Source: IPP Media
 

Attachments

  • New Picture Q.png
    New Picture Q.png
    42.9 KB · Views: 396
Kinachouma zaidi ni kuwa mpaka leo hakuna aliyepanda kizimabani kujibu hili,ukiuliza utamabiwa ‘tumeunda tume' ili wale zaidi au ‘uchunguzi haujakamilika' kama siyo- ‘hakuna ushahidi!!. Mungu tuponye na machungu haya. Mambo haya ndiyo yanayoua uzalendo halafu wanatafuta mchawi- Nape kwa haya kuwaambia watanzania wavae uzalendo ni matusi ya rejareja kama siyo dharua ya hali ya juu.
 
jambo moja linaloniudhi kila siku ni jinsi watanzania tunavyochukuliwa kuwa malofa na mataifa mengine. Habari iliyopo katika magazeti ya guardian ltd ni kwamba qatar walitumia ndege ya kijeshi kuiba wanyama toka tanzania, ndege iliyotua pale kia na kuondoka majira ya alfajiri na mapema na wanyama 116.

Hili si jambo ndogo. Ni uhaini wa hali ya juu kwamba ndege ya jeshi la nchi nyingine inaweza kuingia kinyemela nchini na kuondoka. Nani katika jeshi alitoa kibali cha ndege hiyo si tu kuingia anga la tanzania bali hata kutua, kwa mamlaka ya nani? Ina maana ndege kubwa ya jeshi jingine inaweza kutua nchini bila jk, raisi wa nchi kuwa na taarifa? Na kama raisi alijua aliambiwa inakuja kufanya nini? Na huko qatar, nani aliruhusu hiyo ndege ya jeshi kuja tanzania kuchukua wanyama? Nani katika jeshi au serikali za tanzania na qatar walijua? Au labda maige amesema kweli kwamba katolewa kafara?

Inakuwaje nchi inaruhusu hali ambayo inaweza hata kuingiza askari mamluki (mercanaries) kwa kutumia ndege kubwa ya kijeshi na wala lolote lisifanyike? Viongozi wanatenda kulingana na kiapo cha ofisi walichofanya?

Kweli tanzania tumefikia hatua kama hii ambapo nchi inakuwa kama haina wenye nayo?


View attachment 56608
ndege ya kijeshi ya qatar iliyotumika kuiba wanyama tanzania pale kia

source: Ipp media


mkuu mleta uzi, hizi habari zilitokea mwaka 2010, wakati tunakaribia uchaguzi, kwakweli kuna maswali mengisana zaidi ya hayo uliyojiuliza, zaidi inaonyesha hatuna haja ya kuwa na watu takribini 150,000 wa usalama, ni ushenzi tupu... Hiyo kashifa kwa ichi hata kenya hapo ilikuwa inaondoka na watu wengi vibaya mno, ila kwa tatnzania yoote ni upepo tu yatapita... Na kama unavyoona yanapita kweli. Hakuna haja ya kuwa na watu wa usalama kama hawako tayari kuilinda nchi yetu... Tanzania kuna kila aina ya uozo..na siku hii serikali ikiondoka ndio tutayajua mengi zaidi.. Ila mpaka kuondoka kwake, watu wengi watapoteza maisha.... Ukiiwaza sana nchii yetu na yanayotekea na hatua zinazochukuliwa waweza ingia msituni au kujitoa muhanga, nizaidi ya hasira, watu wanakufa kwa kukosa dawa, za tsh 5000, huku leo kunakigogo anapata allowance ya 80,000,000/= kwa mwezi
 
mkuu mleta uzi, hizi habari zilitokea mwaka 2010, wakati tunakaribia uchaguzi, kwakweli kuna maswali mengisana zaidi ya hayo uliyojiuliza, zaidi inaonyesha hatuna haja ya kuwa na watu takribini 150,000 wa usalama, ni ushenzi tupu...


Mkuu Committed, nimeshangaa sana hata upinzani haukulivalia njuga suala hili, labda habari imefunguka zaidi baada ya taarifa kwamba hawa wanyama walienda Qatar, ambayo imetoka juzi tu hapa. Kweli inaudhi. Nasikia wanyama wengine walipelekwa Pakistan, pamoja na tembo wanne sijui.
 
yani hili halina haja ya kuombwa kuachia ngazi!tatizo nguzo zetu za uongoz hazijielew,mbunge anataka 1 mil kwa halmashaur akipewa kama mil 100 za twiga si ndo hta mtoto wake ataozesha oman kwa sheria aliyoitunga mwenyewe bungen!
 
