Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,436
- 4,429
Kwa siku kadhaa sasa, wizi wa kutisha unafanywa na raia wa kigeni katika benki kadhaa nchini, hasa NBC. Akaunti za wateja wengi zimekombwa kabisa fedha, na sasa kuna malalamiko mengi kutoka kwa wateja. Washiriki wa wizi huu ni raia wa Afrika Magharibi, hasa Nigeria na baadhi ya wazungu kutoka mataifa ya Ulaya. Benki ya NBC imeanza taratibu za kuwarejeshea fedha baadhi wa wateja waliolizwa. Nina ndugu yangu ambaye asubuhi hii kaibiwa Sh milioni 4.65.