na Ahmed Makongo, Bunda


amka2.gif
WATU watatu wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja na Mahakama ya Wilaya ya Bunda, mkoani Mara baada ya kupatikana na hatia ya kuua pundamilia ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kinyume cha sheria.
Hakimu Mkazi Mwandamizi, Joackim Tiganga alisema jana kuwa ametoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka mahakamani hapo.
Hakimu Tiganga, alisema ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwao na kwa watu wengine wenye tabia na nia ya kuwinda wanyama kinyume cha sheria.
Waliohukumiwa kiungo hicho ni Joseph Lazaro, Inocent Amos na Emmanuel Juma, wote wakazi wa Kijiji cha Kunzugu, wilayani hapa.
Awali, Mwendesha Mashitaka wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mwanasheria Emmanuel Zumba, alidai washitakiwa hao walikamatwa na askari wa hifadhi hiyo, wakiwa wanawinda wanyama kwa kuwafukuza na pikipiki, na kisha kuwashambulia kwa silaha za jadi.
Alidai washitakiwa wote walikamatwa wakiwa wameshaua pundamilia mmoja mwenye thamani ya sh 510,000.

 
na Ahmed Makongo, Bunda


amka2.gif
WATU watatu wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kila mmoja na Mahakama ya Wilaya ya Bunda, mkoani Mara baada ya kupatikana na hatia ya kuua pundamilia ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kinyume cha sheria.
Hakimu Mkazi Mwandamizi, Joackim Tiganga alisema jana kuwa ametoa adhabu hiyo baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka mahakamani hapo.
Hakimu Tiganga, alisema ametoa adhabu hiyo ili iwe fundisho kwao na kwa watu wengine wenye tabia na nia ya kuwinda wanyama kinyume cha sheria.
Waliohukumiwa kiungo hicho ni Joseph Lazaro, Inocent Amos na Emmanuel Juma, wote wakazi wa Kijiji cha Kunzugu, wilayani hapa.
Awali, Mwendesha Mashitaka wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Mwanasheria Emmanuel Zumba, alidai washitakiwa hao walikamatwa na askari wa hifadhi hiyo, wakiwa wanawinda wanyama kwa kuwafukuza na pikipiki, na kisha kuwashambulia kwa silaha za jadi.
Alidai washitakiwa wote walikamatwa wakiwa wameshaua pundamilia mmoja mwenye thamani ya sh 510,000.
 
ILi suala la hawa wanyama unaweza ambulia ulcers ebu acheni pls.
Ivi nilidhani hawa ambao waliudhuria ata JKT ndo wangekuwa wazalendo.
Kweli nimeamini kuna watu walikuwa wanasubiri Mwalimu afe ili waharibu!
 
Kiongozi,hili suala lisiwaumize kichwa sana nchi hii ishauzwa. Hii issue ilisukwa na wakubwa wote wanahusika including viongozi wa vyama vya upinzani wanajua na walihusika kwa asilimia zote. Hivi hamuoni kwamba pamoja na ufukunyuaji maovu wote unaofanywa na chadema hawajawahi kulivalia njuga hili swala? The deal was in the making way back in 2009 Dr.Slaa akiwa bado mbunge tena machachari kabisa wa kupinga ufisadi na ubadhilifu. Msiumize vichwa bana tujadili mambo mengine. Wote Slaa,Mbowe,Zitto wanajua na waliupokea mgao wao vizuri sana. Asante.
Mkuu Committed, nimeshangaa sana hata upinzani haukulivalia njuga suala hili, labda habari imefunguka zaidi baada ya taarifa kwamba hawa wanyama walienda Qatar, ambayo imetoka juzi tu hapa. Kweli inaudhi. Nasikia wanyama wengine walipelekwa Pakistan, pamoja na tembo wanne sijui.
 
Kwa hili JK ana kesi ya kujibu.

Angetumia maongezi ya mwisho wa mwezi kutueleza wananchi kuhusu twiga maana wanatafuta sababu ya kuchukiwa ccm wakati kilamtu kachoka, Okampo anatakiwa achunguze hili, Maige aseme ukweli bora afunguke tumwelewe.
 
Huyo ni Jakaya Kikwete tu na uswahiba wake nchi za kiislam kawaruhusu waje wachukue wanyama anayebisha ambane vzuri Maige amsikie
 
...raisi yupi unayetaka atuambie kilichojiri mpaka wanyama wetu wakatoroshwa kwenda Quatar? Unamaanisha huyuhuyu mhongwa suti tano ili kuuza Kilimanjaro Hotel?
 
Kwa mtazamo wangu katika hili, wasio na hatia watatolewa kafara bure. Ni swala kubwa sana ambalo mamlaka kuu zimehusika. haiwezekani swala linalogusa usalama wa nchi na uhujumu uchumi, wanyama zaidi ya mia...???..
 
Back
Top Bottom